WIMBO NA. 7
Yehova, Nguvu Yetu
1. Yah mwenye fadhili, nguvu yetu,
Twakupenda, U Mwokozi wetu.
Twazitangaza habari zako,
Wasikie ama wakatae.
(KORASI)
Yehova Mwamba, na nguvu yetu,
Twalitangaza jina lako.
Yehova mkuu, mwenye nguvu,
U mnara wetu; ngome yetu.
2. Tunashangilia nuru yako;
Twaiona kweli waziwazi.
Tunajifunza sheria zako;
Twautetea Ufalme wako.
(KORASI)
Yehova Mwamba, na nguvu yetu,
Twalitangaza jina lako.
Yehova mkuu, mwenye nguvu,
U mnara wetu; ngome yetu.
3. Tunayafanya mapenzi yako,
Licha ya dhihaka za Shetani.
Hata iwe twakabili kifo,
Hadi mwisho tuwe wa’minifu.
(KORASI)
Yehova Mwamba, na nguvu yetu,
Twalitangaza jina lako.
Yehova mkuu, mwenye nguvu,
U mnara wetu; ngome yetu.
(Ona pia 2 Sam. 22:3; Zab. 18:2; Isa. 43:12.)