Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl uku. 3
  • Utangulizi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utangulizi
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl uku. 3

Utangulizi

Kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo kitakusaidia kupata mistari ya Biblia na masimulizi yatakayokusaidia kukabiliana na changamoto maishani. Pia, kitakusaidia kutafuta mistari hususa ya Biblia ambayo itawatia moyo wengine na kuwasaidia kufanya maamuzi yanayomletea heshima Yehova. Tafuta kichwa unachotaka. Kila kichwa kina maswali mazuri na maelezo mafupi kuhusu masimulizi ya Biblia yatakayokuongoza. (Tazama sanduku “Jinsi ya Kutumia Kitabu Hiki.”) Utapata kwa wingi ushauri, mwongozo, na faraja unayohitaji kutoka katika Neno la Mungu. Pia, utapata hazina unazoweza kushiriki na wengine, yaani, mistari ya Biblia itakayowaburudisha, itakayowasaidia kutatua matatizo yao, na kuwapatia ushauri na kuwatia moyo.

Jinsi ya Kutumia Kitabu Hiki

Ili kupata kichwa unachotaka, unaweza kutumia sehemu ya tafuta, au unaweza kutumia mpangilio wa vikundi. Kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo kimegawanywa katika vikundi vikubwa saba: Changamoto, Familia, Hali ya Kiroho, Kutaniko, Maisha ya Kila Siku, Mwenendo, na Sifa. Vichwa vingi vinapatikana katika vikundi hivyo. Chagua kikundi unachotaka, na utazame orodha ya vichwa vilivyopo. Hata hivyo, ikiwa huna uhakika kichwa unachotafuta kinapatikana katika kikundi gani, chagua Vyote na utazame orodha ya vichwa vyote hadi utakapopata kichwa unachohitaji. Chini ya kila kichwa, utaona vichwa vidogo kadhaa vyenye wino mzito. Baadhi ya vichwa hivyo ni maelezo; vingine ni maswali. Unaposoma maandiko yaliyorejelewa yenye wino mzito ambayo yanafuata baada ya vichwa hivyo vidogo, tafakari jinsi maandiko hayo yanavyounga mkono maelezo au kujibu maswali hayo. Katika visa fulani, kichwa kimegawanywa katika sehemu mbalimbali ili kukusaidia kutafuta haraka zaidi habari unayohitaji. Katika baadhi ya visa, Maandiko ya “Tazama pia” yanapatikana. Maandiko hayo yana habari zinazohusiana na kichwa unachochunguza. Katika visa vingi, utapata pia orodha ya maandiko ya “Masimulizi ya Biblia yanayohusika.” Baada ya maandiko hayo kuna sentensi inayofafanua kwa ufupi maandiko hayo. Unaposoma maandiko hayo, tumia sentensi hizo kukuongoza unapotafakari.

Kitabu hiki hakiorodheshi maandiko yote yanayohusu habari au kichwa fulani. Lakini ni kitabu kizuri kitakachokusaidia kuanza kufanya utafiti wako. (Met 2:​1-6) Ili kufanya utafiti wa kina zaidi, tumia marejeo ya pambizoni katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, na hata habari za utafiti (study notes) ikiwa zinapatikana katika lugha nyingine unayoelewa. Tumia Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova au Fahirisi ili kujifunza kikamili zaidi maana ya andiko fulani na matumizi yake. Soma machapisho ya karibuni zaidi ili kuhakikisha kwamba una uelewaji wa karibuni wa kweli za Kimaandiko.

Acheni kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo kiwasaidie kupata hekima, ujuzi, na uelewaji unaopatikana katika Maandiko Matakatifu. Unapotumia kitabu hiki, utasadiki hata zaidi kwamba “neno la Mungu liko hai nalo ni lenye nguvu.”—Ebr 4:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki