Sherehe
Sherehe ambazo Wakristo wanashiriki
Sherehe pekee ambayo Wakristo wanapaswa kushiriki ni ipi?
Watu wa Mungu wanafurahia kukusanyika kwa ajili ya ibada
Simulizi la Biblia linalohusika:
2Nya 30:1, 6, 13, 14, 18-27—Mfalme Hezekia anapanga sherehe ya pekee ya Pasaka
Sherehe ambazo Wakristo huepuka
Kwa nini ni kosa kushiriki katika sherehe ambayo inahusiana na dini ya uwongo?
1Ko 10:21; 2Ko 6:14-18; Efe 5:10, 11
Tazama pia “Kuchanganya Ibada”
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Kut 32:1-10—Waisraeli wanamkasirisha Yehova wanapochanganya ibada ya kweli na ya uwongo
Hes 25:1-9—Yehova anawaadhibu watu wake kwa kushiriki katika sherehe za dini ya kipagani na kufanya uasherati
Je, Krismasi ni sherehe ya Kikristo?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Lu 2:1-5—Yesu azaliwa wakati wa kuhesabiwa kwa watu; inaelekea Waroma hawangewaambia Wayahudi waasi waliowatawala wasafiri kwa ajili ya kuhesabiwa wakati wa majira ya baridi na mvua
Lu 2:8, 12—Yesu anapozaliwa, wachungaji walikuwa wakiishi nje, jambo ambalo hawangefanya katika majira ya baridi ya mwezi wa Desemba
Je, Wakristo wanapaswa kusherehekea siku za kuzaliwa?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 40:20-22—Farao mpagani anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ambayo inatia ndani mauaji
Mt 14:6-11—Mfalme Herode, mpinzani mwovu wa wafuasi wa Kristo, anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ambayo inafanya Yohana Mbatizaji auawe
Sherehe zinazotegemea Sheria ya Musa
Je, matakwa ya Sheria ya Musa, kutia ndani sherehe mbalimbali, yanawahusu Wakristo?
Tazama pia Gal 4:4, 5, 9-11; Ebr 8:7-13; 9:1-3, 9, 10, 24
Je, Wakristo wanapaswa kushika Sabato ya kila juma?
Tazama pia Kut 31:16, 17
Sherehe za kitaifa
Je, Wakristo wanapaswa kusherehekea matukio ya kihistoria yanayohusu siasa za taifa?
Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika sherehe za kitaifa zinazoadhimisha ushindi wa kivita?
Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika sherehe zinazowatukuza na kuwaabudu watu mashuhuri?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 12:21-23—Mungu alimwadhibu Mfalme Herode Agripa wa Kwanza kwa sababu alikubali kuabudiwa na watu
Mdo 14:11-15—Mtume Barnaba na Paulo wanakataa kuabudiwa
Ufu 22:8, 9—Malaika wa Yehova anakataa kuabudiwa