Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 89-90
  • Sherehe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sherehe
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 89-90

Sherehe

Sherehe ambazo Wakristo wanashiriki

Sherehe pekee ambayo Wakristo wanapaswa kushiriki ni ipi?

Lu 22:19; 1Ko 11:​23-26

Watu wa Mungu wanafurahia kukusanyika kwa ajili ya ibada

Kum 31:12; Ebr 10:​24, 25

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • 2Nya 30:​1, 6, 13, 14, 18-27—Mfalme Hezekia anapanga sherehe ya pekee ya Pasaka

Sherehe ambazo Wakristo huepuka

Kwa nini ni kosa kushiriki katika sherehe ambayo inahusiana na dini ya uwongo?

1Ko 10:21; 2Ko 6:​14-18; Efe 5:​10, 11

Tazama pia “Kuchanganya Ibada”

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kut 32:​1-10—Waisraeli wanamkasirisha Yehova wanapochanganya ibada ya kweli na ya uwongo

    • Hes 25:​1-9—Yehova anawaadhibu watu wake kwa kushiriki katika sherehe za dini ya kipagani na kufanya uasherati

Je, Krismasi ni sherehe ya Kikristo?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 2:​1-5—Yesu azaliwa wakati wa kuhesabiwa kwa watu; inaelekea Waroma hawangewaambia Wayahudi waasi waliowatawala wasafiri kwa ajili ya kuhesabiwa wakati wa majira ya baridi na mvua

    • Lu 2:​8, 12—Yesu anapozaliwa, wachungaji walikuwa wakiishi nje, jambo ambalo hawangefanya katika majira ya baridi ya mwezi wa Desemba

Je, Wakristo wanapaswa kusherehekea siku za kuzaliwa?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 40:​20-22—Farao mpagani anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ambayo inatia ndani mauaji

    • Mt 14:​6-11—Mfalme Herode, mpinzani mwovu wa wafuasi wa Kristo, anasherehekea siku yake ya kuzaliwa, ambayo inafanya Yohana Mbatizaji auawe

Sherehe zinazotegemea Sheria ya Musa

Je, matakwa ya Sheria ya Musa, kutia ndani sherehe mbalimbali, yanawahusu Wakristo?

Ro 10:4; Efe 2:15

Tazama pia Gal 4:​4, 5, 9-11; Ebr 8:​7-13; 9:​1-3, 9, 10, 24

Je, Wakristo wanapaswa kushika Sabato ya kila juma?

Kol 2:​16, 17

Tazama pia Kut 31:​16, 17

Sherehe za kitaifa

Je, Wakristo wanapaswa kusherehekea matukio ya kihistoria yanayohusu siasa za taifa?

Yoh 15:19; 18:36; Yak 4:4

Tazama pia “Serikali—Wakristo Wanadumisha Msimamo wa Kutounga Mkono Upande Wowote”

Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika sherehe za kitaifa zinazoadhimisha ushindi wa kivita?

Zb 11:5; Isa 2:4

Tazama pia “Serikali—Wakristo Wanadumisha Msimamo wa Kutounga Mkono Upande Wowote” na “Vita”

Je, Wakristo wanapaswa kushiriki katika sherehe zinazowatukuza na kuwaabudu watu mashuhuri?

Kut 20:5; Ro 1:25

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mdo 12:​21-23—Mungu alimwadhibu Mfalme Herode Agripa wa Kwanza kwa sababu alikubali kuabudiwa na watu

    • Mdo 14:​11-15—Mtume Barnaba na Paulo wanakataa kuabudiwa

    • Ufu 22:​8, 9—Malaika wa Yehova anakataa kuabudiwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki