Wakfu
Ni sababu gani inayofaa ya kujiweka wakfu kwa Yehova Mungu?
Kum 6:5; Lu 10:25-28; Ufu 4:11
Tazama pia Kut 20:5
Ikiwa tunataka kumtumikia Mungu, tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu Biblia?
Zb 119:105; 1Th 2:13; 2Ti 3:16
Tazama pia Yoh 17:17; Ebr 4:12
Ni lazima tutambue jambo gani kuhusu njia ya Mungu ya kutusaidia kushinda dhambi?
Kutubu mambo tuliyofanya katika maisha yetu ya awali kunahusisha nini?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Lu 19:1-10—Mkuu wa wakusanya kodi, Zakayo, anatubu kwa sababu ya maisha yake ya unyang’anyi na anarudisha pesa za watu aliowadhulumu
1Ti 1:12-16—Mtume Paulo anaeleza jinsi alivyoacha maisha ya dhambi na kupata msamaha kupitia rehema ya Mungu na Kristo
Zaidi ya kuacha matendo mabaya, ni nini kingine tunachopaswa kufanya?
Ni viwango gani vya maadili tunavyopaswa kufuata ili kumtumikia Mungu kwa njia inayokubalika?
1Ko 6:9-11; Kol 3:5-9; 1Pe 1:14, 15; 4:3, 4
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Ko 5:1-13—Mtume Paulo analiagiza kutaniko la Korintho limwondoe mwanamume ambaye ana hatia ya kufanya uasherati wa kupindukia
2Ti 2:16-19—Mtume Paulo anamwonya Timotheo akatae maneno ya waasi-imani, ambayo ni kama kidonda kinachooza
Watumishi wa Mungu wanahitaji kuchukua msimamo gani kuhusu mambo ya ulimwengu huu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Yoh 6:10-15—Baada ya Yesu kufanya muujiza wa kuulisha umati mkubwa, watu wanamtafuta ili kumfanya awe mfalme, lakini Yesu anawatoroka
Yoh 18:33-36—Yesu anafafanua kwamba Ufalme wake hauhusiani na siasa za ulimwengu huu
Roho takatifu inatusaidiaje kumtumikia Mungu?
Tazama pia Mdo 20:28; Efe 5:18
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mdo 15:28, 29—Baraza linaloongoza lililo jijini Yerusalemu linaongozwa na roho takatifu kufanya uamuzi muhimu kuhusu suala la tohara
Ni katika njia gani tunaweza kumtumikia Mungu kama alivyofanya Yesu Kristo?
Kwa nini Wakristo waliojiweka wakfu wanahitaji kubatizwa?
Mt 28:19, 20; Mdo 2:40, 41; 8:12; 1Pe 3:21
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 3:13-17—Yesu anajitoa kufanya mapenzi ya Baba yake, anaonyesha hilo kwa kubatizwa
Mdo 8:26-39—Ofisa Mwethiopia, ambaye tayari ni Myahudi mgeuzwa-imani, yuko tayari kubatizwa baada ya kujifunza ukweli kumhusu Yesu Kristo