Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 114-115
  • Wakfu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakfu
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 114-115

Wakfu

Ni sababu gani inayofaa ya kujiweka wakfu kwa Yehova Mungu?

Kum 6:5; Lu 10:​25-28; Ufu 4:11

Tazama pia Kut 20:5

Ikiwa tunataka kumtumikia Mungu, tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu Biblia?

Zb 119:105; 1Th 2:13; 2Ti 3:16

Tazama pia Yoh 17:17; Ebr 4:12

Ni lazima tutambue jambo gani kuhusu njia ya Mungu ya kutusaidia kushinda dhambi?

Yoh 14:6; Mdo 4:12; Ro 3:23; Gal 1:4; Efe 1:7

Kutubu mambo tuliyofanya katika maisha yetu ya awali kunahusisha nini?

Mdo 3:19; 26:20

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 19:​1-10—Mkuu wa wakusanya kodi, Zakayo, anatubu kwa sababu ya maisha yake ya unyang’anyi na anarudisha pesa za watu aliowadhulumu

    • 1Ti 1:​12-16—Mtume Paulo anaeleza jinsi alivyoacha maisha ya dhambi na kupata msamaha kupitia rehema ya Mungu na Kristo

Zaidi ya kuacha matendo mabaya, ni nini kingine tunachopaswa kufanya?

Ro 12:​1, 2; Efe 4:​17, 18, 22-24; 1Th 1:9

Ni viwango gani vya maadili tunavyopaswa kufuata ili kumtumikia Mungu kwa njia inayokubalika?

1Ko 6:​9-11; Kol 3:​5-9; 1Pe 1:​14, 15; 4:​3, 4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Ko 5:​1-13—Mtume Paulo analiagiza kutaniko la Korintho limwondoe mwanamume ambaye ana hatia ya kufanya uasherati wa kupindukia

    • 2Ti 2:​16-19—Mtume Paulo anamwonya Timotheo akatae maneno ya waasi-imani, ambayo ni kama kidonda kinachooza

Watumishi wa Mungu wanahitaji kuchukua msimamo gani kuhusu mambo ya ulimwengu huu?

Isa 2:​3, 4; Yoh 15:19

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yoh 6:​10-15—Baada ya Yesu kufanya muujiza wa kuulisha umati mkubwa, watu wanamtafuta ili kumfanya awe mfalme, lakini Yesu anawatoroka

    • Yoh 18:​33-36—Yesu anafafanua kwamba Ufalme wake hauhusiani na siasa za ulimwengu huu

Roho takatifu inatusaidiaje kumtumikia Mungu?

Yoh 16:13; Gal 5:​22, 23

Tazama pia Mdo 20:28; Efe 5:18

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mdo 15:​28, 29—Baraza linaloongoza lililo jijini Yerusalemu linaongozwa na roho takatifu kufanya uamuzi muhimu kuhusu suala la tohara

Ni katika njia gani tunaweza kumtumikia Mungu kama alivyofanya Yesu Kristo?

Mt 22:37; Yoh 4:34; 6:38; Ebr 10:​8, 9

Kwa nini Wakristo waliojiweka wakfu wanahitaji kubatizwa?

Mt 28:​19, 20; Mdo 2:​40, 41; 8:12; 1Pe 3:21

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mt 3:​13-17—Yesu anajitoa kufanya mapenzi ya Baba yake, anaonyesha hilo kwa kubatizwa

    • Mdo 8:​26-39—Ofisa Mwethiopia, ambaye tayari ni Myahudi mgeuzwa-imani, yuko tayari kubatizwa baada ya kujifunza ukweli kumhusu Yesu Kristo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki