Kutia Moyo
Kwa nini ni muhimu kwa watumishi wa Mungu kutiana moyo?
Isa 35:3, 4; Kol 3:16; 1Th 5:11; Ebr 3:13
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Nya 32:2-8—Watu wanapokabili tishio kubwa, Mfalme Hezekia anawatia moyo
Da 10:2, 8-11, 18, 19—Malaika alimtia moyo na kumwimarisha nabii Danieli alipozeeka na kukosa nguvu
Kwa nini Yehova anatarajia wazee wa kutaniko wawatie moyo wengine?
Tazama pia Mt 11:28-30
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Kum 3:28; 31:7, 8—Kama Yehova anavyoagiza, nabii Musa anamtia moyo na kumwimarisha Yoshua, atakayechukua nafasi yake
Mdo 11:22-26; 14:22—Wakati wa mateso, mtume Paulo na Barnaba wanawatia moyo Wakristo jijini Antiokia
Kwa nini pongezi ya kutoka moyoni ni sehemu muhimu ya kutia moyo?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Amu 11:37-40—Wanawake wa Israeli wanamtembelea binti ya Mwamuzi Yeftha kila mwaka, ili kumpongeza kwa kuondoka nyumbani na kwenda kutumikia katika hema la ibada
Ufu 2:1-4—Ingawa Yesu alihitaji kuwarekebisha Wakristo wa Efeso, aliwaeleza pia mambo mazuri waliyokuwa wakifanya
Watumishi waaminifu wa Yehova wanatiana moyo jinsi gani?
Met 15:23; Efe 4:29; Flp 1:13, 14; Kol 4:6; 1Th 5:14
Tazama pia 2Ko 7:13, 15, 16
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 23:16-18—Wakati wa hali ngumu Yonathani anamtafuta Daudi, rafiki yake, na kumtia moyo
Yoh 16:33—Yesu anawatia moyo wafuasi wake kupitia mfano wake na kuwahakikishia kwamba wao pia wanaweza kuwa washindi
Mdo 28:14-16—Alipokuwa akielekea Roma ili kesi yake isikilizwe, mtume Paulo alijipa moyo, alipowaona ndugu waaminifu ambao walisafiri ili kukutana naye na kumtia moyo
Kwa nini ni muhimu kuepuka roho ya kutokuwa na heshima au ya kulalamika?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Hes 11:10-15—Nabii Musa anavunjwa moyo sana na mtazamo usiofaa na wa kutotii wa watu
Hes 13:31, 32; 14:2-6—Habari mbaya za wapelelezi kumi wasio waaminifu zinawavunja moyo watu na kusababisha uasi
Kushirikiana na waabudu wenzetu kunawezaje kututia moyo?
Met 27:17; Ro 1:11, 12; Ebr 10:24, 25; 12:12
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Nya 20:1-19—Mfalme Yehoshafati anapokabili tishio kubwa kutoka kwa jeshi kubwa, anawakusanya watu pamoja ili wasali
Mdo 12:1-5, 12-17—Mtume Yakobo anapouawa, na mtume Petro kufungwa gerezani, washiriki wa kutaniko la Yerusalemu wanakutana pamoja ili kusali
Kufikiria mambo mazuri kunawezaje kututia moyo tuvumilie wakati wa hali ngumu?
Mdo 5:40, 41; Ro 8:35-39; 1Ko 4:11-13; 2Ko 4:16-18; 1Pe 1:6, 7
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mwa 39:19-23; 40:1-8—Ingawa anashtakiwa kwa uwongo na kufungwa isivyo haki, Yosefu anaendelea kuwa mwaminifu na anatamani kuwasaidia wengine
2Fa 6:15-17—Nabii Elisha hakuogopa jeshi lilipokuja dhidi yake, na alisali ili mtumishi wake pia asiogope
Kupata kitia moyo katika Neno la Yehova
Ni uhakikisho gani wenye upendo ambao Yehova anatoa?
Kwa nini tunafarijika tunapofikiria subira na rehema ya Yehova?
Yehova anaweza kuwafanyia nini wale wanaojihisi kuwa dhaifu?
Zb 46:1; Isa 12:2; 40:29-31; Flp 4:13
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 1:10, 11, 17, 18—Yehova alisikiliza sala ya Hana na kumsaidia apate kitulizo alipokuwa na mkazo na uchungu
1Fa 19:1-19—Nabii Eliya alipovunjika moyo, Yehova alimpatia msaada unaofaa. Alimtia moyo na kumfariji kwa kumpatia tumaini la wakati ujao
Tumaini la wakati ujao lililo katika Biblia linawezaje kutupatia ujasiri?
2Nya 15:7; Zb 27:13, 14; Ebr 6:17-19; 12:2
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ayu 14:1, 2, 7-9, 13-15—Hata alipovunjika moyo sana, Ayubu alifarijiwa na tumaini la ufufuo
Da 12:13—Nabii Danieli ambaye ana umri wa miaka 100 hivi, anatiwa moyo na malaika anayemweleza kuhusu baraka za wakati ujao
Kwa nini kusali kwa Yehova na kutafakari kumhusu kunaweza kututia moyo?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Sa 30:1-9—Mfalme Daudi anapokabili hali ngumu, anasali kwa Yehova na kupata nguvu
Lu 22:39-43—Anapokabili jaribu gumu zaidi, Yesu anasali kwa bidii, na Yehova anamjibu kwa kumtuma malaika amtie moyo
Ripoti nzuri zinawezaje kututia moyo, na kwa nini ni vizuri kushiriki na wengine ripoti nzuri?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 15:2-4—Mtume Paulo na Barnaba wanawaimarisha ndugu na dada katika makutaniko wanayotembelea
3Yo 1-4—Mtume Yohana aliyezeeka anatiwa moyo sana anaposikia kwamba wale aliowafundisha habari njema wanaendelea kuwa waaminifu