Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 21-22
  • Huzuni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Huzuni
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 21-22

Huzuni

Ni mifano gani ya Biblia inayoonyesha kwamba kuhuzunika mtu anapokufa ni jambo la kawaida?

Mwa 23:2; 24:67; 37:​34, 35; 42:36; Yoh 11:​19, 31, 33-36

Tazama pia 2Sa 1:​17-27; Mdo 9:​36-39

Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova anatamani kuwapatia faraja wale wanaoomboleza?

Zb 34:18; Isa 57:15; 61:​1, 2

Tunapata faraja gani tunapojua ukweli kuhusu hali ya wafu?

Mhu 9:​5, 10; 1Th 4:13

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 20:​37, 38—Yesu anaeleza kwamba tumaini la ufufuo ni hakika kabisa na kwa maoni ya Mungu ni kana kwamba wafu wako hai

    • Yoh 11:​5, 6, 11-14—Yesu anafananisha kifo na usingizi, baada ya kifo cha rafiki yake mpendwa, Lazaro

    • Ebr 2:​14, 15—Mtume Paulo anaeleza kwamba hatupaswi kuogopa kifo kupita kiasi

Kwa nini jina la mtu lina thamani kubwa zaidi wakati anapokufa?

Met 22:1; Mhu 7:​1, 2

Biblia inafafanuaje kifo, na Mungu atafanya nini kuhusu kifo?

Isa 25:8; 1Ko 15:26; Ufu 20:14; 21:​3, 4

Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba wakati ujao kutakuwa na ufufuo?

Isa 26:19; Yoh 5:​28, 29; Mdo 24:15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Biblia inataja kuhusu matukio tisa ya ufufuo, watu wanane walifufuliwa na kuishi duniani. Masimulizi hayo yote yanawapatia faraja na tumaini la wakati ujao wale wanaoomboleza

      • 1Fa 17:​17-24—Nabii Eliya anamfufua mwana wa mjane huko Sarefathi, mji uliopo Sidoni

      • 2Fa 4:​32-37—Nabii Elisha anamfufua mvulana katika mji wa Shunemu na kumkabidhi kwa wazazi wake

      • 2Fa 13:​20, 21—Mwanamume aliyekufa karibuni anafufuka mwili wake unapogusa mifupa ya nabii Elisha

      • Lu 7:​11-15—Katika jiji la Naini, Yesu anasimamisha msafara wa mazishi ili kumfufua mwana wa mjane

      • Lu 8:​41, 42, 49-56—Yesu anamfufua binti mdogo wa Yairo, ofisa msimamizi wa sinagogi

      • Yoh 11:​38-44—Yesu anamfufua Lazaro, rafiki yake mpendwa, na kumkabidhi kwa dada zake, Martha na Maria

      • Mdo 9:​36-42—Mtume Petro anamfufua Dorkasi, mwanamke Mkristo aliyependwa na aliyejulikana kwa matendo yake ya fadhili

      • Mdo 20:​7-12—Mtume Paulo anamfufua mwanamume kijana anayeitwa Eutiko, ambaye alikufa baada ya kuanguka chini kutoka dirishani

    • Yesu Kristo anafufuliwa akiwa kiumbe wa roho asiyeweza kufa, hivyo tunahakikishiwa kwamba ahadi zote za wakati ujao zitatimia

      • Mdo 17:31; 1Pe 3:18

    • Yesu ni wa kwanza kufufuliwa kwenda mbinguni na kupewa uhai usioweza kufa, lakini si wa mwisho; wafuasi wake watiwa-mafuta 144,000 watapata ufufuo kama wake

      • 1Ko 15:​20, 23, 51-53; 1Th 4:​16, 17; Ufu 14:1

Tunaweza kuwasaidiaje wale wanaohuzunika kwa sababu ya kufiwa na mpendwa wao?

Ro 12:15; 2Ko 1:​3, 4; 1Pe 3:8

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki