Huzuni
Ni mifano gani ya Biblia inayoonyesha kwamba kuhuzunika mtu anapokufa ni jambo la kawaida?
Mwa 23:2; 24:67; 37:34, 35; 42:36; Yoh 11:19, 31, 33-36
Tazama pia 2Sa 1:17-27; Mdo 9:36-39
Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova anatamani kuwapatia faraja wale wanaoomboleza?
Tunapata faraja gani tunapojua ukweli kuhusu hali ya wafu?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Lu 20:37, 38—Yesu anaeleza kwamba tumaini la ufufuo ni hakika kabisa na kwa maoni ya Mungu ni kana kwamba wafu wako hai
Yoh 11:5, 6, 11-14—Yesu anafananisha kifo na usingizi, baada ya kifo cha rafiki yake mpendwa, Lazaro
Ebr 2:14, 15—Mtume Paulo anaeleza kwamba hatupaswi kuogopa kifo kupita kiasi
Kwa nini jina la mtu lina thamani kubwa zaidi wakati anapokufa?
Biblia inafafanuaje kifo, na Mungu atafanya nini kuhusu kifo?
Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba wakati ujao kutakuwa na ufufuo?
Isa 26:19; Yoh 5:28, 29; Mdo 24:15
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Biblia inataja kuhusu matukio tisa ya ufufuo, watu wanane walifufuliwa na kuishi duniani. Masimulizi hayo yote yanawapatia faraja na tumaini la wakati ujao wale wanaoomboleza
1Fa 17:17-24—Nabii Eliya anamfufua mwana wa mjane huko Sarefathi, mji uliopo Sidoni
2Fa 4:32-37—Nabii Elisha anamfufua mvulana katika mji wa Shunemu na kumkabidhi kwa wazazi wake
2Fa 13:20, 21—Mwanamume aliyekufa karibuni anafufuka mwili wake unapogusa mifupa ya nabii Elisha
Lu 7:11-15—Katika jiji la Naini, Yesu anasimamisha msafara wa mazishi ili kumfufua mwana wa mjane
Lu 8:41, 42, 49-56—Yesu anamfufua binti mdogo wa Yairo, ofisa msimamizi wa sinagogi
Yoh 11:38-44—Yesu anamfufua Lazaro, rafiki yake mpendwa, na kumkabidhi kwa dada zake, Martha na Maria
Mdo 9:36-42—Mtume Petro anamfufua Dorkasi, mwanamke Mkristo aliyependwa na aliyejulikana kwa matendo yake ya fadhili
Mdo 20:7-12—Mtume Paulo anamfufua mwanamume kijana anayeitwa Eutiko, ambaye alikufa baada ya kuanguka chini kutoka dirishani
Yesu Kristo anafufuliwa akiwa kiumbe wa roho asiyeweza kufa, hivyo tunahakikishiwa kwamba ahadi zote za wakati ujao zitatimia
Yesu ni wa kwanza kufufuliwa kwenda mbinguni na kupewa uhai usioweza kufa, lakini si wa mwisho; wafuasi wake watiwa-mafuta 144,000 watapata ufufuo kama wake