Ibada
Tunapaswa kuelekeza ibada yetu kwa nani peke yake?
Kut 34:14; Kum 5:8-10; Isa 42:8
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 4:8-10—Shetani anasema kwamba atampa Yesu falme zote za dunia ikiwa atamfanyia tendo la ibada; Yesu anakataa, na kuazimia kumwabudu Yehova peke yake
Ufu 19:9, 10—Malaika mwenye nguvu anakataa kuabudiwa na mtume Yohana
Yehova anataka tumwabudu jinsi gani?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Isa 1:10-17—Yehova anakataa na kuchukia matendo ya ibada ya kinafiki ya watu ambao wanakataa kuishi kulingana na viwango vyake
Mt 15:1-11—Yesu anaonyesha kwamba Yehova hakubali ibada ya kidesturi ambayo inakazia kufuata maagizo ya wanadamu badala ya sheria za Mungu
Inapowezekana, kwa nini tunapaswa kumwabudu Yehova pamoja na waabudu wenzetu?
Tazama pia Zb 133:1-3
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 2:40-42—Katika karne ya kwanza, Wakristo walikusanyika pamoja kwa ajili ya kusali, kutumia muda pamoja, na kujifunza mafundisho yaliyoongozwa na roho takatifu
1Ko 14:26-40—Mtume Paulo anatoa mwongozo kwamba mikutano ya kutaniko inapaswa kuwa na utaratibu mzuri na iwe yenye kutia moyo, ili wote waweze kujifunza na kuelewa mambo wanayofundishwa
Tunapaswa kufanya nini ili kuhakikisha kwamba ibada yetu inakubaliwa na Yehova?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ebr 11:6—Mtume Paulo anaeleza kwamba imani ni muhimu ikiwa tunataka kumwabudu Yehova kwa njia anayoikubali
Yak 2:14-17, 24-26—Yakobo, ndugu nusu ya Yesu, anafafanua kwamba imani yetu ni lazima ionyeshwe kwa matendo; imani yetu inatuchochea kutenda