Rehema
Kuonyesha rehema kunatia ndani nini?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Zb 51:1, 2—Mfalme Daudi anapomwomba Yehova rehema, anaomba dhambi zake zisamehewe na kusafishwa
Lu 10:29-37—Yesu anafundisha somo kuhusu rehema kwa kutumia mfano wa Msamaria aliyemwonyesha fadhili na ufikirio Myahudi
Kwa nini wanadamu wote wanahitaji kuonyeshwa rehema?
Tazama pia 1Fa 8:46-50
Yehova ametuwekea mfano gani inapohusu kuonyesha rehema?
Kut 34:6; Ne 9:17; Zb 103:8; 2Ko 1:3
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ayu 42:1, 2, 6-10; Yak 5:11—Yehova anamwonyesha rehema Ayubu na anamfundisha kuonyesha rehema pia
Lu 15:11-32—Yesu anafundisha kuhusu rehema ya Yehova kwa kutumia mfano wa jinsi baba anavyomtendea mwana wake mwasi anayetubu
Kwa nini Yehova anatuonyesha rehema?
Tazama pia Tit 3:4, 5
Dhabihu ya Kristo inatusaidiaje kupata msamaha wa dhambi?
Kwa nini tunapaswa kuomba tuonyeshwe rehema na kwa nini sikuzote tunapaswa kushukuru kwa zawadi hiyo?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Zb 51:1-4—Mfalme Daudi analemewa na hisia za hatia kwa sababu ya dhambi zake, kwa unyenyekevu anamwomba Yehova amwonyeshe rehema
Lu 18:9-14—Yesu anatumia mfano kukazia kwamba Yehova anawaonyesha rehema wale ambao kwa unyenyekevu wanakubali makosa yao
Kwa nini hata wale waliofanya dhambi nzito wanaweza kutumaini kuonyeshwa rehema?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
2Nya 33:9-13, 15—Ingawa Manase, ni mfalme mwovu sana, anatubu na kuomba kuonyeshwa rehema; anarudishiwa ufalme wake, na anaendelea kuonyesha kwa matendo yake kwamba kwa kweli amebadilika
Yon 3:4-10—Ingawa Waninawi ni wakatili sana na wauaji, wanatubu dhambi zao na kuonyeshwa rehema na Mungu
Kwa nini ni muhimu kuungama dhambi zetu kwa Yehova na kubadili njia zetu ili tupate rehema yake?
Rehema ya Yehova haimaanishi kwamba tutaepuka nidhamu au matokeo mabaya ya dhambi zetu
Kwa nini tunapaswa kuwa wenye rehema?
Huenda uhusiano wetu na Yehova utakuwaje ikiwa tutashindwa kuonyesha rehema?
Tazama pia Met 21:13
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 18:23-35—Yesu anatumia mfano kuonyesha kwamba mtu asiyeonyesha rehema, hataonyeshwa rehema na Yehova
Lu 10:29-37—Mfano unaojulikana sana unaonyesha kwamba Yehova na Yesu hawapendezwi na mtu asiyeonyesha rehema, bali wanafurahishwa na mtu anayeonyesha rehema kama vile yule Msamaria