Waangalizi
Waangalizi Wakristo wanapaswa kufikia sifa zipi kwa kiwango kinachofaa ili wastahili kutumikia?
Waangalizi kutanikoni wanahitaji kuwa mfano mzuri katika kutimiza matakwa gani mengine ya Kikristo?
Mt 28:19, 20; Gal 5:22, 23; 6:1; Efe 5:28; 6:4; 1Ti 4:15; 2Ti 1:14; Tit 2:12, 14; Ebr 10:24, 25; 1Pe 3:13
Watumishi wa huduma wanapaswa kufikia sifa zipi kwa kiwango kinachofaa ili wastahili kutumikia?
Roho ya Mungu inahusikaje akina ndugu wanapowekwa rasmi kuwa waangalizi?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 13:2-5; 14:23—Waangalizi wanaosafiri, Paulo na Barnaba, wanawaweka rasmi wanaume wanaotegemeka kuwa wazee katika makutaniko mbalimbali; leo, waangalizi wa mzunguko wanafanya vivyo hivyo, wanamwomba Yehova roho takatifu na kufuata kwa makini Maandiko yaliyoongozwa na roho, ambayo yanataja sifa za kustahili
Tit 1:1, 5—Tito anakabidhiwa kazi ya kutembelea makutaniko mbalimbali, na kuwaweka rasmi wazee
Kutaniko ni mali ya nani, na lilinunuliwa kwa gharama gani?
Kwa nini waangalizi wanafafanuliwa kuwa wale wanaohudumu, au wanaowatumikia wengine?
Kwa nini ni lazima waangalizi waendelee kuwa wanyenyekevu?
Flp 1:1; 2:5-8; 1Th 2:6-8; 1Pe 5:1-3, 5, 6
Simulizi la Biblia linalohusika:
Mdo 20:17, 31-38—Mtume Paulo anawakumbusha wazee kutoka Efeso kuhusu kazi aliyofanya kwa miaka mingi kwa ajili yao, nao wanaonyesha uthamini kwa ajili ya upendo aliowaonyesha
Mwangalizi Mkristo anaonaje mwongozo unaotoka kwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”?
Ni njia gani bora ambayo wazee wanaweza kutumia kuwafundisha wengine?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ne 5:14-16—Kwa sababu anamheshimu sana Yehova, Gavana Nehemia anakataa kutumia vibaya mamlaka aliyo nayo juu ya watu wa Mungu, hata anakataa mambo anayostahili kupata
Yoh 13:12-15—Yesu anawafundisha wafuasi wake kwa kuwawekea kielelezo cha kuwa wanyenyekevu
Mchungaji Mkristo anawezaje kuonyesha upendo kwa kila mtu kutanikoni?
Wazee wanawasaidiaje wale walio wagonjwa kiroho?
Wazee wana jukumu gani wanapofundisha?
1Ti 1:3-7; 2Ti 2:16-18; Tit 1:9
Tazama pia 2Ko 11:2-4
Kwa nini ni lazima wazee wajitahidi sana kuhakikisha kwamba kutaniko ni safi kiadili?
1Ko 5:1-5, 12, 13; Yak 3:17; Yud 3, 4; Ufu 2:18, 20
Tazama pia 1Ti 5:1, 2, 22
Wazee wanajitahidi kuwazoeza akina nani?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mt 10:5-20—Yesu anawazoeza mitume wake 12 kabla ya kuwatuma katika kazi ya kuhubiri
Lu 10:1-11—Yesu anawapatia wanafunzi wake 70 maagizo muhimu kabla ya kuwatuma katika kazi ya kuhubiri
Ni nini kitakachowasaidia wazee kushughulikia majukumu yao mengi?
Tazama pia Met 3:5, 6
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Fa 3:9-12—Mfalme Sulemani anasali kwa Yehova apate utambuzi na uelewaji anaohitaji ili kuwahukumu watu wa Yehova
2Nya 19:4-7—Mfalme Yehoshafati anawaweka rasmi waamuzi katika majiji ya Yuda, na kuwakumbusha kwamba Yehova atakuwa pamoja nao wanapotimiza mgawo huo muhimu
Kutaniko linapaswa kuwaonaje waangalizi waaminifu?
1Th 5:12, 13; 1Ti 5:17; Ebr 13:7, 17
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Mdo 20:37—Wazee wa Efeso hawasiti kuonyesha jinsi wanavyompenda mtume Paulo
Mdo 28:14-16—Mtume Paulo anaposafiri kwenda Roma, akina ndugu kutoka katika jiji hilo wanasafiri kilomita 65 hivi ili kukutana naye katika Soko la Apio, na kumtia moyo sana