Useja
Kwa nini ni sahihi kusema kwamba useja ni zawadi?
Kwa nini si sawa kumshinikiza Mkristo mseja kuoa au kuolewa?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Ro 14:10-12—Mtume Paulo anaeleza kwa nini ni kosa kumhukumu Mkristo mwenzetu
1Ko 9:3-5—Mtume Paulo ana haki ya kuoa; hata hivyo, kuwa mseja kunamruhusu akazie fikira huduma yake
Je, waseja wanapaswa kuhisi kwamba ni lazima wafunge ndoa ili wawe na maisha yenye furaha?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Amu 11:30-40—Binti ya Yeftha anabaki akiwa mseja na anakuwa na maisha yenye kuridhisha
Mdo 20:35—Maneno ya Kristo yanadokeza kwamba ingawa hakufunga ndoa alikuwa na furaha kwa sababu ya kutoa
1Th 1:2-9; 2:12—Mtume Paulo, mwanamume mseja, anaeleza kuhusu shangwe na matokeo yenye kuridhisha ambayo anapata katika huduma yake
Kwa nini ni lazima waseja, kama tu watumishi wote wa Mungu, wadumishe mwenendo ulio safi kiadili?
1Ko 6:18; Gal 5:19-21; Efe 5:3, 4
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Met 7:7-23—Mfalme Sulemani anafafanua matokeo mabaya anayopata mwanamume kijana ambaye anaruhusu ashawishiwe na mwanamke mwenye maadili mapotovu
Wim 4:12; 8:8-10—Msichana Mshulami anasifiwa kwa mwenendo wake safi
Ni chini ya hali gani lingekuwa jambo la hekima kwa mseja kufikiria kufunga ndoa?
Tazama pia 1Th 4:4, 5