YEHOVA-NISI
(Yehova-nisi).
Jina la madhabahu ya ukumbusho iliyojengwa na Musa baada ya Waisraeli kuwashinda Waamaleki vitani huko Refidimu.—Kut 17:8, 13-16.
Jina hilo linamaanisha “Yehova Ni Nguzo Yangu ya Ishara,” kwa kuwa neno nis·siʼ linatokana na neno nes (linalomaanisha nguzo ya ishara). Watafsiri wa Septuajinti ya Kigiriki waliamini kwamba neno nis·siʼ linatokana na neno nus (linalomaanisha kukimbia ili kupata kimbilio), kwa hiyo ilisemekana maana ya Yehova-nisi ni “Yehova Ni Kimbilio Langu,” hata hivyo katika Vulgate ya Kilatini iliaminika kwamba neno hilo linatokana na neno na·sasʼ (linalomaanisha kuinua; kupandisha), kwa hiyo ilisemekana maana ya jina hilo ni “Yehova Hunikweza.”—Kut 17:15, maelezo ya chini.