Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • dx96-12 kur. 3-4
  • Jinsi ya Kutumia Fahirisi Hii

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutumia Fahirisi Hii
  • Fahirisi ya Machapisho ya Watch Tower 1996-2012
Fahirisi ya Machapisho ya Watch Tower 1996-2012
dx96-12 kur. 3-4

JINSI YA KUTUMIA FAHIRISI HII

MAMBO YALIYOMO NA MANUFAA YA KUITUMIA

Mashahidi wa Yehova wanafurahi kuandaa Fahirisi hii yenye marejeo ya vitabu vilivyochapishwa au kusahihishwa katika miaka inayoonyeshwa.

Makala zinazochapishwa kwa ukawaida katika Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, na Huduma Yetu ya Ufalme zimeorodheshwa chini ya vichwa vikuu vinavyolingana na kichwa cha makala, kama vile MASWALI KUTOKA KWA WASOMAJI.

Habari zaidi kuhusu jinsi ya kutumia Fahirisi zinapatikana chini ya kichwa kikuu, FAHIRISI.

Fahirisi hii itakuwa yenye manufaa sana kwako kuhusiana na huduma yako ya shambani, utendaji wako kutanikoni, na funzo lako la kibinafsi. Pia, itakuandalia mwongozo unaofaa katika familia na katika shughuli zako za kila siku.

FAHIRISI YA HABARI

Jinsi Vichwa Vikuu Vilivyoorodheshwa. Vichwa vikuu vimeorodheshwa kialfabeti. Ikiwa unatafuta idadi au hesabu fulani, tafuta kulingana na vile idadi au hesabu hiyo inavyotamkwa (k.m., 144,000 inapatikana chini ya “M,” kulingana na jinsi idadi hiyo inavyotamkwa, yaani, “mia moja”). Vichwa vinavyohusisha miaka vimeorodheshwa kwa kutumia maneno “mwaka wa,” kwa hiyo, ili kupata 1914, angalia MWAKA WA 1914. Majina ya maeneo yanayoanza na herufi “St.” yameorodheshwa kana kwamba herufi “St.” ni neno la Kiingereza “Saint.” Kwa hiyo, majina hayo utayapata chini ya herufi “S.” Alama za mabano na vituo vinatangulia nambari na herufi (k.m. KONGO [Kinshasa]; KONGO, JAMHURI YA; KONGO YA UBELGIJI).

Habari chini ya vichwa vikuu au vichwa vidogo zimepangwa kialfabeti, hata hivyo, nyingine zimeorodheshwa kulingana na utaratibu wa nambari (k.m., ona kichwa kidogo “Baadhi ya Zile Amri Kumi,” chini ya kichwa kikuu AMRI KUMI). Orodha za miaka, kama ile iliyo chini ya kichwa TAREHE, zimepangwa kulingana na wakati wa matukio. Orodha za maandiko, kama ile iliyo chini ya kichwa BIBLIA, USAHIHI WA, zimepangwa kulingana na utaratibu wa vitabu vya Biblia.

Jinsi ya Kupata Habari. Habari zimepangwa kupatana na jambo linalozungumziwa, bali si kupatana na kichwa cha sura au makala. Hata hivyo, nyakati nyingine maneno makuu katika kichwa cha makala yametumiwa kama kichwa kikuu.

Fahirisi hii imeorodhesha maneno kwa kutumia vitenzi, vifungu vya maneno, na nomino (katika hali ya umoja au ya wingi). Vifungu fulani vya maneno vimeorodheshwa kama vinavyotumika (k.m., KUTIA MAFUTA). Lakini vifungu vingine vimeorodheshwa kulingana na neno muhimu katika kifungu (k.m., hakuna kichwa kikuu “UKOSEFU WA MAADILI,” bali MAADILI, UKOSEFU WA). Usipopata neno unalotafuta katika hali ya umoja, angalia hali ya wingi (k.m., neno “MCHEZO” halipatikani katika Fahirisi hii, bali neno MICHEZO, lililo katika hali ya wingi). Kitenzi chenye kiambishi-awali “ku-” kimetumiwa badala ya shina la neno (k.m., hutapata neno “CHEZA” bali kitenzi KUCHEZA). Usipopata kitenzi unachotafuta, angalia nomino (k.m., nomino UFUMAJI imetumiwa bali si kitenzi “KUFUMA”). Hata hivyo, maneno fulani yameorodheshwa kama nomino na vilevile kama kitenzi (k.m., kuna kichwa kikuu KUZOEZA/KUZOEZWA, na pia MAZOEZI).

Ili kupata habari fulani, itafute chini ya neno au kifungu cha maneno kinachofafanua habari hiyo vizuri. Ukitafuta neno au kifungu cha maneno kinachofafanua waziwazi habari unayotaka, utapata habari hususa. Kwa mfano, iwapo unataka habari kuhusu kutiwa damu mishipani, angalia kichwa KUTIA DAMU MISHIPANI badala ya kichwa DAMU.

Mambo yaliyoonwa katika utumishi yanapatikana chini ya kichwa MAMBO YALIYOONWA KATIKA HUDUMA YA SHAMBANI. Yanapatikana pia chini ya vichwa vingine vikuu vinavyohusu huduma ya shambani, na vilevile vitabu mbalimbali vilivyoorodheshwa katika Fahirisi hii kama vichwa vikuu. Mambo yaliyoonwa yanapatikana pia chini ya jina la nchi ambako jambo fulani lililoonwa lilitukia.

Majina ya watu binafsi yameorodheshwa kama vichwa vikuu mara chache tu. Mengine yanapatikana chini ya kichwa MASIMULIZI YA MAISHA YA MASHAHIDI WA YEHOVA. Majina ya Mashahidi wote wanaotajwa katika Fahirisi hii yameorodheshwa chini ya nchi walikotumika.

Chini ya vichwa fulani vidogo kuna orodha za miaka au majina ambayo yanaweza kutumiwa kutafuta vichwa vingine vikuu. Kwa mfano, chini ya kichwa kikuu MAKUSANYIKO YA WILAYA NA YA KIMATAIFA, utapata kichwa kidogo “Orodha Kulingana na Mwaka.” Chini ya kichwa hicho kidogo utapata “2005, ‘Utii wa Kimungu,’ Makusanyiko ya Wilaya.” Tafuta kichwa kikuu “UTII WA KIMUNGU,” MAKUSANYIKO YA WILAYA (2005), na utapata marejeo yote yanayohusu kusanyiko hili katika vitabu mbalimbali vinavyorejelewa katika Fahirisi hii. Makusanyiko yasiyo na kichwa hususa, yanapatikana chini ya jina la jiji ambapo kusanyiko lilifanyiwa, kwa mfano, COLUMBUS, OHIO, MAKUSANYIKO.

Baada ya kupata kichwa kikuu, soma kwanza vichwa vya marejeo vilivyo chini ya kichwa hicho. Vichwa vya marejeo vinaweza kukusaidia kupata kichwa kinachozungumzia kihususa zaidi habari unayotafuta (k.m., chini tu ya kichwa kikuu NAFSI kuna kichwa cha marejeo “ONA PIA KUTOKUFA KWA NAFSI”). Ikiwa hakuna vichwa vya marejeo vinavyofaa chini ya kichwa kikuu, chunguza habari zilizo chini ya kichwa hicho. Pia kuna vichwa vidogo, na baadhi ya vichwa hivyo vimeorodheshwa chini tu ya vichwa vya marejeo ili uweze kuvipata moja kwa moja (k.m., MASIMULIZI YA MAISHA YA MASHAHIDI WA YEHOVA; [ONA PIA MASIMULIZI YA WATU BINAFSI]; [Kuna vichwa vidogo: Majina ya Walioandika; Vichwa Mbalimbali]).

Ikiwa hupati habari unayotafuta chini ya neno au kifungu cha maneno ulichochagua, jaribu kutumia kisawe au neno lingine lenye maana pana zaidi.

Hata ukipata marejeo yanayofaa chini ya kichwa fulani, kumbuka kwamba huenda usipate marejeo yote kuhusu habari unayofanyia utafiti chini ya kichwa hicho. Kwa hiyo, ni vizuri kutafuta habari chini ya vichwa vingine pia, hasa kuhusu mambo muhimu.

Zingatia: Jina “Wanafunzi wa Biblia” (herufi za kwanza “W” na “B” zinapokuwa kubwa) linamaanisha Mashahidi wa Yehova kuanzia siku za C. T. Russell hadi mwaka wa 1931, wakati jina Mashahidi wa Yehova lilipoanza kutumiwa.

FAHIRISI YA MAANDIKO

Maandiko Katika Fahirisi Hii. Maandiko yaliyoorodheshwa katika Fahirisi ya Maandiko ni yale tu ambayo yamefafanuliwa kwa njia fulani. Yaani, maandiko ambayo maana au muktadha wake umefafanuliwa, sababu ya kuyaandika imeonyeshwa, au neno fulani la lugha ya awali limefafanuliwa.

Maandiko ambayo yametumiwa tu kuthibitisha habari fulani, hayajaorodheshwa, kwa vile hayajafafanuliwa. Kwa mfano, ikiwa andiko fulani kama vile Ezekieli 18:4 limetumiwa tu kuonyesha kwamba nafsi inaweza kufa, basi andiko hilo halijaorodheshwa, kwa kuwa halijafafanuliwa.

Jinsi ya Kupata Habari za Ufafanuzi. Marejeo yenye nambari za kurasa zinazofuatana (k.m., 23-25) yanaonyesha kurasa ambapo andiko limenukuliwa, kutajwa, na kufafanuliwa. Huenda andiko lisipatikane kwenye ukurasa wa kwanza ulioonyeshwa; lakini huenda ikawa ufafanuzi wa andiko hilo unaanza kwenye ukurasa huo. Katika visa fulani, ufafanuzi wa andiko unaanza, halafu habari nyingine zinatajwa, kisha ufafanuzi unaendelea. Kwa hiyo, hakikisha umesoma kurasa zote zilizoonyeshwa.

MAREJEO

Jinsi Yalivyopangwa. Marejeo yamepangwa kulingana na mwaka, na mwaka wa karibuni zaidi unatangulia. Marejeo ya kila mwaka yanafuatana hivi: Mnara wa Mlinzi, Biblia, vitabu, vijitabu na broshua, Amkeni!, na Huduma Yetu ya Ufalme. Marejeo ya Mnara wa Mlinzi, Amkeni!, na Huduma Yetu ya Ufalme yanaanza na toleo la kwanza la mwaka hadi toleo la mwisho. Marejeo ya Huduma Yetu ya Ufalme yanarejelea habari katika chapa ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo, kama habari zilizorejelewa hazipatikani katika toleo lilelile la chapa ya Congo-Kinshasa, huenda zikapatikana katika toleo la mwezi tofauti la chapa hiyo, au zisipatikane kabisa.

Tunatumaini kwamba Fahirisi hii itakusaidia ukiwa mwanafunzi mnyofu wa Biblia ‘kutembea kwa kumstahili Yehova kwa kusudi la kumpendeza yeye kikamili unapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema na kuongezeka katika ujuzi sahihi wa Mungu.’—Kol. 1:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki