Mahali pa Mataifa Yote
Kwamba katika ufalme wa Mungu na vile vile katika usimamizi wake na katikati ya raia zake watakuwamo watu wa mataifa yote, inaonyeshwa wazi sana katika Biblia. Ufunuo 5:9, 10 unasema kwamba kwa damu yake mwenyewe Kristo ‘alimnunulia Mungu watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,’ na, chini ya usimamizi wake, “watatawala kama wafalme.” Watatawala juu ya nani? Ufunuo 7:9 unajibu: “mkutano mkubwa sana . . . watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha,” wote ni waabudu wa Mungu wa kweli.