Sababu Gani Kukawia?
● Imesemekana kwamba kadiri ambavyo mtu ni mvivu, ndivyo asemavyo atafanya mambo “kesho.” Ikiwa jambo limepaswa kufanywa, sababu gani ukawie kulifanya? Huu ndio wakati wa kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Mungu. Juu ya mtu mvivu Biblia inasema hivi: “Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono upate usingizi! Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi.”—Mit. 6:10, 11.