Sababu Gani “Vilemba Vingi”?
● Ufunuo 19:12 wamsimulia Yesu Kristo, “MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA,” kama akiwa na “vilemba vingi” juu ya kichwa chake. Kwa sababu gani? Walipokuwa na mamlaka juu ya nchi zaidi ya moja, wafalme wa kale mara nyingi walivaa zaidi ya taji au kilemba, kimoja. Kwa mfano, uhakika wa kwamba Misri ya Juu na Misri ya Chini ilitawalwa na mtawala mmoja mkuu zaidi ungeweza kuonekana kutokana na vazi la kifalme kichwani—taji maradufu au ya mwungano. Kwa hiyo, vilemba vingi juu ya kichwa cha Bwana Yesu Kristo vingeonyesha kwamba ana utawala mkubwa, wa ulimwenguni pote akiwa “MFALME WA WAFALME.”