Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 4/15 kur. 191-192
  • Historia ya Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Historia ya Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • TAMASHA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKMA
  • MATUMAINI YA MAMBO BORA UJAPOKUWAPO ‘UTUMWA WA KIBABELI’
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 4/15 kur. 191-192

Historia ya Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa

BAADA ya mwanzoni mwa Oktoba 1914, wafuasi waliotiwa mafuta wa Kristo walitangaza kwamba Majira ya Mataifa yalikuwa yamekoma na kwamba mataifa yalikuwa yanakaribia kuharibiwa katika Har–​Magedoni. (Luka 21:24; Ufu. 16:14-16) ‘Mashahidi wawili’ hao wa mfano waliutangaza ujumbe huo wa maombolezo kwa mataifa kwa siku 1,260, au miaka mitatu u nusu (Oktoba 4/5, 1914, mpaka Machi 26/27, 1918). Ndipo taratibu ya kinyama ya kisiasa ya Ibilisi ilipofanya vita juu ya ‘mashahidi wawili’ wa Mungu, mwishowe ‘ikawaua’ kwa habari ya kazi yao ya kutesa ya kutoa unabii wakiwa “wamevikwa magunia,” nao adui zao wa kidini, wa kisiasa, wa kijeshi na wa mahakma wakapata faraja kuu kwa sababu hiyo. (Ufu. 11:3-7; 13:1) Huo ulikuwa ndio unabii, nao ulitimizwa. Lakini kwa njia gani?

Mei 7, 1918, mahakma iitwayo United States District Court ya Wilaya ya Mashariki ya New York ilitoa amri ili watumishi wakuu wa Watch Tower Society wakamatwe. Waliokamatwa walikuwa Msimamizi J. F. Rutherford, Katibu-Mweka-Hazina W. E. Van Amburgh, Clayton J. Woodwoth na George H. Fisher (watungaji wawili wa The Finished, Mystery), F. H. Robinson (mshiriki wa halmashauri ya uandikaji ya Watch Tower), A. H. Macmillan, R. J. Martin na Giovanni DeCecca.

TAMASHA KATIKA CHUMBA CHA MAHAKMA

United States ilikuwa vitani. Hivyo kesi ya Wanafunzi wa Biblia juu ya shtaka la kuwa waasi-serikali ilivuta sana fikira za watu. Nia ya watu hadharani ilikuwa nini? Walipendelea kitu cho chote chenye kuendeleza jitihada ya vita. Jamii za wanamuziki zilipiga muziki nao askari wakatembea kijeshi wakizunguka-zunguka karibu na Brooklyn Borough Hall. Katika chumba cha mahakma kesi ile ya siku kumi na tano iliendelea, ushuhuda chungu nzima ukatolewa. Acheni tuingie ndani tuone yaliyoendelea.

A. H. Macmillan, mmojawapo wa washtakiwa, anatusaidia kuona hali ilivyokuwa, kwa maana baadaye aliandika hivi: “Wakati wa kesi serikali ilisema kwamba mtu akisimama katika pembe ya barabara na kusema sala ya Bwana kwa kusudi la kuvunja watu moyo wasijiunge na jeshi, angeweza kupelekwa gerezani. Kwa hiyo unaweza kuona ilivyokuwa vyepesi kwao kujua kusudi la mtu. Walidhani wangeweza kujua aliyokuwa akiwaza mtu mwingine, na kwa hiyo walituchukulia hatua kwa msingi huo hata ingawa tulithibitisha kwamba wakati wo wote hatukufanya shauri la kufanya lo lote kuzuia watu wasiingie jeshini wala hatukuvunja mtu moyo asifanye hivyo. Ilikuwa kazi bure kueleza hayo yote. Viongozi fulani wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo na marafiki zao wa kisiasa walikuwa wamekata shauri kutupata. Kwa ruhusa ya Hakimu Howe, tulishtakiwa kwamba kusudi letu lilipaswa kufahamiwa kutokana na matendo yetu. Mimi nilionekana kuwa mwenye hatia kwa sababu tu nilithibitisha cheki iliyotiwa sahihi kwa kuongeza sahihi yangu kwa kusudi ambalo halikuweza kujulikana, na kwamba nilitia sahihi hati fulani iliyosomwa na Ndugu Rutherford katika mkutano wa baraza. Hata hivyo hawakuweza kuhakikisha ilikuwa sahihi yangu. Udhalimu uliofanywa juu ya jambo hilo baadaye ulitusaidia katika rufani yetu.”

Mwishowe, baada ya kesi hiyo ndefu, siku iliyokuwa ikingojewa ya kutolewa kwa uamuzi ikafika. Juni 20, 1918, karibu saa 11 jioni, kesi ilipelekwa kwa baraza ya mahakimu. Baadaye J. F. Rutherford alisema hivi: “Baraza ya mahakimu ilisita-sita kidogo kabla haijatoa hukumu. Mwishowe Hakimu Howe akawapelekea agizo kwamba lazima walete hukumu yenye kusema tu ‘Wenye Hatia,’ kama alivyotuambia mmoja wa washiriki wa baraza ya mahakimu baadaye.” Baada ya karibu saa nne na nusu za kufikiri, baraza ya mahakimu ilirudi saa 3:40 usiku wakiwa na hukumu yao kuonyesha tu ‘Wenye Hatia.’

Saba kati ya washtakiwa walihukumiwa miaka minane gerezani (miaka ishirini kila mmoja kwa mashtaka manne, yenye kuhesabiwa wakati ule ule mmoja yote pamoja). Hukumu ya Giovanni DeCecca ilikawizwa, lakini mwishowe akahukumiwa miaka 40, au miaka kumi kwa kila moja la mashtaka yale manne. Washtakiwa walipaswa kutumikia vifungo vyao katika gereza kuu la United States katika Atlanta, Georgia.

Katika kitabu chake Preachers Present Arms, Ray H. Abrams alifikiria kesi ya J. F. Rutherford na washirika wake akasema hivi:

“Uchunguzi wa kesi yote unaonyesha kwamba makanisa na viongozi wa kidini ndio waliokuwa chanzo cha majaribio ya kufutilia mbali Warusselli. . . .

“Wakati habari za hukumu za miaka 20 zilipofikia waandikaji wa magazeti ya kidini, karibu kila gazeti, kubwa na dogo, lilichapwa habari za kufurahia tukio hilo. Mimi mimeshindwa kuona maneno yo yote ya kuonyesha huruma katika magazeti yo yote ya dini ya orthodoksi. ‘Hakuwezi kuwa na shaka,’ kamalizia Upton Sinclair, kwamba ‘mateso . . . kidogo yalisababishwa na uhakika wa kwamba wao walikuwa wameamsha chuki ya baraza za dini za “orthodoksi.”’ Sasa ilielekea serikali ilifaulu kuwatimizia makanisa jambo ambalo makanisa yalikuwa yamejitahidi pamoja kulifanya yakashindwa​—kuponda-ponda hawa ‘manabii wa Baali’ watoweke milele.”

MATUMAINI YA MAMBO BORA UJAPOKUWAPO ‘UTUMWA WA KIBABELI’

Tangu mwaka wa 607 mpaka 537 K.W.K. Wayahudi walihuzunika wakiwa watumwa katika Babeli ya kale. Kwa kulingana na hilo, waabudu wa Yehova walio wakf waliotiwa mafuta kwa roho takatifu yake waliingizwa katika utumwa wa Kibabeli na kuhamishwa katika kipindi cha Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ya 1914-1918. Hasa uzito wa hali yao ya utumwa ulionwa wakati ndugu wanane wale waaminifu wa makao makuu ya Sosaiti walipofungwa katika gereza kuu katika Atlanta, Georgia.

Lakini wakati huo wote wenye magumu, hata toleo moja la The Watch Tower halikukosa kuchapwa.

—Kutoka 1975 Yearbook of Jehovah’s Witnesses.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki