“UZAO” WA KIDUNIA WA NYOKA
(Funzo la Kitabu hs 3:19-42)
1. Kwa sababu gani Wakristo wanatiwa moyo wasiwe kama Kaini, mwana wa kwanza wa wanadamu wote?
“UZAO” uliokuwa fumbo wa “mwanamke” wa Mungu haukuwa mwana wa kwanza wa Hawa, aliyemwita Kaini. Kuwa kwa Ka-ini mwana wa kwanza kati ya wanadamu wote hakukumpa haki ya kutumikia kama “uzao” huo ulioahidiwa. Tena, kisigino cha Kaini hakikutiwa jeraha na Nyoka Mkuu, Ibilisi. Kaini alijeruhi mtu kichwani, Habili, ndugu yake mcha Mungu, kwa kumwua labda kwa kumponda kichwani. Mahali pa kubarikiwa na Mungu na kupokea roho takatifu Yake, Kaini akawa wa pili katika Biblia kuitwa ‘mlaaniwa,’ maana Nyoka wa mfano au Ibilisi ndiye aliyekuwa wa kwanza. (Mwa. 3:14; 4:11) Kwa njia hiyo Kaini alijifanya sehemu ya “uzao” wa kidunia wa Nyoka Mkuu, Ibilisi, ambaye alimwiga kwa kusema uongo na kuua mwanadamu. Hakumpenda ndugu yake, aliyeweza kumwona, wala Mungu, ambaye hakuweza kumwona. Wa-fuasi wa Kristo wanatiwa moyo wawe tofauti na Kaini, katika maneno yanayofauta:
“Tupendane sisi kwa sisi? si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu mafendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.” (I Yohana 3:11, 12) “OIe wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini.”—Yuda 11.
2, 3. Kaini alimwiga Ibilisi kwa kutenda dhambi ya namna gani, na ni kwa sababu ya jambo gani lililoonekana wazi Kaini aliweza kufanya hivyo?
2 Kaini alimwiga Ibilisi, baba yake wa kiroho, “yule mwovu,” katika kutenda dhambi juu ya roho takatifu ya Mungu. Hiyo haimaanishi kwamba Kaini, mwana wa kwanza wa Adarnu na Hawa, alikuwa na roho takatifu wakati mmoja. Wazazi wake wa kidunia walikuwa wamepoteza roho takatifu kwa sababu ya kuvunja amri ya Mungu kwa makusudi. Lakini Kaini aliona utendaji wa roho takatifu. Wakati gani na jinsi gani?
3 Huo ulikuwa wakati Kaini alipomtolea Mungu toleo la ukulima wake, na hali ndugu yake mdogo Habili akimtolea Mungu dhabihu ya wanyama aliochinja wa kundi lake la kondoo. Je! matoleo yote mawili ya ndugu hao yalikubaliwa na Mungu? Mwanzo 4:4-7 hutuambia hivi: ”[Yehova] akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. [Yehova] akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.”
4. Kaini aliona roho takatifu ikijionyeshaje?
4 Bila shaka, Mungu hakuwatokea Kaini na Habili wakati huo. Hatuambiwi jinsi alivyomkubali Habili na dhabihu yake. Lakini bila shaka kulikuwa na ushuhuda wenye kuonekana. Ulikuwa utendaji wa roho takatifu ya Mungu. Kaini aliuona, bila kuambiwa na Mungu. Kwa hiyo akawaka kwa hasira kuu nao uso wake uka’kunjamana. Hakutenda kwa unyenyekevu wala hakutubu alipoona roho takatifu ikitenda kazi na kutoka kwa Mungu aliyekuwa akimtolea toleo lisilokubaliwa.
5. Dhambi ya Kaini juu ya roho takatifu ilikuwa ya namna gani, na kwa sababu gani?
5 Ni wazi kwamba Kaini hakuwa akifenda haki. Sauti ya Mungu iliyotoka kafika makao yasiyoonekana ilimweleza hivyo. Kaini alikataa kunyenyekea kwa sababu alikuwa na kiburi mno, akakosa kutubu na kugeuka afanye mema, ingawa dhambi ilikuwa ikimwotea kama ikiwa katika mlango wa nyumba yake na kutamani awe mateka wake. Yeye hakutaka kuishinda, bila kujali roho takatifu ya Mungu ilivyomwonyesha. Kwa sababu hakutaka kutia furaha usoni pake, alifanya hila juu ya yeye aliyekubaliwa na Mungu akamwua. Hivyo alitenda dhambi juu ya roho takatifu.
6. Twaweza kusema nini juu ya kama yule ambaye sasa akawa Ibilisi alikuwa na roho takatifu akaona ikitenda kazi?
6 Mungu alichukizwa akamlaani Kaini, Lakini Nyoka Mkuu, Ibilisi, alip’endezwa kwa maana sasa aliona mwana wake wa kidunia aliyetenda sawasawa na baba yake wa kiroho. Ibilisi mwenyewe alikuwa ametenda dhambi juu ya roho takatifu. Yule ambaye sasa akawa Ibilisi alikuwa ameona utendaji wa roho takatifu katika makao ya mbinguni na wakati wa kuumbwa kwa dunia na kwa mwanadamu mkamilifu juu yake, licha ya kumwona Mungu mwenyewe. (Ayubu 38:7) Wakati alipokuwa hajishawishi mwenyewe, alikuwa na kadiri fulani ya roho ya Baba yake wa mbinguni. Alijua mambo aliyokuwa amewezeshwa kufanya na roho takatifu hiyo. Aiiona pia “roho ya fadhili zisizostahilika” ambayo Mungu alionyesha Adamu na Hawa kwa kuwawezesha wafurahie uzima mkamilifu wa kibinadamu katika paradiso ya kidunia. Hata hivyo ‘mwana huyo wa Mungu’ wa mbinguni alifanya nini?—Ebr. 10:29, NW.
7. ‘Mwana huyo wa Mungu’ aliendeleaje katika hatua yenye dhambi juu ya roho takatifu na hivyo alijifanya mwenyewe kuwa nini?
7 Alieleza habari mbaya juu ya “roho ya fadhili zisizostahilika” kwa kumwambia Hawa kwamba roho hiyo iliongozwa na choyo kwa upande wa Mungu. Vilevile, kwamba katazo ambalo Mungu aliweka juu ya kula mti wa ujuzi wa mema na mabaya liliongozwa na hofu ya Mungu kwamba viumbe vyake wa kibinadamu huenda wakapata uwezo wa kujifanyia maamuzi bila kumtegemea, maamuzi ya yaliyo haki na mabaya, yaliyo mema na mabaya. Kwa hiyo, wakati ‘mwana wa Mungu’ wa kiroho alipopotoa mambo ya haki kwa makusudi akamdanganya Hawa atende dhambi, alitenda dhambi juu ya roho takatifu, dhambi asiyoweza kusamehewa mtu. Alijiacha ashawishwe na taraja la kichoyo la kupata enzi kuu juu ya dunia na wakaaji wake wa kibinadamu kisha akachukua hatua anyakue enzi kuu hiyo. Alipofanya hivyo alipoteza roho takatifu ya Mungu. Matunda ya roho ya Mungu yalinyauka katika maisha yake. Alijifanya Ibilisi, mwenye kustahili uharibifu tu.—Ebr. 12:29; 6:7, 8.
8. Ibilisi akawaje “mkuu wa pepo,” na kwa sababu gani wale wanaozoea uchawi hwatakuwa katika ufalme wa Mungu?
8 Mtenda dhambi huyo wa kwanza juu ya roho takatifu alijifanya shetani. “Wana wa Mungu” wa kimalaika waliojiunga naye baa-daye kumwasi Mungu wakawa mashetani kama Ibilisi. Mashetani hao wakawa “uzao” wa Nyoka Mkuu, na hivyo Ibilisi akawa ndiye “mkuu wa pepo,” ambaye akaitwa Beelzebuli. (Mt. 12:24-27) Hao ndio waendelezaji wa ushetani, kwa kusudi la kuondoa wafu wasimwabudu Mungu mmoja aliye hai na wa kweli, Yehova. Wamepangwa katika jamii ya “pepo wachafu.” (Mt.‘ 10:1, 8; 12:43-45) Kuzoea uchawi kwa maongozi ya mashetani hao kwaweza kutokeza uchafu wa kiroho tu kwa mzoeaji na kumfanya mchafu machoni pa Mungu. Mazoea ya uchawi ni mojawapo ya kazi za mwili wenye dhambi nayo yafazuia mfu asishiriki katika ufalme wa Mungu na baraka zake. Roho wachafu hao wanapinga roho takatifu ya Mungu, naye akataza mtu asihusiane hata kidogo na roho wachafu.—Kum. 18:9-14; Gal. 5:19, 20; Ufu. 9:20, 21; 21:8.
NI “ROHO” YA NAMNA GANI?
9. Kwa sababu gani yatupasa sasa tuweze kujua namna ya roho inayoendesha taratibu ya zamani iliyopo?
9 Ni jambo la maana zaidi sana tujue mambo yaliyotangulia. Kwa kuyajua tunaweza kufahamu sababu ya wanadamu kuwa katika hali ya sasa. Tumo katika karne ya 20, karne iliyokuwa na mwanzo mzuri sana kulingana na maoni ya kibinadamu. Kulingana na hesabu ya wakati ya Maandiko Matakatifu, tumefika karibu miaka elfu sita tangu ‘mwana wa Mungu’ mwenye kujitafutia yake mwenyewe alipoasi enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova na kuwaongoza Adamu na Hawa katika uasi wa namna iyo hiyo juu ya Mungu. Baada ya wanadamu hao wawili waasi kuondolewa katika paradiso ya Edeni, taratibu mpya ya kibinadamu ilianza duniani, iliyo tofauti na iliyokuwa imekusudiwa na Muumba wao kwa Dunia yetu. Kwa hiyo kufika hapo yatupasa tuweze kujua ni roho ya namna gani inayoendesha taratibu ya zamani iliyopo.
10. Tunapotaja roho inayopndesha taratibu ya zamani, twamaanisha nini kwa kutumia neno “roho”?
10 Tunaposema “roho” twamaanisha nguvu ya utendaji isiyoonekana, nguvu yenye kuhuisha, yenye kufia uhai, yenye kutia nguvu na kuongoza jamii ya kibinadamu kwa ujumla. Inaongoza mwendo wao wa maisha. Inawaongoza wote upande fulani. Hivyo wafu kwa ujumla wanaelekea upande mmoja bila kujua sana. Wanafanya mambo kama kwamba waii-zaliwa wakajua kuyafanya papo hapo, wakiongozwa na maono fulani ya ndani wafuate mwendo wa kawaida na kielelezo fulani cha maisha. Huenda kukawa na tofauti ndogo ndogo ikitegemea tofauti za nyutu za wafu, lakini jamii ya kibinadamu kwa ujumla ina maisha na malengo yale yale chini ya taratibu ya mambo iliyopo.
11, 12. (a) Ni nani mtawala asiyeonekana wa taratibu hii ya zamani, na je! amekuwa peke yake katika utawala huo? (b) Matokeo ya utawala huo usioonekana yamekuwa ya namna gani?
11 Roho hiyo inayoendesha taratibu ya zamani ya mambo iliyopo leo imeharibiwa sana na watu wasioonekana wenye nguvu zipitazo za wanadamu wanaotawala taratibu hii ya mambo na kusimamia. Hakuwezi kuwa na shaka juu ya yeye anayetawala taratibu yote. Huko nyuma katika mileani (miaka elfu) ya tano ya kuwako kwa taratibu ya zamani, Yesu Kristo alimtangaza Shetani Ibilisi kuwa “mkuu wa ulimwengu huu,” ambaye hakuwa na urafiki naye. Usiku wa mwisho wa kuishi kwake duniani akiwa mwanadamu, Yesu Kristo aliwaa-mbia mitume wake hivi: “Yuaja mkuu wa uli-mwengu huu, wala hana kitu kwangu.” (Yohana 12:31; 14:30; 16:11) Katika utawala usioonekana juu ya wanadamu Shetani Ibilisi hayuko peke yake. Ana malaika mashetani ambao yeye ni mwenye enzi juu yao. Mashetani wote hao wameshiriki kufanya mambo ya taratibu ya zamani’iliyopo ya jamii ya kibinadamu yawe kama yalivyo.
12 Utawala wao wenye nguvu zipitazo za kibinadamu umeleta madhara. Kuna ushuhuda unaohakikisha hilo ulioandikwa na mfume Yohana kwa habari ya vile mashetani wangetupwa wakati ujao kutoka katika rnbingu takatifu Unabii huo, unaopatikana katika Ufunuo 12:7-12, wasema:
“Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na maliaka zake Wakapigana na joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa parnoja naye. . . . Ole wa nchi na bahari! kwa maana ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.”
13. Kulingana na Ufunuo 13:4, Shetani yule “joka” amepotoa dunia yote inayokaliwa na watu akaiingiza katika ibada gani?
13 Jambo mojawapo ambamo Mdanganyaji Shetani Ibilisi, amepotoa dunia yote inayokaliwa na wafu ni kumwabudu yeye mwenyewe. Watu wanyofu lakini waliodanganywa huenda wakashtuka kujua hivyo, lakini Ufunuo 13:4 wasema yafuatayo juu ya watu wanaaingia katika siasa za.ulimwengu: “Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama.”
14. “Mungu wa taratibu hii ya mambo” anafahamika kutokana na tendo gani lake juu ya nuru ya habari njema?
14 Vilevile tunayo maneno ya mtume Paulo yanayoonyesha kwamba Ibilisi hasa ndiye anayeabudiwa na ulimwengu wa wanadamu wakijua au bila kujua. Paulo alisema hivi: “Ikiwa, sasa, habari njema tunazozitangaza zimefichwa kweli, zimefichwa kati ya wale wanaoangamia, ambao miongoni mwao mungu wa taratibu hii ya mambo amepofusha akili za wasioamini, ili mwangaza wa habari njema zenye utukufu juu ya Kristo, ambaye ni mfano wa Mungu, usipate kung’aa kwa kupenya.” (2Kor. 4:3, 4, NW) Taratibu hii ya mambo ina “mungu” wake. Uungu wake na utawala vyake pia juu ya dunia bila shaka wapaswa kuharibu roho inayaendesha taratibu ya zamani ya mambo iliyopo.
15. Sote tumepatwaje na lile ambalo “mungu wa taratibu hii ya mambo” alifanya karibu na mwanzo wa historia ya kibinadamu?
15 Karibu na mwanzo wa historia ya kibi-nadamu yeye ambaye sasa ndiye “mungu wa taratibu hii ya mambo’’ alisababisha kuanguka kwa wazazi wetu wa kwanza wa kibinadamu. Adamu na Hawa walikazwa wakose kumtii Muumba wao. Hilo lilitukia kabla sisi hatujazaliwa. Sote tumepatwa na matokeo mabaya ya tukio hilo. Katika Warumi 5:12 mtume Pa-ulo asema kweli anapoandika hivi: “Kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote walitenda dhambi.” Sisi tuliingia chini ya laana ya Mungu tufe kwa sababu tumerithi kutokamilika, udhambi na upotovu wa adili. Tulikuwa kama wafu. Kwa Mungu hatukuishi.
16, 17. Kwa sababu gani wakati huo tulikuwa kama wafu kwa Mungu, na ni nini kilichosemekana kilitenda kazi ndani yetu?
16 Tulikuwa warithi wa hasira ya Mungu, “watoto wa hasira.” Tulikuwa ‘tumefarikishwa na uzima wa Mungu.’ (Efe. 4:18) Ni kama vile Wakolosai 1:21 pia inavyosema: ‘Mlikuwa hapo kwanza mmefarikishwa, tena adui katika nia zenu, kwa matendo yenu mabaya.’ Kwa sababu ya hali hiyo ya wakati huo, Yehova Mungu hakuwa akifanya kazi ndani yetu. Basi, ni nani au ni nini kilichokuwa kikifanya kazi ndani yetu?
17 Maneno yaliyomo katika Waefeso 2:1-5, waliyoandikiwa Wakristo waliogeuzwa, yatujibua ulizo hilo: “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; ambao zamani, sisi sote nasi tuliendenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine. Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu [alitupenda].”
18. Kulingana na watafsiri wengine wa Biblia, “roho” inayotajwa katika Waefeso 2:2 inamaanisha nini, nayo iko chini ya utawala wa nani?
18 Ni nani “roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi”? Yeye ndiye mwasi wa kwanza apitaye wote wenye kumwasi Yehova Mungu, yaani, Ibilisi, “nyoka wa zamaini.” Lakini hapa yatupasa tukumbuke kwamba, katika Waefeso 2:2, neno “roho” hufahamika na watafsiri wengine wa Biblia kumaanisha kitu kisicho na utu. Wanaliona kuwa nguvu ya utendaji isiyoonekana inayoongozwa na “mfalme wa uwezo wa anga” na kwamba inatenda kazi ndani ya wale wasiomtiii Yehova Mungu. Kwa mfano, tafsiri ya Young ya Waefeso 2:2 yasema hivi: “ambayo katika hiyo ninyi wakati mmoja mlitembea kulingana na umri wa ulimwengu huu, kulingana na mtawala wa mamlaka ya hewa, ya roho inayofanya kazi sasa katika wana wa kutokutii.” (Tazama tafsiri ya Rotherham pia.) “Roho” hiyo isiyo na utu ingekuwa chini ya utawala wa mtumiaji mwovu wa “hewa.” Ingetia nguvu wale wanaojiongoza “kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu,” wakikosa kumtii Mungu.
19, 20. 1 Yohana 2:15-17 yaonyeshaja jinsi roho inayoendesha taratibu ya zamani iliyopo inavyojionyesha kuwa?
19 Twaweza kupata wazi wazo la wazi juu ya jinsi roho hiyo inayoendesha taratibu ya zamani ya mambo iliyopo ilivyo au inavyojionyesha kuwa? Na tuangalie yanayoandikwa na mtume Yohana Aonyapo Wakristo wasiwe na roho hiyo ya kilimwengu, aandika hivi: “Msiwe mkipenda wala ulimwengu wala vitu vilivyomo katika ulimwengu. Mtu ye yote akipenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo katika yeye; kwa sababu kila kitu kilichomo kafika uiimwengu—tamaa ya mwili na famaa ya macho na kujionyesha kwa mtu mali yake —hakitokani na Baba, bali chatokana na ulimwengu. Tena, ulimwengu unapita na ndivyo na iamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadurnu milele.”—1 Yoharia 2:15-17, NW.
20 Kwa hiyo roho ya taratibu ya zamani inaongoza walimwengu watamani vitu vinavyopendeza sana macho na kutamani mambo yanayofurahisha miili yao; na kwa hiyo tamaa hizo zinawafanya wajifikirie wenyewe tu. Kwa sababu ya kutamani sana kwa uchoyo vitu vinavyopendeza macho na mwili wenye dhambi, walimwengu hao wanajikusanyia mali nyingi, wapate kufurahia. maisha. Kwa sababu ya kiburi cha kuwa na mali, wanapenda kujionyesha ili wengine wawastaajabie. Hiyo inafanya wasiokuwa na mali hizo watake kujipatia pia.
21. Ni kwa njia gani Wayahudi wa karne ya kwanza walikataa kupokea roho ya Mungu, na kulingana na Warumi 1:26-32, ni mambo gani yaiyowapata waliporuhusiwa kufuata njia yao wenyewe?
21 Huko nyuma .katika karne ya kwanza ya Wakati wefu wa Kawaida kulikuwako Wayahudi waliopenda kujawa na roho inayoendesha taratibu ya mambo ya ulimwenguni pote. Hekalu alilojenga Mfalme Horode lilisimama bado katika mji wao mkuu Yerusalemu, nao waliifahamu Torati waliyopewa kupitia kwa nabii Musa. Hawakutaka kupokea roho ya Mungu iliyoonyeshwa katika Ukristo safi uliokuwa ukitangazwa wakati huo katika dunia yote iliyokaliwa na watu. Kwa hiyo Yehova Mungu aliwaacha wafuate njia yao, kama israeli wa kale wenye kuasi imani. Matokeo yao yalikuwaje? Katika Warumi 1:26-32, mtume Paulo atupasha habari, akisema:
“Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asiii kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapdta nafsini mwao malipo ya upotovu wao yaliyo haki yao. Na karna walivyokatad kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, ng hadaa? watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti; wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.”
22, 23. Ukristo ulipoenea, je! roho iliyokuwa ikiendesha taratibu ya zamani ilibadilishwa, naye Paulo alitabiri nini katika 2 Timotheo 3:1-12?
22 Katika kizazi hicho cha mitume wa karne ya kwanza W.K. imani ya kweli ya Kikristo ilitangazwa, na kwa hiyo je! roho takatifu ya Mungu isingechukua mahali pa roho iliyoendesha taratibu ya mambo ya zamani kadiri Ukristo ulivyoenea? Na je! sivyo ilivyokuwa hasa baada ya Jumuiya ya Wakristo kuanzwa na mfalme Mrumi, Konstantino Mkuu, kafita karne ya nne W.K.? Je! wakati huo basi roho mpya, safi, ya kidini haikutiwa katika jarnii ya kibinadamu yenye kusonga mbele? Sivyo kulingana na yaliyoandikwa na mtume Paulo| aliyetiwa gerezani, karibu na mwaka 65 W.K. Katika barua yake ya mwisho, aliyoandikia mwenzi wake wa muda mrefu, Timotheo, alitabiri hivi:
23 “Siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipe-nda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; . . . Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya ufauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.”—2 Tim. 3:1-5, 12.
24. Kwa sababu gani hatutaki kuwa na roho inayoendesha wanaounga mkono taratibu ya zamani?
24 Sifa zote zilizotajawa sasa hivi zaonyesha roho inayoongoza umati wa wanadamu wanaoiunga mkono taratibu ya mambo ya zamani. Je! hiyo ndiyo namna ya roho tunayotaka iongoze maisha zefu? Sivyo; sivyo tukiamua kulingana na matunda ambayo wenye kuiunga mkono taratibu ya zamani wanavuna kufokana na roho hiyo! Twataka kwa unyofu kuwa na roho tofauti, roho yenye kutenda kazi ilete tarafibu bora ya mambo, Hiyo yatutaka tuwe na roho nyingine moja tu iliyo tofauti na hiyo—roho takatifu.—Kufota Holy Spirit—the Force Behind the Coming New Order, sura ya 3.