Historia ya Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa
KITU kingine kipya kinachojulikana sana kilitokea mwaka wa 1968. The Watchtower lilitangaza “Habari Njema kwa Mataifa Yote” Makusanyiko ya Wilaya, likasema: “Ijumaa kitu kimepangwa ambacho kitawashangazeni licha ya kuwafurahisheni, kwa sababu kitasaidia sana kazi ambayo tutafanya miaka inayokuja.”
Watumishi wa Yehova walitaka kujua ni nini kitu hicho. Walipata jibu baada ya hotuba ya shauku ya msingi yenye kichwa “‘Habari Njema’ za Ulimwengu Pasipo Dini ya Uongo.” Mwishoni mwake kitabu kipya chenye kurasa 192 cha mfukoni na cha kusaidia watu wajifunze Biblia kilitolewa. Kitabu hicho, Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele (katika Kiingereza) kilipokewa furaha kuu. (Katika Kiswahili kilitokea mwaka mmoja baadaye.)
MSAADA WA WAKATI WAKE
Tangu 1960 mpaka 1965 hesabu ya mwaka ya wenye kubatizwa ilikuwa ikifika 60,000 tu. Walakini, mwaka wa 1966 hesabu ya wenye kuzamishwa ilishuka ikawa 58,904. Chini ya hali hizo angeweza kuuliza hivi, Je! kazi inaanza kwenda polepole? Baada ya muda fulani ilifahamika sivyo.
Mwaka wa 1967 wa utumishi watu 74,981 walibatizwa. Hilo lilikuwa ongezeko nalo lilitia ndugu matumaini mema. Halafu ukafika mwaka wa 1968, nacho kitabu Kweli kikatokea na mpango wa kujifunza Biblia na watu kwa miezi sita ukaanza.
Kitabu Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele kimeenezwa sana sana. Je! ulijua kwamba sasa kinachapwa katika lugha 92? Tena, katika miaka sita iliyofuata kutolewa kwa kitabu hicho, zaidi ya nakala 80,000,000 zimechapwa. Kitabu hicho kimesaidia mamia ya maelfu ya watu kupata ujuzi sahihi wa Maandiko na ‘kulishika sana neno la uzima.’ (Flp. 2:16, NW)
Kuchapwa kwa wingi kwa vitabu vya kusaidia watu wajifunze Biblia kumefanya viwanda vya Watch Tower Society viendelee kupanuka, si katika United States tu, bali pia mahali pengine duniani pote.
Katika Watchtower Farms, mboga, matunda, nyama, maziwa na jibini na kadhalika zinatayarishwa kulisha wafanya kazi wa makao makuu ya Sosaiti. Zaidi ya hilo, kati ya majumba mengi sana katika shamba Na. 1 kuna viwanda viwili. Kiwanda Na. 1 kina mashine nne za kuzunguka, na kila moja yaweza kuchapa magazeti 12,500 kwa saa moja. Katika kiwanda Na. 2 kuna nafasi ya kutosha kuweza kuweka karatasi na mashine nyingine kumi na nne licha ya vifaa vingine. Mashine sita za kuzunguka zimekwisha anza kufanya kazi huko, na jumla inakuwa mashine kumi katika viwanda hivyo viwili. Kazi itakapomalizwa kufanywa, viwanda hivyo vitakuwa na nafasi ya sakafu ya futi za mraba 400,000. Kufika Oktoba 1974, zaidi ya wafanya kazi wa kawaida na wa muda 460 walikuwa wakitumikia Watchtower Farms.
Watch Tower Society haikupanua viwanda katika United States peke yake. Mpanuko umefanywa duniani pote. Sasa Mashahidi wa Yehova wana viwanda katika Australia, Brazil, Canada, Uingereza, Finland, Ufaransa, Ujeremani, Ghana, Japan, Nigeria, Philippines (visiwa), Afrika Kusini, Sweden na Switzerland. Kwa kweli, watu wa Yehova wana viwanda vya uchapaji 37 ulimwenguni. Na, tangu mwaka wa 1955 wameongeza hesabu ya mashine zao za kuzunguka zilizopo duniani pote kutoka tisa kufika 64. Kwa hakika, viwanda vinapatikana vya kutimiza maagizo yanayoongezeka ya vitabu vinavyohusu Biblia.
Sifa yapaswa kumwendea nani kwa sababu ya mpanuko wote huo wa kitheokrasi? Haukuletwa na mipango wala jitihada za wanadamu peke yao. Sifa yapaswa kumwendea Yehova Mungu, anayekuza vitu. Yeye ndiye amefanikisha jitihada za watu katika kuzihubiri habari njema za Ufalme.—1 Kor. 3:5-7.
MPANGO WA KUNDI KAMA WA MITUME
Sasa na turudie “Jina la Kimungu” Kusanyiko la Wilaya la 1971. Sehemu za maana zaidi zilikuwa zile zilizohusu mipango ya kuongozea kundi la Kikristo la kwanza.
Baraza inayoongoza ya mashahidi wa Yehova ilikuwa imechunguza Biblia karibu na wakati huo kuhusu mpango wa kundi uliofanywa na mitume. Uhitaji ulionekana wazi wa kufanya mabadiliko fulani. Ingawa miaka iliyotangulia mwanamume mmoja Mkristo aliyekomaa ndiye aliyekuwa akitumikia kama mtumishi wa kundi, au mwangalizi-msimamizi, akisaidiwa na “watumishi” waliowekwa, mitume waliongoza kila kundi kwa kuwa na baraza ya wazee. (Matendo 20:17-28; 1 Tim. 4:14) Pia, wakati wa karne ya kwanza W.K. bila shaka baraza ya wazee ya kundi ilipokezana zamu za uenyekiti. Kwa hiyo ilionekana inafaa mwenyekiti tofauti wa baraza ya wazee atumikie kila mwaka kukiwa na zaidi ya mzee mmoja kundini.
“HII NI KAZI YA MUNGU”
Alipofikiria mpango mpya wa kundi wa wazee na watumishi wa huduma, Roger Morgan alisema hivi: “Hii ni kazi ya Mungu.” Bila shaka wengine watakubaliana naye, kwa maana huenda wakawa wamefikiria faida zinazotokana na mpango huo. Zamu za kwanza za madaraka zilianzwa Septemba 1972, na kufika Oktoba 1 mipango ya mambo katika makundi mengi ilikuwa imekwisha badilishwa. Katika visa vingi, aliyekuwa msaidizi wa mtumishi wa kundi ndiye akawa mwangalizi-msimamizi, aliyekuwa mtumishi wa kundi akawa mwangalizi wa Shule ya Kitheokrasi, na kadhalika. Huo ulikuwa uhakikisho wa kwamba Wakristo hutambua utawala wa Yehova, njia yake ya kutenda mambo katika kundi la watu wake Kila mwaka wazee kundini walipokezana zamu za vyeo mbalimbali, nao walifanya kazi pamoja kama baraza, wakifikiria hali njema ya kiroho ya kundi na uhitaji wa kushirikiana wote pamoja kulichunga kundi la Mungu alilowakabidhi.—1 Pet. 5:2.
Kumekuwa na faida nyingi kutokana na mpango wa kundi. Kwa mfano, Edgar C. Kennedy aona hiyo “yaweza kuwa njia ya kuwa imara zaidi ikiwa wakati fulani kundi litazuiwa lisiweze kupashana habari na baraza inayoongoza kwa kipindi fulani.” “Bila shaka haya ni maendeleo ya ajabu katika tengenezo la Yehova,” kasema Grace A. Estop, “nayo yaonyesha vile yeye anavyotayarisha vizuri watu wake kwa ajili ya kipindi kitakachofuata taratibu hii ya mambo.” Ndiyo sababu The Watchtower lilisema hivi juu ya makusanyiko ya wilaya ya 1972: “Kwa kweli, Yehova anaingiza watu wake waliokusanywa katika hali ya kitengenezo ambamo wataweza kuokoka Har–Magedoni waingie katika taratibu mpya ya Mungu wakiwa chini ya utawala wa kimungu.”
Angalia kwa ufupi vile kazi ya kufanya wanafunzi na kuwabatiza imeongezeka. Mwaka wa 1968 waliobatizwa walikuwa 82,842. Miaka ya 1969 mpaka 1973, jumla ya watu 792,019 walibatizwa. Jitihada zinapoendelea kufanywa kwa shauku ili kukusanya “mkutano mkubwa,” maelfu mengi yanabatizwa kila mwaka. Mwaka wa utumishi wa 1974 peke yake, watu 297,872 walizamishwa kuonyesha wakf wao kwa Yehova Mungu! Watu wa Mungu wanasisimka sana wanaposhiriki katika kazi hii ya ajabu ya kukusanya watu na kumletea Yehova sifa. Leo wako zaidi ya mashahidi wa Kikristo wa Yehova milioni mbili wanaozihubiri habari njema za ufalme wa Mungu.
(Mwisho)—Kutoka 1975 Yearbook of Jehovah’ Witnesses.