Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 10/15 kur. 476-480
  • Vita Katika “Har–Magedoni”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vita Katika “Har–Magedoni”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • KUANGAMIZWA KWA WAPINZANI WA MFALME
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 10/15 kur. 476-480

Vita Katika “Har–​Magedoni”

(Makala ya funzo la kitabu)

1. Katika taarifa ya mapema juu ya vita katika Har–​Magedoni, ni masimulizi gani ambayo mtume Yohana alitoa juu ya wale ambao wangekuwa wakipigana upande wa haki?

UWANJA wa pigano waitwa kwa mfano Har–​Magedoni. Wakati wa vita hii ni baada ya uharibifu wa moto wa Babeli Mkuu unaoletwa na zile “pembe kumi . . . na huyo mnyama.” (Ufu. 17:16 mpaka 19:9) Kama mwandikaji habari za gazeti fulani la habari, mtume Yohana anatangulia kutupa taarifa ya vita katika “Har–​Magedoni,” akiandika: “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wakweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita. Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe. Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu. Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi. Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi. Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.”​—⁠Ufu. 19:11-16.

2. (a) Kwa sababu gani Imani kuu itahitajiwa upande wa mashahidi wa Yehova duniani wakati huo? (b) “Upanga mkali” unaotoka katika kinywa cha Mfalme wa wafalme ni nini?

2 Haya “majeshi yaliyo mbinguni,” chini ya amri ya Mfalme wa wafalme, hayatajionyesha kwa mataifa yenye kupigana duniani. Hivyo itataka imani upande wa mashahidi wa Yehova wasiodhuru, wasio na silaha duniani kusadiki kwamba majeshi haya ya kimbinguni yatawaokoa katika shida yao kubwa zaidi. Hata hivyo majeshi hayo yasiyoonekana yatafanya utendaji wao vitani usikike na mataifa yote yaliyo chini ya uongozi wa Gogu wa Magogu, Shetani Ibilisi. Mfalme wa wafalme “atawachunga” mataifa “kwa fimbo ya chuma,” nao wataisikia watakapovunjwa-vunjwa kama vyombo vya udongo vya mfinyanzi. Yeye ni Neno la Mungu, na hivyo “upanga mkali” unaotoka katika kinywa chake ni maneno ya hukumu yanayotoka katika kinywa chake kwa kuuawa kwa mataifa; na yale ambayo kinywa chake husema yatafikilizwa juu ya mataifa, kuwaua.

3. (a) Litakaloyapata mataifa litakuwaje kama lile la zabibu katika shinikizo la mvinyo? (b) Hasira ya Yehova itaonyeshwa kana kwamba kwa njia gani kulingana na Maandiko?

3 Kwa kuwa Mfalme wa wafalme pia “anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi,” hili laonyesha kwamba mataifa yatakuwa kana kwamba yanapondwa-pondwa. Ili kufaa mfano huu, watatupwa katika “shinikizo la mvinyo” kubwa sana kama zabibu zilizoiva ambamo “ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi” italetwa juu yao kwa matokeo yenye kuponda. Mfalme wa wafalme na majeshi yake ya kimbinguni yenye kupanda farasi watajiunga katika kazi ya kuponda, kukanyagwa kwa shinikizo hili la mvinyo la mfano. Namna ya mkanyago wa mfano italingana na jinsi Yehova Mungu Mwenyezi anavyosema ataonyesha hasira yake kuu na ghadhabu yake yenye moto juu ya vikosi vya Gogu wa Magogu, kana kwamba kwa tetemeko la ardhi, maradhi ya kuambukia, mvua yenye mafuriko, mvua ya mawe, moto na kiberiti, pamoja na kumwagika kwingi kwa damu.​—⁠Eze. 38:18-22; linganisha Yoeli 3:9-16; Ufunuo 14:18-20.

4, 5. Ni nani, kwa wazi, atakayekuwa mshindi katika vita ya ulimwengu wote katika Har–​Magedoni? (b) Ni mwaliko gani wanaopewa “ndege wote warukao katikati ya mbingu” hata kabla ya kumalizika vita?

4 Majeshi yenye mataifa mengi yaliyojipanga vitani chini ya Gogu wa Magogu wao wa kiroho yanawezaje kutazamia kumshinda Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, anayepigania enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mungu Aliye Juu Zaidi na Mwenyezi, Yehova? Hawawezi kufanya hivyo kamwe kama tengenezo la Umoja wa wa Mataifa na mataifa yenye silaha za atomiki yasivyoweza! Atakayekuwa mshindi katika vita ya ulimwengu wote katika Har–​Magedoni ni jambo lenye kuonekana wazi. Mizoga ya adui watakaokufa ambayo Mungu Mwenyezi atajaza uwanja wa pigano inatolea ndege wote walao mizoga wanaoruka katikati ya mbingu ile iitwayo “karamu ya Mungu iliyo kuu.” Kabla vita hiyo haijapiganwa mpaka mwisho, malaika wa kimbinguni mwenye kupambwa nuru ya jua anafananishwa kama akiwatolea mwaliko ndege hawa wote waje kwenye karamu kuu ambayo Mungu anawaandalia katika Har–​Magedoni. Kwa habari ya hili, Yohana mwandikaji wetu wa habari asema:

5 “Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu; mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.”​—⁠Ufu. 19:17, 18.

6. (a) Ni kwa sababu gani ndege hawaalikwi kujilisha yule “mnyama” na “nabii wa uongo”? (b) Katika unabii wa Ezekieli, ni viumbe gani zaidi ya ndege vinavyoalikwa kwenye karamu?

6 Twaona kwamba “ndege wote warukao katikati ya mbingu” hawaalikwi wajilishe mizoga ya yule “mnyama” wa kisiasa na “nabii wa uongo” wa kisiasa. (Ufu. 13:1-8, 11-13; 16:13) Mfano unaotolewa hapa ni ule wa uwanja wa pigano wenye kujaa mizoga ya majeshi ya vita yenye kupigana tu. Si mfano unaoonyesha kufuatiwa kwa mnyama-mwitu mkali na shambulio la kijeshi juu ya “nabii wa uongo” aliye peke yake. Katika njozi ya nabii Ezekieli ya shambulio la majeshi ya Gogu juu ya watu wa Yehova waliorudishwa katika paradiso yao ya kiroho, zaidi ya “ndege wa kila namna” wanaalikwa wajilishe mizoga ya adui walioshindwa. “Kila mnyama wa kondeni” pia anaalikwa ajilishe “nyama yao walio hodari,” “farasi, na magari ya vita, na mashujaa, na watu wote wa vita.” (Eze. 39:17-20) Kudharau na kukirihi kwa Yehova wale waliopondwa na majeshi yake ya kimbinguni katika “shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi” kwaonyeshwa kwa kuacha ile mizoga ya adui waliouawa kukaa bila kuzikwa iwe chakula cha ndege na wanyama wanaokula mizoga.

7. Ufunuo sura ya 17 waelezaje juu ya mwungano wa majeshi ya kidunia chini ya Gogu wa Magogu katika kushambulia kwao Mfalme wa Yehova?

7 Tengenezo zima lenye mwungano lionekanalo la Shetani Ibilisi litakuwa katika vita. Kuunganishwa kwa majeshi ya kidunia chini ya Gogu wa Magogu kupigana na Mfalme wa wafalme wa Yehova kunafananishwa kama shambulio linalofanywa na “mnyama” aliye peke yake, mwenye vichwa saba na pembe kumi, lakini anayefananisha kundi la watu wengi. “Mnyama” huyu mwekundu sana anafananishwa kwanza akiharibu Babeli Mkuu, ile milki ya ulimwengu ya dini ya uongo. Kwa habari ya watawala wa kisiasa wenye kuchukia dini wanaofananishwa na pembe kumi za yule “mnyama” ambaye ni mfano wa kundi la watu wengi, mtume Yohana aliambiwa hivi: “Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama [Umoja wa Mataifa] nguvu zao na mamlaka yao. Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana-Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme; na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.”​—⁠Ufu. 17:13, 14.

8. (a) Ni nini maana ya kwamba Mwana-Kondoo huitwa “Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme”? (b) Nani watakaokuwa watu wa kushambuliwa na yule “mnyama” anayefananisha Umoja wa Mataifa?

8 Kupigana kwa mnyama mwenye vichwa saba, pembe kumi na mwana-kondoo kwaonekana kama pigano ambalo wenye kupigana wanatofautiana nguvu. Lakini yule Mwana-Kondoo wa mfano katika unabii huu ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme aliyewekwa na Yehova, kwa hiyo anawapita mabwana na wafalme wote ambao wameungana katika yule “mnyama” wa mfano, Umoja wa Mataifa wenye wanachama 144. Wakiwa wa kidunia, hawawezi kumwona Mwana-Kondoo kwa macho yao ya kibinadamu wapate kupigana naye moja kwa moja. Lakini duniani wanaweza kuona mabaki waliotiwa mafuta wa “hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu” walio katika mwili. Kwa sababu hawa wanamwakilisha Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana, mataifa-wanachama wa Umoja wa Mataifa wanafanya vita naye kwa kupigana wazi na mabaki waliotiwa mafuta wa warithi washirika wake wa Ufalme. Wanaoshirikiana na mabaki hawa waaminifu ni washiriki wasiohesabika wa ule “mkutano mkubwa,” wanaounga mkono kwa uthabiti enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova na wanaomfuata Mchungaji Mwema, Yesu Kristo Mwana wa kifalme wa Yehova. Hivyo wale wanafunzi walio upande wa “mkutano mkubwa” hushiriki pia pamoja na mabaki waliotiwa mafuta shambulio la Umoja wa Mataifa wenye kuchukia dini.

9. Ni ushindi wa namna gani utakaotukia wakati huo (a) upande wa Mfalme wa wafalme? (b) upande wa raia zake za kidunia?

9 Zile “pembe kumi” na yule “mnyama” mwekundu sana watashindwa kuharibu wajumbe wote waaminifu wa Mfalme wa wafalme walio duniani. Kama katika ule mfano wa unabii wa shambulio la Gogu wa Magogu, watashindwa kuifutilia mbali paradiso ya kiroho walimo wale “walioitwa, na wateule, na waaminifu” na “mkutano mkubwa” chini ya ulinzi wa Mfalme wa wafalme. (Ufu. 7:9-17; 12:17) Akiwa na majeshi ya kimalaika ya kimbinguni Mfalme wa wafalme atazishinda kwa halisi zile “pembe kumi” zinazopigana za lile tengenezo la ulimwengu la yule “mnyama.” Duniani “hao walio pamoja naye [Mfalme wa wafalme] ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu” watashinda kwa imani ya Kikristo, wasiikane kamwe ile haki ya Mfalme wa wafalme ya kutawala dunia yote, wasiikane kamwe ile enzi kuu ya ulimwengu wote ya Mfalme wa Umilele, Yehova Mungu. (Ufu. 15:3) Ule “mkutano mkubwa” wa wakazi wenzao katika paradiso ya kiroho vilevile watakataa kukubalia dai la yule “mnyama” mwenye pembe kumi, vichwa saba, la utawala wa ulimwengu juu ya dunia yote.

10, 11. (a) Je! hata hivyo, yaelekea wengine wenye kushinda kwa imani watakufa mikononi mwa adui wakati huo? (b) Ni tumaini gani litakalowatia nguvu waonyeshe imani yao thabiti kwa enzi kuu ya Yehova katika njia hii? (c) Je! yaelekea mabaki waliotiwa mafuta na “mkutano mkubwa” watafutiliwa mbali kabisa na adui wakati huo?

10 Huenda wengine kati ya wale wanaoshinda kwa imani wakaruhusiwa na Mungu Mwenye Nguvu Zote waonyeshe imani yao thabiti kwa enzi kuu Yake ya ulimwengu wote kwa kupata mauti mikononi mwa wapinzani wenye jeuri wa ufalme wa Kimasihi wa Yehova. Walakini, hili halitamaanisha wanauawa na majeshi ya kimalaika ya Yehova yaliyo chini ya Amiri-Jeshi wake, Yesu Kristo.

11 Hawa wanaokufa kwa uaminifu kwa ajili ya enzi kuu ya ulimwengu wote watakufa wakiwa waaminifu, kama washuhudiaji wa utawala wenye haki wa Yehova kupitia kwa Kristo. Watakufa kwa kibali na kuthamini kwa Yehova. Hawatatupwa katika “mauti ya pili” ya uharibifu wa milele kama unavyofananishwa na “ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti.” (Ufu. 19;20; 20:10, 14, 15; 21:8) Watakufa bila kushindwa kama Yesu Kristo mwenyewe, wakiwa na tumaini lenye kutia nguvu la ufufuo kutoka kwa wafu katika wakati wake Mungu. (Ufu. 2:10; 14:13; 20:4, 6, 11-13) Walakini, washiriki wote wa mabaki waliotiwa mafuta hawatauawa na wapinzani wenye kupigana wa ufalme wa Kimasihi wa Yehova. Pia, Ufunuo 7:9-14 watuhakikishia kwamba waokokaji wengine wa upeo huu wa “dhiki kubwa” watakuwa washiriki wasiohesabika wa ule “mkutano mkubwa.” Huenda watu mmoja mmoja wakaruhusiwa kufa, lakini sio mabaki wote na “mkutano mkubwa” wote.

KUANGAMIZWA KWA WAPINZANI WA MFALME

12. Katika Ufunuo 19:19-21, ni masimulizi gani ambayo mtume Yohana anatoa juu ya wale watakaouawa katika Har–​Magedoni?

12 Wale walio duniani watakaouawa katika “vita ya siku ile ya Mungu Mwenyezi” katika Har–​Magedoni kama wasiostahili uzima wa milele, wanaripotiwa na mtume Yohana katika Ufunuo 19:19-21. Katika taarifa hiyo ya mapema ya habari. Yohana anaandika hivi: “Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye [Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana] aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake. Yule mnyama [taratibu ya kisiasa ya ulimwenguni pote ya Shetani] akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale waliopokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu [moja wa Mataifa] yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti; na wale waliosalia waliuawa kwa upanga wake yeye aliyeketi juu ya yule farasi, upanga utokao katika kinywa chake. Na ndege wote wakashiba kwa nyama zao.”

13. Mataifa yataonyesha kuchukia dini wakati huo kwa kadiri gani?

13 Wakati wa kupiganwa kwa vita hii katika Har–​Magedoni, Babeli Mkuu atakuwa amekwisha kuuawa. Hii ndiyo sababu uharibifu wa milki hiyo ya ulimwengu ya dini ya uongo hausimuliwi hapa. Pia wakati kuchukia dini kabisa kutakapoenea katika mataifa, “wafalme” wo wote ambao huenda kwa muda wakalia kwa sababu ya kutoweza tena kuzini na Babeli Mkuu, watakuwa wametoweka, vilevile “wafanya biashara” wo wote waliolia na kuomboleza kwa sababu ya kutoweza kufanya tena biashara ya kichoyo pamoja naye, pia “kila nahodha na kila aendaye mahali popote kwa matanga, na mabaharia, nao wote watendao kazi baharini,” wote wanalia na kuomboleza kwa sababu hawawezi tena kuendelea kufanya uchuuzi wao wa kichoyo pamoja na Babeli Mkuu. (Ufu. 18:9-19) Ikiwa wanataka kusalia baada ya uharibifu wa Babeli Mkuu, itawapasa watu hao wachukie dini kabisa, isipokuwa kuabudu ile “sanamu” ya kisiasa ya “mnyama” mwenye vichwa saba, pembe kumi aliyepewa nguvu, mamlaka na kiti cha enzi na Shetani yule Joka.​—⁠Ufu. 13:1-8; 14:9-11; 16:2.

14. Je! kuharibiwa kwa milki ya ulimwengu ya dini ya uongo kutakakofanywa na watawala wa kidunia waonyesha wanaupenda ufalme wa Kimasihi wa Mungu, nao wanaonyeshaje hivi?

14 Hivyo wakati wa utimizo wa ile njozi ya pigano ya Ufunuo 19:19-21, yule “mnyama” wa mfano na “wafalme wa nchi, na majeshi yao” watakuwa wamemharibu Babeli Mkuu kwa kuonyesha chuki yao juu ya “kahaba” huyo wa kidini. Hakuwakilisha kamwe serikali ya kitheokrasi ya Yehova, wala hata sehemu yake ile iitwayo Jumuiya ya Wakristo haikufanya hivyo. Walakini, kuharibiwa kwa Babeli Mkuu kama dini ya uongo hakuonyeshi kwamba “wafalme wa nchi, na majeshi yao” wanaupenda ufalme wa Kimasihi wa Mungu. Wafalme hao wa kidunia na majeshi yao wanauchukia ufalme huo kwa sababu wanapenda enzi yao wenyewe ya kisiasa itawale dunia yote. Hivyo sasa, Babeli Mkuu akiisha kutoweka, wanaweza kukaza fikira juu ya kupigana na Yesu Kristo na ufalme wa kimbinguni ambao anaendesha.

15. (a) Ni kwa sababu gani mabaki na “mkutano mkubwa” ni wenye kuchukiza sana sana kwa “wafalme wa nchi, na majeshi yao”? (b) Ni kwa njia gani adui za watu wa Yehova wanaweza kutazamiwa kufanya vita juu yao?

15 Mabaki yaliyosalia ya warithi wa shirika wa Kristo na pia “mkutano mkubwa” wa wenzi wao wenye imani thabiti wamejifanya kuwa watu wa kushambuliwa na mataifa ya kilimwengu kwa sababu wametangaza habari njema za ufalme wa Kimasihi katika dunia yote inayokaliwa na watu kuwa ushuhuda kwa mataifa yote mpaka mwisho uje. (Mt. 24:14) Watangazaji hao wa enzi kuu ya ulimwengu wote ya Yehova ni wenye kuchukiza sana sana kwa “wafalme wa nchi, na majeshi yao.” Hivyo wanaonyesha uadui wao kwa Mfalme wa wafalme asiyeonekana kwa kufanya vita kwa njia waliyo nayo, ya kisiasa, ya kivita, ya kisheria na ya kiuchumi. Shime ya “wafalme wa nchi, na majeshi yao” itakuwa waangamize kabisa! Mfalme wa wafalme wa kimbinguni ataona tendo lao la uadui juu ya mabaki waliotiwa mafuta na “mkutano mkubwa” kama akifanyiwa yeye mwenyewe. Katika ishara ya wakati barabara kutoka kwa Amiri-Jeshi Mkuu kuliko wote, Yehova Mungu, yeye na majeshi yake ya kimalaika wataanza kupigana vita na adui wenye kumkaidi Mungu duniani.

16, 17. (a) Umoja wa adui za kidunia wa Mungu unavunjwaje katika Har–​Magedoni, kama inavyosimuliwa katika Ufunuo 19:20? (b) Ni jambo gani linaloonyeshwa na uhakika wa kwamba yule “mnyama” na “nabii wa uongo” “wangali hai” wakati tendo hili linapotukia? (c) Ni jambo gani linaloonyeshwa na uhakika wa kwamba wanatupwa katika “ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti”?

16 Hatua ya kwanza ni kuvunja umoja wa adui za kidunia. Hii yamaanisha kuivunja-vunja taratibu ya kisiasa ya ulimwengu kama inavyofananishwa na “mnyama” atokaye baharini. Mvunjo huo utafuatana na mvunjo wa Mamlaka ya Ulimwengu ya Nane, ule Umoja wa Mataifa kama tengenezo la dunia la amani na usalama wa ulimwengu, lililofananishwa na “sanamu ya yule mnyama,” na pia Mamlaka ya Ulimwengu ya Saba, yaani, Mamlaka ya Mwungano wa Sehemu Mbili za Waingereza na Waamerika, kama inavyofananishwa na “nabii wa uongo.” Kwa sababu hiyo, mtume Yohana atuambia hivi:

17 “Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti.” (Ufu. 19:20) Matengenezo haya ya kisiasa yakiwa “wangali hai” wakati tendo hili linapotukia, yaonyesha kwamba matengenezo haya ya kilimwengu ya leo yatakuwa bado yakitenda kazi wakati “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” katika Har–​Magedoni itakapoanza. Yule “mnyama” mwenye kutawala ulimwengu na pia “nabii wa uongo.” Waingereza na Waamerika, watakamatwa wakiwa katika jitihada zao za uharibifu juu ya mabaki waliotiwa mafuta na “mkutano mkubwa” katika paradiso yao ya kiroho. Kuvunjwa kwao kutafuata, na, badala ya kuharibu mabaki na “mkutano mkubwa,” matengenezo haya ya kisiasa ya wanadamu wenye kumkaidi Mungu yataangamizwa milele. Kifo chao chenye jeuri kitakuwa “mauti ya pili” ambayo kutoka hiyo hawataweza tena kuwa matengenezo. Hivyo wanafananishwa kama wakivurumishwa katika “ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti.”

18. Taratibu ya kale ionekanayo ya wanadamu itakapoondolewa, wale wenye kuokoka watakuwa na tumaini gani zuri sana?

18 Hivyo ndivyo taratibu ya kale ionekanayo ya wanadamu itakavyoondokea taratibu mpya ya Mungu ya dunia kwa kutoweka kwa jeuri kwa Babeli Mkuu wa kidini na matengenezo ya kisiasa yanayofananishwa na yule “mnyama” mwenye vichwa saba na yule “nabii wa uongo.” Utakuwa wakati wenye taabu kuliko wakati wo wote wa historia ya kibinadamu kuishi katika huo. (Mt. 24:21, 22; Dan. 12:1) Hata hivyo watakuwako waokokaji wa taabu hiyo duniani. Wenye furaha ni hawa watakaookoka waingie katika taratibu mpya ya Mungu yenye baraka!

—⁠Kutoka Kitabu Man’s Salvation Out of World Distress at Hand! sura ya 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki