Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w76 11/1 kur. 497-500
  • Kuzitazamia “Mbingu Mpya na Nchi Mpya”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzitazamia “Mbingu Mpya na Nchi Mpya”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Vichwa vidogo
  • (Makala ya funzo la kitabu)
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
w76 11/1 kur. 497-500

Kuzitazamia “Mbingu Mpya na Nchi Mpya”

(Makala ya funzo la kitabu)

1, 2. (a) Ni mabadiliko gani katika ulimwengu ambayo watu wenye umri wa miaka 70 au 80 wameona tangu mwaka wa 1914? (b) Yale ambayo wameona yamepatanaje na yale ambayo Yesu alitabiri, kama yalivyoandikwa katika Luka 21:25, 26, juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo”?

ULIMWENGU mpya na ulio bora u karibu​—⁠kadiri kizazi hiki kinavyokaribia mwisho wake. Hakuna shaka juu ya hili. Kwa neno hili “ulimwengu” tunamaanisha jamii ya kibinadamu inayoishi chini ya namna ya serikali. (Mt. 24:34; Marko 13:30; Luka 21:32) Sisi wazee wa “kizazi hiki” wenye umri wa miaka 70 au 80 tumeuona “ulimwengu” ukibadilika kuwa mbaya zaidi, ukiendelea kuharibika tangu ule mwaka wenye maana wa 1914 W.K. Sisi, tulio wa watu wote walio hai duniani leo, twaweza kushuhudia ukweli wa unabii wa Kristo wa karne ya kwanza W.K. juu ya “mwisho wa taratibu ya mambo.” Tumeona aliyotabiri tangu mwanzo wake katika mwaka wa 1914:

2 “Katika dunia taabu ya mataifa, na matata, kwa sababu bahari na mawimbi zitanguruma; watu wakizimia kwa woga, na kwa kutazamia maneno yanayokuja katika dunia; kwani nguvu za mbingu zitatetemeshwa.” (Luka 21:25, 26, Biblia ya Kiswahili ya Zaire) Ni tumaini la bure kutazamia ulimwengu wa sasa kuwa bora na kujiokoa wenyewe. Watu wenye kupenda haki wanatamani sana ulimwengu bora, jamii bora ya kibinadamu. Kwa furaha i karibu!

3. Wafuasi waaminifu wa Yesu Kristo wamewezaje kushikamana na mwendo mzuri, ijapokuwa kuharibika kwa ulimwengu unaowazunguka?

3 Wafuasi waaminifu wa nyayo za Nabii Mkuu, Yesu Kristo, wamefanya yale ambayo mtume wake Petro aliandika na kuwaambia wafanye. Wameliangalia “neno la unabii” lililohakikishwa sana kama vile wangeangalia taa inayowaka katika mahali pa giza, kuangazia mioyo yao. Kama mtume Petro alivyowaandikia waamini wenzake wa Kikristo katika barua yake ya pili: “Tuna neno la unabii lililo imara zaidi, na inawafaa ninyi kuliangalia, kama taa inayongaa katika pahali pa giza hata mapambazuko, na nyota ya asubui itasimama mioyoni mwenu. Mukijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko unafasiriwa kama mutu fulani tu anavyopenda. Maana unabii wo wote haukuletwa kwa mapenzi ya mutu, lakini watu walisema yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na [roho takatifu].” (2 Pet. 1:19-21, Biblia ya Kiswahili ya Zaire) Kuangalia kwao kwa uaminifu unabii huo ulioongozwa na Mungu kuliwawezesha washikamane na mwendo mzuri mpaka sasa. Na sasa ile siku mpya inapambazuka na ile nyota ya asubuhi imezuka, na macho yao yamebarikiwa kuona utimizo wa kisasa wa unabii wa Biblia.

4, 5. (a) Kwa habari ya unabii huo ulioongozwa na Mungu, kila mmoja wa sisi lazima afanye nini? (b) Sababu gani ya kufanya hivyo inatolewa na mtume Petro?

4 Ijapokuwa tumeona na kushuhudia mambo mengi yenye kutia imani nguvu yanayoshuhudia kutokosa kwa unabii wa Biblia, ni lazima bado tulinde imani yetu na uhakika katika unabii huo ulioongozwa na Mungu usiotimizwa bado au unaotimizwa. Hivi ndivyo hata ijapo twaishi katika “siku za mwisho” wa taratibu hii ya kale ya mambo na tumekuwa tukiishi tangu mwisho wa “majira ya Mataifa” katika mwaka wa 1914 W.K. Mtume alizitazamia hizo “siku za mwisho” akaona yafaa kuandika barua yake ya pili awaonye waamini wenzake juu ya mashambulio ya imani yao ya Kikristo yaliyotazamiwa kuja katika siku hizo zenye hatari. Baada ya kuonya juu ya kuja kwa waalimu wa uongo na kuingizwa kwa “mafundisho ya [kidini yenye kuharibu] ya imani ya uwongo” miongoni mwa watu wa Yehova, Petro aliendelea kueleza kusudi la kuandika barua yake ya pili, akisema:

5 “Wapenzi, hii ni barua ya pili ninayowaandikia ninyi; katika zote mbili ninaamsha nia zenu safi nikiwakumbusha ninyi, mupate kukumbuka maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu, na amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu. Mukijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho wenye kuzihaki watakuja na zihaka zao, wakifuata tamaa zao wenyewe wakisema: Iko wapi ahadi ya kuja kwake? kwa maana tangu baba zetu walipolala, vitu vyote vinakaa kama vilivyokuwa tangu mwanzo wa kuumbwa.”​—2 Pet. 3:1-4; 2:1, 2 Biblia ya Kiswahili ya Zaire.

6. (a) Tukikumbuka “maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu” juu ya hizi “siku za mwisho,” tutakuwa tukifikiria unabii uliotolewa kwa muda wa miaka mingapi? (b) Je! kuwapo kwa “wenye kuzihaki” kunathibitisha unabii una makosa?

6 Ili sisi leo tukanushe dhihaka ya wenye kudhihaki ambao kutokea kwao katika hizi “siku za mwisho” kulitabiriwa, ni jambo lenye haraka sana sisi waamini tukumbuke yale ambayo manabii wa Yehova walioongozwa walisema, hata ijapo haya yaliandikwa zamani kabla ya kutokea kwa wenye dhihaka wa kisasa. Tangu nabii Henoko aliyeishi kabla ya gharika mpaka Malaki nabii wa Kiyahudi aliyeishi baada ya uhamisho yapata miaka elfu tatu, manabii wa Yehova waliomtangulia Yesu Kristo wametabiri matukio na hali zinazotazamiwa kuwa ishara ya “siku za mwisho.” (Mwa. 5:18-24; Ebr. 11:5; Yuda 14, 15; Malaki, sura ya nne) Hivyo si jambo lisilotazamiwa kuona wenye kudhihaki wanaoharibu imani wanatokea katika hizi “siku za mwisho” wa taratibu hii mbovu ya mambo. Badala yake, kutokea kwao kwathibitisha usahihi wa unabii kwa kuutimiza.

7. (a) “Bwana na Mwokozi” ambaye Petro anataja ni nani? (b) Ni “amri” gani ambayo alitoa kupitia kwa mitume wake, na kwa sababu gani kwa kufikiria hivyo?

7 Kulingana na mtume Petro, jambo jingine la kukumbukwa katika wakati huu wa mwisho katika historia ya kibinadamu ni “amri ya Bwana na Mwokozi iliyoletwa na mitume yenu.” (2 Pet. 3:2) Yesu Kristo ndiye “Bwana na Mwokozi” anayetajwa hapa. (2 Pet. 3:18) Kupitia kwa mitume wake waliochaguliwa, yaani, “mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo,” na pia mtume Paulo, aliwapa amri wafuasi wake wote ili waendelee kukesha na kujihadhari na manabii wa uongo na akina Masihi au Makristo wa uongo. Kwa kuwa aliacha wanafunzi wake wasijue siku na saa barabara ambayo angekuja tena kufikiliza hukumu za Mungu juu ya wasioaminika na waovu, alikuwa mwenye kufikiria sana katika kuwaamuru waendelee kuwa tayari na kukesha. (Ufu. 21:14; Mt. 24:36-44; 25:13) Haiwapasi waache dhihaka ya wo wote ambao wamepoteza imani iwageuze.

8. Wanapouliza, “Iko wapi ahadi ya kuja kwake?” wenye kudhihaki wangemaanisha nini?

8 Wenye kudhihaki walitazamiwa kuuliza ulizo hili lenye kupinga, “Iko wapi ahadi ya kuja kwake?” Ndiyo, wangesema, namna gani ahadi hii ya kuwapo kwake? Uko wapi ushuhuda wa utimizo wake?

9, 10, (a) Je! wangekuwa wakimaanisha “kuja” (kuwapo) kwa nani? (b) Mtume Petro alifanya nini ili aamshe taraja lenye shauku la “kuja” kwa Kristo katika mioyo ya waamini wenzake?

9 Je! wangekuwa wakimaanisha “kuja” (kuwapo) kwa nani? Kwa wazi ni “kuja” kwa Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, ambako mtume Petro alisema juu yake mwanzoni mwa barua yake ya pili. Mtume Petro hakukutazamia “kuja” huko kwa Yesu Kristo katika wakati wake duniani, hata hivyo hakutaka akose kuliamsha taraja lenye shauku la kuwapo huko kulikoahidiwa katika mioyo ya waamini wenzake. Kwa sababu hiyo, aliandika hivi:

10 “Ndiyo, nitatenda kwa bidii hata kwa kila wakati nyuma ya kufa kwangu mupate kukumbuka maneno haya. Maana hatukufuata hadizi zilizotengenezwa kwa hila, wakati tulipowajulisha ninyi uwezo na kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo, lakini sisi wenyewe tuliona ukubwa wake. Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, wakati sauti ilipokuja kwake toka utukufu mukubwa: Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninayependezwa naye. Nasi tulisikia sauti hii ikitoka mbinguni, wakati tulipokuwa pamoja naye katika mulima mutakatifu. Nasi tuna neno la unabii lililo imara zaidi.” 2 Pet. 1:15-19; Mt. 17:1-9, Biblia ya Kiswahili ya Zaire.

11. (a) Mataraja yenye makosa juu ya “kuwapo” kwa Yesu Kristo yametokezaje mashaka mengi? (b) Kuanzia na mwaka wa 1870, Charles Taze Russell alifahamu nini juu ya kuja kwa pili kwa Kristo na “kuwapo” kwake?

11 Ikiwa wenye dhihaka wa kisasa wanafikiria kufika na kuwapo kunakoonekana kwa Yesu Kristo katika mwili wanakosea sana. Walidanganywa na mafasirio yenye makosa ya unabii yanayoenea katika Jumuiya ya Wakristo leo. Wakati wa karne ya kumi na tisa W.K. kulikuwako matabiri fulani juu ya kuja kunakoonekana kwa Bwana Yesu Kristo katika mwili katika miaka fulani. Kutotimizwa kwa matabiri hayo katika tarehe zilizotangazwa bila shaka kulileta suto jingi juu ya fundisho la Biblia la kuja kwa pili kwa Yesu Kristo na kuwapo kwake kama Mfalme wa kimbinguni. Kulitokeza mashaka mengi juu ya ukweli wa fundisho hilo, uhakika wa kuja na kuwapo huko kwa Kristo. Kuanzia na mwaka wa 1870 Charles Taze Russell na wanafunzi wenzake wasio wa kimadhehebu wa Maandiko yaliyoongozwa na Mungu walifahamu kwamba kuja kwa pili kwa Kristo kusingeonekana na macho ya kibinadamu, kungekuwa katika roho, na kwamba kuja kungeanza kipindi kijulikanacho kama “kuwapo” kwake, au (Kigiriki) pa·rou·siʹa.​—⁠Mt. 24:3, margin, ERV (1881)

12, 13. (a) Kulingana na kuhesabu kwa Russell, “kuwapo” kwa Kristo kulikuwa kumeanza wakati gani? (b) Nani wameiona “ishara” inayoshuhudia kuwapo kwa Kristo kuanzia mwaka wa 1914 W.K.?

12 Kulingana na tarehe yenye makosa iliyokuwa imefanyizwa kutokana na Biblia ya King James Authorized Version, Russell alihesabu kwamba “kuwapo” kwa Kristo kulikuwa kumeanza katika mwaka wa 1874 W.K., bila kuonekana na macho ya kibinadamu na kuonwa tu kwa macho ya imani. Hii ndiyo sababu, alipoanza kuchapa gazeti jipya la kidini kwa kutetea dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo, Russell aliliita Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence. Walakini, matukio duniani tangu mwisho wa “majira ya Mataifa” yamekuwa yakitimiza unabii wa Biblia na kuthibitisha kwamba “kuwapo” au parousia kulikoahidiwa kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme kulianza kwanza karibu na Oktoba 4/5, 1914 W.K. Tangu wakati huo peke yake imekuwa sahihi kusema juu ya “kuwapo” kusikoonekana, kwa kifalme kwa Kristo kwamba kumetukia. Sisi wazee wenye umri wa miaka 70 au 80 tumeona yakitimizwa karibu mambo yote yaliyotabiriwa na Yesu Kristo katika kujibu ulizo aliloulizwa na mitume wake:

13 “Mambo haya yatakuwa lini, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo [Kigiriki: pa·rou·siʹa] kwako na ya mwisho wa taratibu ya mambo?”​—⁠Mt. 24:3, NW; Rotherham; Young; Diaglott; margin.

14. Ni nini kimezuia wale wanaoshikamana na makanisa ya Jumuiya ya Wakristo wasifahamu “kuwapo” kusikoonekana kwa Yesu Kristo?

14 Mpaka leo hii makanisa yenye madhehebu ya Jumuiya ya Wakristo yanashikilia tafsiri ya kawaida ya neno la Kigiriki pa·rou·siʹa kama “kuja.” Wakitazamia kuja kwake kwa kuonekana katika mwili, wanakataa kupambanua “kuwapo” kusikoonekana, kwa kiroho kwa Yesu Kristo katika mamlaka ya Ufalme tangu kumalizika kwa Majira ya Mataifa katika mwaka wa 1914. Huku kumewatolea nafasi wenye dhihaka wadhihaki lile wazo la “kuwapo” kulikoahidiwa kwa Kristo na kutoa sababu ya kukataa kwao kusadiki, wakisema: “Ku wapi kuwapo [pa·rou·siʹa] kwake kulikoahidiwa? Kwani, tangu babu zetu walipolala katika mauti, mambo yote yaendelea barabara kama tangu mwanzo wa kuumba.”​—2 Pet. 3:4, NW.

15. (a) Wenye kudhihaki wanabisha juu ya msingi gani kwamba Yesu Kristo hajarudi? (b) Ni kwa sababu gani wana makosa?

15 Wenye dhihaka hao wanaona wanaume wakioa na wanawake wakiozwa, sawasawa kama tangu siku za wazao wa Adamu na kuendelea. Wanaona vitoto vikizaliwa kama tangu wakati wa kuzaliwa kwa Kaini na kuendelea. Wanadamu wanaendelea kufa, sawasawa kama babu zetu walivyokufa. Hakuna kikomo cha mwendo wa kufa, kama kile kinachotazamiwa kutukia duniani baada ya kuanza utawala wa Kristo wa miaka elfu. Ufufuo wa kuja kwenye uzima katika dunia ya Paradiso haujatukia bado, kama ule walioahidiwa wafu wa kidunia ambao wamekombolewa na Yesu Kristo. Dhambi na pia mauti yaendelea kutawala wanadamu. Hivyo, kwao wale wenye dhihaka wasio na imani, mambo yote yaendelea barabara kama tangu mwanzo wa kuumbwa kwa kibinadamu na tangu wazee wao walipokufa. Basi, kwa maoni yao, hatujaingia bado katika “wakati wa mwisho”; Yesu Kristo hajarudi bado; hajaanza jambo hilo kama kuwapo. Wanasema yote haya, ijapokuwa utimizo wote wa unabii wa Biblia tangu mwaka wa 1914 W.K. unaothibitisha kuwapo kwake kusikoonekana tangu wakati huo. Hivyo wenye dhihaka hao wanakawiza tu “kuwapo” kwa Bwana Yesu Kristo katika akili zao.​—⁠Dan. 12:4; Mt. 24:3, NW.

16. Ni nini kusudi la kudhihaki, lakini sababu gani kunakosa shabaha yake?

16 Wenye dhihaka waliotabiriwa kutukia “siku za mwisho” ni kutia na makasisi wenye kujulikana sana wa Jumuiya ya Wakristo. Kusudi la kudhihaki ni kuutilia shaka unabii wa Biblia au kuharibu imani na kusadikishwa kwa mashahidi wa Kikristo wa Yehova, mabaki ya Israeli wa kiroho na vilevile “mkutano mkubwa” wa waamini wenzao wenye imani thabiti. Lakini, wakilitii onyo la mtume Petro, watangazaji hawa wa kuwapo kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme wa kimbinguni hukataa kuharibiwa imani yao. Wanategemea kutoshindwa kwa neno la Mungu, hata likitolewa kwa namna ya unabii au utabiri wa mambo yajayo. Wanajua kwamba wakati Mungu anaposema jambo fulani kwa kuamuru, lazima lifanywe, lazima litukie. Wanaamini yanayosemwa na Zaburi 115:3: “Lakini Mungu wetu yuko mbinguni, alitakalo lote amelitenda.” Na kwa kuwa wenye dhihaka wanataja “kuumbwa” katika hoja yao, waamini wanyofu wa Yehova wanajua kwamba, alipopendezwa kuziumba mbingu na dunia, neno lake lililosemwa lilitimia, likaleta matokeo​—⁠Kutoka Kitabu Man’s Salvation Out of World Distress at Hand!, sura ya 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki