Sababu Mtu wa Kiroho “Hatambuliwi na Mtu”
◇ Mtume Paulo aliandikia Wakristo katika Korintho akawaambia: “Mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.” (1 Kor. 2:15) Hiyo ina maana gani? Kwa msaada wa roho ya Mungu, mtu wa kiroho anaweza kukadiri mambo vizuri. Lakini, yeye mwenyewe hawezi kuchunguzwa kikweli na wale wasio na ufahamu wa kiroho. Watu wasio wa kiroho watakata maneno vibaya kumhusu yeye, kwa sababu wana msingi mbaya. Ndivyo walivyofanya kwa habari ya Kristo Yesu, kama Isaya 55:3, 4 ilivyotabiri. Kwa hiyo, mtu wa kiroho hawezi kabisa ‘kutambuliwa na mtu’ ye yote, yaani, na mtu ye yote asiye wa kiroho.