‘Wakati Ambao Nchi Iigawanyika’
◇ Biblia inasema hivi: “Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza ni Pelegi, maana katika siku zake nchi iligawanyika.” (Mwa. 10:25) Kulingana na vile tunavyoweza kuona katika Maandiko, mgawanyiko huo unaotajwa ulitokea wakati Yehova Mungu alipochafua lugha ya wajenzi wa Babeli na kuwatawanya. (Mwa. 11:1, 7) Jina Pelegi lina maana ya “mgawanyiko.” Lakini, inatupasa tujue kwamba mgawanyiko huo haukutokea alipozaliwa, bali “katika siku zake.” Kwa hiyo ikiwa yeye aliitwa Pelegi alipozaliwa, jina lake lilikuwa likitoa unabii wa mgawanyiko mkuu uliotukia muda wa maisha yake.