Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w77 8/15 uku. 369
  • Kujizuia kwa Wanawake Wasiingiliwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujizuia kwa Wanawake Wasiingiliwe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
w77 8/15 uku. 369

Kujizuia kwa Wanawake Wasiingiliwe

● Baada ya kuchunguza visa 36 vya wanawake waliokuwa karibu kuingiliwa, na vingine 36 vya wanawake walioingiliwa hasa, Frank J. Javorek wa Denver General Hospital alitaja sababu kubwa zilizofanya wengine waingiliwe kabisa na wengine wasiingiliwe. Kulingana na gazeti “Science News,” mambo makubwa yaliyofanya wengine waingiliwe na wengine wasiingiliwe ni “kama mwenye kuingiliwa alipiga makelele au akapaza sauti kuomba msaada, na kama alijaribu kukimbia. Jambo jingine la maana zaidi ni jinsi mtaa anamoishi mtu huyo ulivyo na kama yeye alikuwa macho kabisa wakati aliposhambuliwa.”

Bila shaka, katika hali fulani mtu hasikiwi anapopiga makelele, tena inakuwa haiwezekani kukimbia. Lakini, wanawake 86 kwa 100 waliopiga makelele, na kukimbia pia, hawakuingiliwa.

Linalopendeza ni kwamba, sheria ya Mungu kwa Waisraeli wa kale ilisema wazi kwamba, ikiwa msichana aliyeposwa alifanya uasherati na mwanamume, wote wawili walipaswa kuuawa. Lakini, ikiwa msichana alipiga makelele kuomba msaada, lakini kusiwe na mtu wa kumsaidia, alionekana hana hatia kwa sababu ya makelele yake. Basi mwanamume peke yake ndiye aliyeuawa, naye msichana akaachiliwa.​—Kum. 22:23-27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki