Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 2/1 kur. 3-4
  • Unaweza Kupata Amani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kupata Amani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Acha “Amani Ya Mungu” Ilinde Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Amani ya Kimungu kwa Wale Wanaofundishwa na Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 2/1 kur. 3-4

Unaweza Kupata Amani

NI NANI asiyetaka amani? Inaweza kuwa furaha kubwa kuona jamaa, jirani, makabila na mataifa yakiweza kuwa na amani na usalama wa kiasi fulani. Lakini, katika ulimwengu huu amani inaharibiwa mara nyingi wakati watu wanapogombana sana. Labda wewe unashangaa ukiuliza kwa nini ni vigumu sana kupata amani ingawa inatamanika sana.

Mapigano yanatokea hasa wakati watu wanapopuza maongozi mazuri ya Mwanzishi wa amani, yaani, Muumba wa mwanadamu. Yakobo mwanafunzi Mkristo alionyesha hivyo, akasema: “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu? Mwatamani, wala hamna kitu; mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.”​—Yak. 4:1-3.

“Mungu wa amani,” Yehova, anapinga choyo ya namna zote. Wanaomtegemea yeye kwa imani hawatamani vitu vya watu wengine, kwa hiyo hawawi na pupa wakijaribu kupata vitu visivyo vyao. Wanafuata shauri hili la Biblia: “Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.”​—1 Kor. 10:24; Flp. 4:9.

Ebu fikiri uone ni mapigano mengi namna gani ambayo yangeweza kuepukwa kama watu wote wangetanguliza faida za wengine mbele ya zao wenyewe. Hakuna mtu angedanganywa, na kwa hiyo hakuna mtu angeona uchungu. Mtu asipokuwa na choyo, wenzake pia hawawi na choyo. Kwa mfano, baba akijinyima mambo fulani anayopenda ili kufaidi mkewe na watoto, jamaa inakaribiana zaidi. Mfano wa baba wa kutokuwa na choyo unaleta hali iyo hiyo kati ya washiriki wengine wa jamaa. Basi, badala ya kuwa na ugomvi na ubishi, jamaa inakuwa na amani na utulivu. Washiriki wa jamaa wanatafuta nafasi za kutendeana mambo.

Faida zinazoweza kutokea katika jamaa kusipokuwa na choyo zinaweza kutokea pia kati ya watu wengi. Hali hiyo inaweza kuondoa mtengano unaoletwa na ukabila, majimbo na utaifa. Labda wewe umeona kwamba mtengano huo haumo kati ya Wakristo wanaoitwa Mashahidi wa Yehova. Duniani mwote wanajulikana kuwa watu wasiojiingiza katika mizozo ya ulimwengu. Umoja wao ulio mwingi ajabu unaonekana hasa katika makusanyiko yao makubwa. Mtu mmoja anayeishi pwani ya magharibi ya United States aliandika hivi: “Ingawa mimi si mshiriki wa madhehebu hii, nimefanya uchunguzi mzuri na wa unyofu nikaona ni lazima niache kuwa na mashaka juu ya jinsi watu hawa wamejitoa kabisa kuifuata njia yao ya maisha ya Kikristo . . . Kila mwaka mamia ya magazeti ulimwenguni mwote yamekuwa na makala zenye kueleza utaratibu na adabu zilizo na watu hao pamoja na watoto wao, wanapokuwa na makusanyiko ya mataifa yote.”

Lakini, hapo kwanza wengi ambao sasa ni Mashahidi wa Yehova walikuwa wakichukia sana watu au mambo bila sababu nzuri. Hawakuwa wenye amani na Mungu wala na wanadamu wenzao. Lakini walipojifunza Biblia walisaidika kuwa na maoni tofauti sana. Wakawa tofauti na watu wengi walioishi katika nchi moja na Yesu katika karne ya kwanza W.K., kwa hiyo wakayafahamu “yapasayo amani.” (Luka 19:42) Kwa sababu ya mambo waliyojifunza, walitubia mawazo na matendo yao ya zamani, wakageuka kabisa na kuanza kumtumikia Mungu wakiwa wanafunzi wa Yesu Kristo. Hivyo wakawa wenye amani na Muumba.

Juu ya vile mtu anavyokuwa baada ya kupata amani hiyo, Biblia inasema hivi: “Amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu.” (Flp. 4:7) Utulivu unaokuja kwa sababu ya kuwa na uhusiano unaokubaliwa na Muumba unalinda moyo na nia ya mtu asije akawa na wasiwasi mwingi mno wa kutafuta mahitaji yake. Mtu huyo hasumbukii sana riziki ya kila siku, kwa maana anakuwa na hakika Mungu atajibu sala zake na kumbarikia jitihada zake apate riziki. Basi moyo wake na akili zinatulia.

Tena, mtu anapofuata Neno la Mungu, anaendelea kuwa na dhamiri safi. Yeye hawi na wasiwasi wala mvurugo wa akili unaotokea kwa sababu ya kufuata njia mbaya kwa makusudi. Anajisikia kama mtunga zaburi: “Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, maana Wewe, [Yehova], peke yako, ndiwe unijaliaye kukaa salama.”​—Zab. 4:8.

Mtu huyo anakuwa na uhusiano mzuri zaidi pamoja na wanadamu wenzake kwa sababu hana choyo. Wenzake wakijua kwamba anapenda kuwaona wakiwa na hali njema, wao wenyewe wataelekea zaidi kumtendea mambo mema na ya uaminifu.

Mtu akiwa na uhusiano unaokubaliwa na Yehova Mungu, anakuwa pia na ahadi ya kupata amani wakati ujao. Sisi hatuwezi kuubadili ulimwengu wala kuiondoa choyo inayoleta mapigano. Lakini, Muumba atahakikisha kwamba maneno ya Isaya yametimizwa: “Nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.”​—Isa. 2:4.

Tunaweza kutazamia maneno hayo yanayohusu amani yatimizwe kabisa wakati gani? Wewe unawezaje kuwa kati ya wale watakaofurahia amani wakati ujao? Mashahidi Wakristo wa Yehova walio katika eneo lako wanaweza kukujibia maulizo hayo kwa kutumia Biblia. Ikiwa hujaonana nao karibuni, inafaa uzungumze nao habari za Maandiko wakikutembelea tena. Utajionea mwenyewe jinsi unavyoweza kupata amani sasa na wakati ujao pia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki