Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 5/15 kur. 6-10
  • Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NAMNA MTU ANAVYOWEZA KUPATA AMANI
  • KUFANYA AMANI NA WENGINE
  • AMANI YA ULIMWENGU
  • Acha “Amani Ya Mungu” Ilinde Moyo Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Jinsi Wewe Unaweza Kuona Amani ya Kimungu kwa Ukamili Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Amani ya Kweli—Kutoka Chanzo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Amani​—Unaweza Kuipataje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 5/15 kur. 6-10

Jinsi Ambavyo Amani Yaweza Kupatikana Duniani

AMANI ya ulimwengu haiwezi kupatikana tu kwa jitihada za kupunguza silaha, au kwa mikataba ya amani, hata kwa kuacha vita vya maneno au vita vya silaha. Hata wateteaji wa amani sasa wanasema kwamba amani inapaswa kuwa na msingi katika ujamii na vilevile katika maisha ya jamaa. James Laue wa Shule ya Shughuli ya Amani ya Kitaifa asema hivi: “Kushikamanisha [amani] na kufanya amani katika ujamii kumetusaidia kufafanua amani ni nini. Kuendelea kwa njia za kusuluhisha mapigano yanayotokea kila siku, nyumbani au shuleni, kwaweza kusaidia kuleta amani kati ya mataifa.”

Hilo ni jambo gumu sana kufanya. Akiandika katika gazeti To the Point International chini ya kichwa “Naam, Amani ya Ulimwengu Ni Shughuli ya Kila Mtu,” George Mikes anatoa maoni haya:

“Tumefunzwa tuwapende jirani zetu. Jambo ambalo ni gumu sana kulifanya tena linachosha. Unaweza kumpenda karibu kila mtu isipokuwa jirani yako. Kwanza kabisa, jirani wa kila mtu anachukiza, hapendeki na ni mtu mwenye kujitia katika mambo [yako]—hali mtu anayeishi milango michache mbele kidogo anapendeka, anapendeza na ni mwenye heshima. Iwapo unaishi katika Chelsea [sehemu moja ya nchi ya Uingereza], hutakuwa na magomvi yo yote na wakaaji wa Turnham Green [sehemu nyingine ya nchi ya Uingereza] nawe utakuwa na uhusiano mzuri sana na watu katika Crouch End [sehemu za mbali]. Vivyo hivyo Waingereza wanawapenda watu wa Australia na wa New Zealand​—katika pembe ile nyingine ya ulimwengu—​walakini sikuzote hawajawapenda Wafaransa au Wajeremani.”

Kwa hiyo haiwezekani kukawako amani ya ulimwengu tusipopatana, kwanza, na wale walio karibu zaidi nasi. Je! kwa kweli kuna ‘ufundi’ fulani utakaotokeza jambo hilo? Hata kidogo. Kwa hakika, wanadamu ni wenye akili sana na sana sana ni wajuzi wa ufundi. Wameutumia katika kila jitihada, kutia ndani kufanya amani. Kwa ujumla, wamefaulu kadiri fulani karibu katika kila jambo​—sayansi, siasa, biashara, uuzaji na utangazaji wa vitu—​isipokuwa kufanya amani, ambako kunatia ndani uhusiano wa karibu zaidi wa kibinadamu. Ufundi hautafaa katika jambo hilo. Sababu gani hivyo? Kwa sababu amani, ambayo kwa kweli huanzia nyumbani, lazima itoke moyoni. Amani inatia ndani, si kuvumiliana tu, au kuwa na nguvu za silaha zinazolingana, bali upendo wa kweli na ufahamu kumwelekea mtu yule mwingine au jamaa ile nyingine au ujamii au taifa​—bila kujali kabila, dini au cheo cha mtu katika ujamii.

Je! jambo hilo linaweza kufikiwa? Katika wakati huu, ni wachache tu wanaoweza. Walakini wachache hawa, hata hali yao ya ulimwengu iweje, wanaweza kuwa na amani sasa. Wanaweza kuendeleza amani katika utendaji wanaouongoza. Namna gani?

NAMNA MTU ANAVYOWEZA KUPATA AMANI

Kwanza, mtu hufanya amani pamoja na Mungu kwa kuangalia Biblia yeye mwenyewe na kwa kujitahidi kujua mpango ambao Mungu amefanya wa kumkaribia Yeye. Mtu hawezi kufanya jambo hilo kwa funzo lo lote la kijuu-juu. Ni lazima achunguze. Ni lazima ‘ahakikishe mambo yote’ na anapaswa ‘kushikilia sana lililo jema.’​—1 The. 5:21, NW.

Mtu anayefanya hivyo huja kutambua, kwanza kabisa, kwamba yeye ni mkosaji naye anahitaji msaada. Ni lazima akubali kwamba yeye hana uwezo ndani yake wa kufanya matendo yatakayompendeza Mungu na kwamba yeye hana hekima ya kuleta amani ya kweli, yenye kudumu kwa mtu ye yote. Njia ya pekee ya kupata amani pamoja na Mungu ni kuondoa kizuizi cha amani​—dhambi yetu wenyewe inayotuzuia njia. Jambo hilo si gumu kufanya. Halihitaji hekima au uweza mwingi. Imani katika Mungu na katika ahadi zake ndiyo njia rahisi, na nyepesi. Njia hiyo imewekwa wazi sana katika kitabu cha Biblia cha Warumi, sura ya 5, ambapo twasoma hivi:

“Kwa maana hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu. Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema. Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.”​—Rum. 5:6-10.

Kupatanishwa huko na Mungu kunatokeza amani pamoja na Mungu. Mtume Paulo anaandika hivi: “Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na tuwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.” (Rum. 5:1) Nayo si mapatano ya kitambo tu au amani ya muda, na kusahau dhambi za wakati uliopita ambazo mtu alifanya. Amani hiyo ni yenye kuendelea pamoja na Mungu, kupitia kwa Kristo, ikimsaidia mtu kuanzia wakati huo na kuendelea kutembea katika njia inayodumisha amani. Mungu anakuwa rafiki bora zaidi wa mtu huyo.​—Linganisha Yohana 15:15.

Yesu alisimulia amani hiyo kwa mitume wake, akisema hivi: “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo.” (Yohana 14:27) Ulimwengu unatoa kadiri fulani ya amani kupitia kwa rafiki wachache, anasa, mali, kujulikana, cheo, kupandishwa cheo, kadiri fulani ya utulivu, na kadhalika, vilevile kupitia kwa taratibu zake za filosofia na dini ya uongo. Walakini amani ambayo Kristo humpa mtu anayeonyesha imani kweli kweli katika dhabihu yake yenye kuondoa dhambi ni tofauti sana. Kwanza kabisa, mtu huyo anapata dhamiri safi, iliyotulia, amani ya kweli ya ndani, ya akili, maelekeo yenye amani yanayotokeza uhusiano mzuri na wengine, kusudi kubwa zaidi maishani na tumaini imara kwa wakati ujao.

Namna gani? Mtume Petro anatuambia kwamba wakati mtu anapoonyesha imani katika “habari njema,” na kuweka wakf maisha yake kwa Mungu na kubatizwa, tendo lenyewe la kubatizwa ni “ombi linalofanywa kwa Mungu ili kupata dhamiri njema.” (1 Pet. 3:21, NW) Kwa sababu ya kurithi hali yenye dhambi, katika wakati uliopita, mtu, amekuwa na dhamiri mbaya, ambayo ilimlemea kama mzigo mkubwa. Juu ya hilo, Yesu alisema hivi: “Heri wenye huzuni [wanaohuzunishwa na hali yao ya umaskini wa kiroho]; maana hao watafarijika.” (Mt. 5:4) Yeye anatoa mwaliko huu kwa wote: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.”​—Mt. 11:28.

Inaburudisha kama nini, pia, kushiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme ambayo Yesu aliianzisha alipokuwa hapa dunia ambayo katika hiyo aliwazoeza wanafunzi wake na ambayo alisema ingefikia upeo wake mwishoni mwa taratibu hii ya mambo, na ndiyo sasa! (Mt. 4:17; 9:35; 10:7; 24:3, 14) Kufanya mapenzi ya Mungu katika njia yake ni jambo lenye kujenga kiroho, lenye kutosheleza na msaada wa kufanya amani na Mungu. Mashahidi wa Yehova wanapoenenda katika utumishi wake, ‘kwa kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani wanaweza kuwa na hakika ya uangalizi na ulinzi wake katika kila hali.​—Efe. 6:14-16.

Mtume Paulo anazungumza juu ya mioyo ya Wakristo kuwa ‘imenyunyizwa iache dhamiri mbaya.’ Hiyo ni kwa sababu Mungu amesema hivi: “Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.” (Ebr. 10:17, 22) Akiwa amefarijiwa dhamiri, Mkristo wa kweli anaweza kuwa na amani ya kweli ya ndani, amani ya akili. Yeye hahangaiki sana juu ya hali za ulimwengu. Hata magonjwa na kifo haviogopeshi kama zilivyoogopesha wakati mmoja. Maarifa ya mpango wa ufufuo yanaondoa woga huo.​—1 The. 4:13, 14.

KUFANYA AMANI NA WENGINE

Mtu aliye wakf na kubatizwa yu katika hali nzuri ya kufanya amani na wengine. Lo lote afanyialo mtu mwenzake lapaswa kufanywa kwa upendo. Wakati wo wote asiache choyo, pupa, kiburi, wivu au tamaa ya kulipa kisasi iwe kichocheo chake. Watu huona unyofu wa moyoni, ukarimu, upendo wa kweli, na, kisha, wanaitikia kwa kuonyesha sifa kama hizo. Yesu alitaja kanuni ambayo kwayo mtu anaweza kuwa mwendelezaji wa amani. Yeye alisema hivi: “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.​—Luka 6:38.

Upendo huo na kutoa huko, iwapo vitaendeleza amani ya kweli, vyapaswa kuwa kwa wingi, bila upendeleo au bila kuonea. Twapaswa kuwa jirani wa kweli kweli kwa watu wote ambao twajipata kuwa kati yao, bila kujali dini yao, taifa, rangi au cheo cha ujamii. Mtume Paulo alitaja kwamba hilo ni jambo la lazima la Kikristo. Yeye alisema hivi: “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote” na, “Kama yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” (Ebr. 12:14; Rum. 12:18) Yesu alionyesha kwa mfano wenye nguvu uhitaji wa kuwa jirani mwema, mwenye kusaidia kila mtu, kuchukua wakati kujulisha “habari njema” kwa wote, na kutia bidii na kutumia mali kusaidia wengine katika taabu, kwa kadiri hali inavyoruhusu. Yesu alionyesha jambo hilo kwa nguvu sana kama iwezekanavyo kwa kumwonyesha mwanamume fulani Msamaria kuwa jirani mwema, kwa kuwa kulikuwako uadui kati ya Wayahudi na Wasamaria.​—Luka 10:29-37.

Namna gani ikiwa jirani zetu hawauonyeshi upendo kama huo? Mkristo hana la kufanya juu ya hilo, walakini anaweza kuendelea kuwa mwenye amani yeye mwenyewe. Iwapo mtu mwingine ye yote anataka kuiharibu amani au kufanya vita, Mkristo anaweza kumtegemea Mungu kupata msaada wa kuendeleza usawa na kuepuka kulipa kisasi. Shauri la Biblia ni hili: “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. . . . Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu.” (Rum. 12:17-19) Hatari ya kweli ikimwelekea, Mkristo huweka tumaini katika Mungu kwamba madhara yenye kudumu yasije juu yake. Mtume Paulo aliueleza uhakika huo, akisema hivi: “Nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka . . . wala wenye uwezo, . . . wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”​—Rum. 8:38, 39.

AMANI YA ULIMWENGU

‘Walakini ni namna gani’ huenda mtu akauliza, ‘kuishi huko kwa amani kutaleta amani ya ULIMWENGU?’ Ikiwa peke yake, amani yetu ya binafsi haitaweza. Lakini Mungu wa Wakristo ndiye ‘Mungu atoaye amani’ naye Kristo Yesu ndiye “Mfalme wa amani.” (Rum. 16:20, NW; 1 Kor. 14:33; Isa. 9:6) Wale ambao hawataki amani kabisa, ambao ni wenye kuharibu amani wakati wote, wale wasioweza kuwa na amani isipokuwa tu wakitawala, ni lazima waondolewe duniani. Mungu anasema ‘atawaharibu hao waiharibuo nchi,’ kama alivyofanya wakati mmoja uliopita, wakati wa gharika ya duniani pote ya siku za Nuhu. (Ufu. 11:18; Mwa. 6:12, 13) Kuna bei ya amani, nayo Biblia yasema kwamba, “mtu asiye haki ni fidia ya wenye haki; naye afanyaye hila ni badala ya watu wa adili.” (Mit. 21:18) Mungu atawaharibu waovu wote.

Mfalme wa Amani, mfalme wa Mungu wa dunia yote, atakomesha mapigano yote ya kitaifa. Kama vile Mungu alivyofanya katika kuwalinda watu wake Israeli katika nyakati za kale, ndivyo yeye, kupitia kwa Mfalme wake aliyeteuliwa, atakavyofanya duniani pote, na katika njia yenye kudumu. Zaburi ya 46, ikisimulia ulinzi wa Mungu juu ya Yerusalemu kutokana na mataifa adui yaliyowazunguka, inatoa mfano wa atakayofanya kwa ajili ya wenye amani. Inasema hivi: “[Yehova] wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. Njoni myatazame matendo ya [Yehova], jinsi alivyofanya [maajabu] katika nchi. Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari [ya matumizi ya vita].”​—Zab. 46:7-9.

Kukiwa na amani na upatano duniani, kazi zenye kufaidi dunia zitaweza kufanywa pasipo kuwa na kizuizi, utajiri wa ujamii hautatumiwa kwa makusudi ya vita na mkazo kamili utakuwa juu ya mipango yenye faida. Mazao mengi ya dunia hayatatumiwa vibaya. Kwa habari ya mtu mmoja mmoja, ataweza kusitawisha karama na uweza wake na kusaidia bure hali njema ya wengine. Amani ya kweli ya ulimwengu inaweza kuletwa na kuendelezwa tu kupitia kwa amani iliyofanywa pamoja na Mungu. Hali hiyo ya upatano kati ya Mungu na wanadamu inasimuliwa kwa maneno haya ya Zaburi ya 85: “Fadhili na kweli zimekutana, haki na amani zimebusiana. Kweli imechipuka katika nchi, haki imechungulia kutoka mbinguni. Naam, [Yehova] atatoa kilicho chema, na nchi yetu itatoa mazao yake.”​—Zab. 85:10-12.

Ikiwa wewe ni mpenda amani, unaweza kufurahia amani pamoja na Mungu na pamoja na Wakristo wenzako sasa, na kadiri fulani ya amani pamoja na wengine, kama kionjo cha kimbele cha amani kamili itakayofurahiwa karibuni katika taratibu mpya ya Mungu. Amani pamoja na Mungu ndilo jambo la kwanza la lazima, kisha, kuwa na amani pamoja na wengine wa imani ile ile na pamoja na watu wote kwa kadiri inavyokutegemea wewe. Mungu anahakikisha amani kamilifu, yenye kudumu kwa wakati wake. Itakuja upesi baada tu ya yeye ‘kuharibu wale waiharibuo dunia.’​—Ufu. 11:18.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Neno la Mungu linaionyesha njia ya kuwa na amani pamoja naye

[Picha katika ukurasa wa 9]

Twaweza kuzishiriki “habari njema” za amani pamoja na jirani yetu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki