Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w78 10/1 kur. 3-4
  • Jina la Mungu Limo Ndani ya Biblia Yako? Linapaswa Kuwamo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Limo Ndani ya Biblia Yako? Linapaswa Kuwamo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu na Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
w78 10/1 kur. 3-4

Jina la Mungu Limo Ndani ya Biblia Yako? Linapaswa Kuwamo?

JUMAPILI asubuhi Mei 8, 1977, mhudumu Jack Siebert, alikuwa na kazi nyingi akizungumza juu ya Biblia na vikundi vya jamaa katika nyumba yenye vyumba vingi katika Mji wa New York.

Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka kati ya 21 na 25 alipendezwa kusikia ujumbe wa Biblia akasema kwamba angependa kujipatia Biblia. Bw. Siebert alimtolea nakala moja. “Je! hii ni Biblia kweli kweli?” akauliza. Alipohakikishiwa kwamba ilikuwa Biblia kamili katika lugha ya kisasa, aliipokea kwa furaha akailipia.

Baadaye mhudumu huyo alirudi akiwa na rafiki yake. Mwanamke yule akawakaribisha, lakini akasema: “Juma lililopita ulinidanganya. Hii si Biblia ya kweli!” Alimaanisha nini?

Aliendelea kusema: “Katika Biblia hii jina Yehova linaonekana mara nyingi. Ilinikasirisha sana, nilipokuwa nikiisoma, hata nikafuta jina hilo katika kila mahali nilipoliona!”

Je! unafikiri kwamba mwanamke huyu mwenye moyo mnyofu alikuwa na sababu ya kukasirika? Je! ni kweli kwamba “Yehova” si jina la Mungu na halipaswi kuwa katika Biblia? Je! limo ndani ya Biblia unayoitumia? Je! linapaswa kuwamo? Je! wewe unatumia jina la pekee kwa kumtaja Mungu?

Kuhusiana na kisa hiki, mhudumu huyu alitoa habari juu ya jina la Mungu zilizomshangaza mwanamke huyo. Kwa kweli, hata alifadhaika, akasema: “Kwa sababu gani sikujifunza hayo katika kanisa langu? Kwa sababu gani hawakunifundisha mambo hayo?”

Kwa kweli, ye yote anayesoma Biblia anapaswa kujua mambo yaliyoonyeshwa na Bw. Siebert. Na ndivyo ilivyo kwa mtu ye yote anayetumia Sala ya Kielelezo, akisema: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe.”​—Mt. 6:9, Union Version.

Kwa kweli jina hilo ni gani? Je! jibu lako ni “Bwana,” “Mungu,” “Yehova,” “Yahweh,” au jinginelo? Katika Biblia ya Union Version, “Yehova” linaonekana mara kumia tu, wakati tafsiri nyingine zinapotumia “Yahweh” au “Yehova” mara elfu nyingi. Ni gani linalofaa? Nazo tafsiri chache zinalo hilo jina la Mungu katika kinachoitwa “Agano Jipya.” Je! Biblia yako inalo? Je! inapaswa kuwa nalo?

Katika nyakati za karibuni, habari mpya yenye kusisimua juu ya jina la Mungu imepatikana! Utaiona katika makala zinazofuata. Ziangalie, kwa kuwa wewe mwenyewe unahusika (unapaswa). Namna gani hivyo?

Biblia inazungumza juu ya Mungu akiwaangalia kwa njia ya pekee wale wanaomheshimu na kuzungumza habari zake. Kisha inaongeza hivi: “Kumbukumbu ikaandikwa mbele zake la wale wanaomwogopa yeye walioendelea kukumbuka jina lake.” (Mal. 3:16, New English Bible) Je! ndivyo ilivyo kwako? Je! Mungu ameweka kumbukumbu lako wewe, kwa sababu unamwogopa yeye na kulikumbuka jina lake na kulitumia? Habari inayofuata itakuwa juu ya jina lake na lako.

[Maelezo ya Chini]

a Kutoka 6:2-9: Zaburi 83:18; Isaya 12:2; 26:4; Yeremia 16:21; Habakuki 3:19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki