Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 5/1 kur. 9-14
  • Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jambo Unalotenda kwa Kusikia Jina Hilo
  • Matendo Yake ya Upendo
  • Yesu na Jina la Baba Yake
  • Kazi Nzuri Ajabu
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Mungu Anaitwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Je! Jina Lenyewe Linapasa Kutumiwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 5/1 kur. 9-14

Jina Lililo Kuu Kupita Majina Yote

“Lazima wewe uwaambie Waisraeli jambo hili, kwamba ni Yehova yule Mungu wa babu zao, yule Mungu wa Abrahamu, yule Mungu wa Isaka, yule Mungu wa Yakobo, ambaye amekutuma wewe kwao. Hilo ndilo jina langu milele; huo ndio mtajo wa cheo changu katika kila kizazi”—KUTOKA 3:15, The New English Bible.

1. Jina lina ubora gani, kwa kulinganishwa na maneno mengine yanayoweza kutumiwa kutambulisha mtu?

KILA mmoja wetu ana jina. Jina letu linatambulisha kila mmoja wetu kuwa ni mtu. Unaposikia jina la mtu fulani anayekuchukiza sana unakuwa na maoni mabaya, lakini kutajwa kwa jina la mtu unayependa sana kunakutia upesi mawazo yenye kupendeza na ya kufurahisha. Zaidi ya jina lako, kuna maneno mengine yanayoeleza pande moja moja zilizo waziwazi za maisha yako. Mtu yule yule mmoja huenda akaitwa Profesa, Bwana-Mkubwa, Baba au Babu, ikitegemea hali zinazohusika. Kila moja la maneno hayo linaweza kutokeza mawazo tofauti-tofauti juu ya mtu huyo, kuelekeza fikira kwenye upande tofauti wa maisha yake. Lakini jina lake linatukumbusha sisi juu ya utu wake wote—pande zote za maisha yake, kila jambo tunalojua juu yake.

2, 3. Ni kwa njia gani maneno tunayotumia kutambulisha Mungu yangeweza kuleta tofauti juu ya fikira tulizo nazo juu yake?

2 Je! kanuni iyo hiyo inahusika katika fikira zetu juu ya Mungu? Je! mtajo unaotumia kumwita unaleta tofauti fulani juu ya maoni uliyo nayo kuhusu Muumba?

3 Maneno “Muumba” na “Mwenye Nguvu Zote” yanaelekeza fikira kwenye pande fulani za utendaji wake. “Bwana” linaelekeza fikira kwenye mamlaka yake. “Mungu” linaeleza kwamba ana sifa na uwezo unaozidi ule wa kibinadamu. Huenda mtu mwenye kusoma tafsiri za Kifaransa zilizofanywa na Segond na Darby, akiona jina la Mungu limebadilishwa likawa l’Éternel (yule Wa Milele) huenda akapata maoni juu ya Mungu yaliyo tofauti kidogo na yale ya mwenye kusoma Biblia za Kiingereza ambazo watafsiri wazo wamebadili jina la Mungu likawa “Bwana.” Hivyo, mwandikaji mmoja wa kidini alisema hivi: “Kama jina la Mungu binafsi lingeingizwa ndani ya ibada ya Kikristo na uanachuo wa kidini matokeo yangeweza kuwa ya kushangaza na ya kutokeza ujuzi mpya.”

4. (a) Ni nini linaloweza kusemwa juu ya maneno mbalimbali tunayotumia kumtaja Mungu? (b) Ni kwa kadiri gani jina lake linatumiwa katika Maandiko?

4 Yale maneno mbalimbali yanayoeleza Mungu alivyo—Bwana, Mwenye Nguvu Zote, Muumba—ni sahihi. Yanatumiwa katika Biblia. Lakini, kuna neno ambalo Biblia inatumia mara nyingi kuliko lo lote la hayo. Hilo ni JINA la kibinafsi la Mungu, na jina hilo linapasa kutukumbusha juu ya mambo yote tunayojua juu yake. Jina hilo, ambalo kwa wingi linatamkwa leo kuwa Yehova, au Yahweh, linaonekana katika maandishi ya kwanza kabisa ya Biblia mara nyingi sana kuliko neno jinginelo lote la kumtaja Mungu. Kile kichapo kinachoitwa Comprehensive Concordance of the New World Translation of the Holy Scriptures kimetumia nafasi ya safu 43 ili kuweza kuonyesha kila mara ambayo neno “Mungu” au “-a Mungu” limetumiwa katika Biblia, lakini ni safu 77 ambazo kimetumia kuonyesha kila mara ambayo neno “Yehova” au “-a Yehova” linaonekana.

5. (a) Andiko la Kutoka 3:15 (NW ) linatuambia nini juu ya jina la Mungu? (b) Ni nini linaloweza kusemwa juu ya tamko la jina “Yehova”?

5 Jina hilo halikuchaguliwa na wanadamu. Biblia inasema kwamba Mungu ndiye aliyelichagua, na kwamba ndiye aliyesema linapasa kutumiwa. Yeye alisema: “Lazima wewe uwaambie Waisraeli jambo hili, kwamba ni YEHOVA yule Mungu wa babu zao, yule Mungu wa Abrahamu, yule Mungu wa Isaka, yule Mungu wa Yakobo, ambaye amekutuma wewe kwao. Hilo ndilo jina langu milele; huo ndio mtajo wa cheo changu katika kila kizazi.” (Kutoka 3:15, NE) Kwa sababu gani tafsiri hiyo ya kisasa inayokubaliwa mahali pengi sana inatumia jina Yehova katika andiko hilo? Kwa sababu hilo ndilo tamko lililo desturi ya Kiingereza la jina la Mungu ambalo linaonekana mara elfu nyingi katika Biblia ya Kiebrania ya kwanza kabisa.

6. Ni faida gani nyingine ya kutumia jina la Mungu?

6 Wakati Biblia inapotumia jina la kutaja Mungu, jina hilo linatusaidia tumfikirie yeye kuwa mtu mwenye utu, wala si kama nguvu fulani tu. Linatusaidia tumkaribie zaidi. Kwa watu wengi Mungu anaelekea kuwa ni kama yuko mbali. Hata hivyo mtume Paulo aliandika hivi: “Hawi mbali na kila mmoja wetu.”—Matendo 17:27.

Jambo Unalotenda kwa Kusikia Jina Hilo

7, 8. Wewe unatendaje unaposikia jina Yehova likitajwa? Kwa sababu gani?

7 Wewe unatenda namna gani unaposikia jina hilo ambalo Biblia inatumia kumtaja Mungu? Je! jina hilo linakufanya upesi uwe na mawazo yasiyofaa au unakuwa na mawazo ya kupendeza, ya kufurahisha? Je! wewe umefundishwa kuwa na maoni yasiyofaa juu ya jina ambalo kwalo Mungu alisema anapaswa kujulikana, au jina hilo linakutia hisi ya kujisikia ukiwa na uthamini wa moyoni, kama vile Biblia inavyoonyesha ndivyo unavyopaswa kujisikia?

8 Tunaposikia jina Yehova likitajwa tunapaswa kumfikiria Muumba wa mbingu na dunia. Katika Kiebrania cha kwanza kabisa, Biblia inasema: “Yehova Mungu [Yehova Elohim] alifanya dunia na mbingu.” Pia inasema hivi: “Na Yehova Mungu akaanza kufanya umbo la yule mtu mume kwa mavumbi ya kutoka kwenye ardhi na kupuliza ndani ya mianzi ya pua ya huyo mtu mume ile pumzi ya uhai, na yule mtu mume akaja kuwa nafsi inayoishi.” (Mwanzo 2:4, 7, NW ) Hivyo, sisi tuna deni la uhai kwake Yeye. Utendaji wake wa kuumba ulifanya kuwako kwako mwenyewe kuwezekane. Je! uhakika huo unaleta badiliko katika namna unavyotenda unaposikia jina la Mungu likitajwa?

9. Jina hilo linapasa kutukumbusha juu ya jambo gani jingine?

9 Zaidi ya kuwa ndiye Muumba, yeye ndiye Mkusudiaji. Inaaminiwa kwamba jina Yehova linamaanisha “Yeye anafanya iwe.” Yeye anajifanya awe jambo lo lote linalotakwa ili makusudi na ahadi zake zitimizwe bila kushindwa.

10. Ni nini maana ya Kutoka 6:3?

10 Yehova alimwambia Musa hivi: “Nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.” (Kutoka 6:3) Je! maana yake ni kwamba Abrahamu (Ibrahimu), Isaka na Yakobo hawakusikia kamwe jina hilo? Hapana, haingeweza kumaanisha hivyo, kwa maana kabla ya hapo Yehova alikuwa amemwambia Musa kwamba yeye ndiye Mungu wa wanaume watatu hao. (Kutoka 3:15) Tena, kama inavyoonyeshwa na makala iliyotangulia ambayo inasema “Je Jina Lenyewe Linapasa Kutumiwa? ” (ukurasa wa 4), watumishi hao waaminifu waliendelea kulitumia jina hilo. Lakini sasa jina hilo lilikaribia kufunuliwa kwa njia mpya. Jambo ambalo hawakuwa wamejua ni ile maana iliyoongezwa ambayo jina hilo lingekuwa nayo baada ya watu kuona kadiri ambayo Yehova angefikia kuhakikisha kwamba ahadi na makusudi yake yametimizwa.

11. Sasa Waisraeli walikaribiaje kujua Yehova katika njia yenye maana zaidi ya vile babu zao walivyokuwa wamemjua?

11 Makusudi gani? Watu walikuwa karibu kushuhudia yale Mapigo Kumi ya kuogopesha sana. Walikuwa karibu kupitishwa katika Bahari Nyekundu bila kukanyaga maji. Wangepewa ile Sheria wakiwa chini ya hali za kuwatia woga mwingi kwenye Mlima Sinai. Wangelindwa walipitie “jangwa lile kubwa la kutisha” na kuingizwa ndani ya Nchi ya Ahadi.—Kumbukumbu la Torati 1:19; Kutoka 6:7, 8; 14:21-25; 19:16-19.

Matendo Yake ya Upendo

12, 13. Ni nini mengine ya mambo ambayo Biblia inatuambia juu ya matendo ya upendo ya Yehova?

12 Masimulizi yote ya Biblia yanaeleza namna Muumba alivyo. Yanasimulia uaminifu wake, unyofu na haki yake. Biblia inasema: “Yehova ni mwema na mnyofu.” Inasema: “Maana wema wake, jinsi ulivyo mwingi! ” “Yeye Mwamba, kazi yake ni kamilifu; maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili.”—Zaburi 25:8, NW; Zekaria 9:17; Kumbukumbu la Torati 32:4, UV.

13 Biblia inamwonyesha Yehova kuwa Mfalme (Zaburi 10:16; Danieli 4:34), Mwamuzi (Zaburi 50:6; 98:9), Baba (Isaya 64:8; Mathayo 6:6-9), Mume mwenye mke (Isaya 54:5; Yeremia 3:14), Mwalimu (Zaburi 71:17; Isaya 50:4; 54:13) na Msaidiaji (Zaburi 30:2; 115:9-13; 121:2). Jina lake linapasa kutukumbusha juu ya matendo yake ya upendo, juu ya uhakika wa kwamba yeye ana kanuni zinazofaa zilizowekwa imara na kwamba ana haki ya kutaka utii na kujitoa kwa watoto wake wa kidunia. Maandiko yanasema hivi: “Yehova anajulikana kwa hukumu ambayo amefikiliza.” “[Yehova] huwahifadhi wote wampendao, na wote wasio haki atawaangamiza.”—Zaburi 9:16, NW; 145:20 UV.

14. (a) Waandikaji na waimbaji wa Zaburi walionyeshaje walikuwa na tumaini hakika katika Yehova? (b) Mithali zinaonyesha nini juu yake?

14 Jina hilo linaonekana mara 749 katika kitabu kamili cha Biblia cha Zaburi. Zaburi au nyimbo hizo za sifa, ziliimbwa na waabudu wenye kujawa na furaha ambao walitoa “shukrani kwa jina la Yehova” kwenye hekalu katika Yerusalemu. (Zaburi 122:1-4, NW ) Waandikaji na waimbaji wa zaburi hizo walijua jina la Yehova (Zaburi 9:10), walilitumaini jina lake (33:21), waliita jina lake (80:18; 105:1), walitolea jina lake takatifu shukrani (106:47), walitafuta msaada kwa jina lake (124:8) na waliendelea kulisifu jina lake (68:4; 135:3). Jina lake halikuwa jina la kufichwa bali lenye kupendwa. (Zaburi 89:1; 92:1-5) Si kwamba tu Yehova ndiye aliyeyatenda matendo ya upendo yanayosifiwa katika zile Zaburi bali pia yeye ndiye aliyetia roho yake katika hekima iliyoandikwa katika kitabu cha Biblia cha Mithali. Kinasema hivi: “kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima; kutoka kinywa chake kuna maarifa na ufahamu.” (Mithali 2:6, NW ) Ikiwa tafsiri yako ya Biblia inatumia neno “Bwana” katika vifungu hivyo, uwe na uhakika wa kwamba katika Kiebrania cha kwanza kabisa jina la Mungu linaonekana katika kila kimoja cha vifungu hivyo.

15. (a) Jina la Yehova linapasa kutukumbusha juu ya matukio gani ya kutazamisha? (b) Kulingana na Danieli 2:20, 21 na 4:17, ni nini kinachotutolea msingi wa kubariki (kuhimidi) jina la Yehova?

15 Jina lenyewe linapasa kutukumbusha juu ya jumla yote ya historia, unabii, sheria na hekima ambayo imepangwa katika Biblia. Linapasa kutukumbusha juu ya unabii mbalimbali wa kushangaza sana ulioshughulika na vile hasa sehemu kubwa ya historia ya ulimwengu ingetukia. Yehova alifanya matukio ya historia ya kweli yatukie kwa njia ambayo unabii wake mbalimbali ungetimizwa juu ya Misri, Ashuru, Babuloni, mwungano wa Umedi na Uajemi, Ugiriki na Roma, na kuendelea hivyo kuipitia karne yetu ya 20 yenye msukosuko mpaka huko mbele—Danieli, sura 2, 7, 8.a

Yesu na Jina la Baba Yake

16. (a) Kukaa kwa Yesu duniani kunapasa kuwe na matokeo gani juu ya uthamini wetu wa Baba yake, Yehova Mungu? (b) Ni kwa njia gani hasa Yesu alijulisha jina la Baba yake?

16 Uthamini wenye uchangamfu ambao jina la kimungu Yehova linapasa kuletea mioyo yetu unapasa kutia ndani jambo lililo la maana hata zaidi—kwamba kwa mwujiza alipeleka duniani “mzaliwa wa kwanza” wake, yule “Neno,” ambaye akawa Yesu Kristo. (Waebrania 1:6; Yohana 1:1-3; Warumi 5:6-8) Katika sala aliyopelekea Baba yake wa kimbingu, Yesu alisema: “Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu . . . Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo.” (Yohana 17:6, 26) Si kwamba wafuasi wake hawakuwa tayari wamejua jina la Mungu. Kama ilivyoonyeshwa katika ile makala inayosema “Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kikristo” (ukurasa wa 8), wao waliliona jina hilo katika vitabu vyao vya kukunjwa vya Biblia katika lugha ya Kiebrania na pia katika tafsiri ya Biblia ya Kigiriki waliyoitumia. Lakini kwa sababu ya kuhubiri kwa Yesu, jina hilo lilipata maana zaidi—sawasawa na vile lilivyokuwa limepata kwa sababu ya matendo aliyoyafanya Yehova huko nyuma katika siku za Musa. Yesu alipanua kwa njia nzuri ajabu maarifa yetu ya kumjua Yehova na kumthamini, juu ya utu wake na makusudi yake. Sisi tunajua jina la Yehova kwa njia kubwa zaidi sana kupitia Yesu, ambaye alisema: “Mafunzo yangu si yangu mimi, ila ni yake yeye aliyenipeleka.” Yesu aliutoa ukombozi na akaweka njia ya kumfikia Baba. Hivyo Yesu alisema hivi: “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”—Yohana 7:16; 14:6.

17. Ni matumizi gani ya kimbingu juu ya jina la Mungu yaliyotabiriwa katika kitabu cha Ufunuo?

17 Katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo, ambacho kimeweka maandishi ya njozi ya Yohana ya matukio yanayotendeka siku zetu, bado jina la Yehova linaendelea kusifiwa. Wakati Babuloni Mkuu, ile milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, inapoharibiwa, kundi kubwa katika mbingu linatamka shangwe kubwa hii: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uwezo ni vya Mungu wetu.” Halafu “wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wanaoishi wakaanguka chini na kuabudu Mungu ambaye ameketi juu ya kile kiti cha ufalme, wakisema, ‘Amina. Haleluya! ’ ” (Ufunuo 19:1, 4, Revised Standard Version) “Haleluya” maana yake nini? Huko nyuma katika ukurasa wa 4 tumekwisha kuona kwamba neno “Yah” ni namna fupi zaidi ya kishairi inayosimamia “Yehova.” Hivyo, Kamusi inayoitwa The Random Dictionary of the English Language inasema kwamba neno “Haleluya” limetokana na neno la Kiebrania la kusema “Sifu(ni) Yehova.” Kwa hiyo Mungu anaabudiwa mbinguni kwa mlio wa shangwe unaosema: “Sifuni Yehova! ”

Kazi Nzuri Ajabu

18. Kujua mambo ambayo Yehova amefanya “kwa ajili ya jina lake” kunatusaidia tuthamini nini?

18 Jina la Mungu linapasa kutumiwa. Linapasa kutukumbusha juu ya kazi zake na fadhili za upendo wake. Biblia inatuambia kwamba yeye alifanya vitu hivyo vya ajabu “kwa ajili ya jina lake, ayadhihirishe matendo yake makuu.” (Zaburi 106:8) Kazi nzuri ajabu alizofanya “kwa ajili ya jina lake” hazikufanywa kwa majisifu bali kutusaidia tuthamini kwamba yeye ni Mungu, kwamba ana haki ya kutuambia mambo tunayopaswa kufanya, na kwamba tunaweza kuwa na tumaini hakika kabisa kwamba ahadi zake zitatimizwa. (1 Samweli 12:22) Hivyo yeye alisema: “Kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote. . . .Naam, nimenena, nami nitatekeleza; nimekusudia, nami nitafanya.”—Isaya 46:9-11.

19. Ni maneno gani yenye kutia uhakikisho ambayo Yoshua alisema juu ya kutegemeka kwa Neno la Mungu?

19 Karne nyingi kabla ya hapo, Yoshua alikuwa amewakumbusha Waisraeli hivi: “Nyote mnajua mioyoni mwenu, na [nafsini] mwenu, ya kuwa halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena [Yehova], Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu, hapana neno lo lote mlilopungukiwa.”—Yoshua 23:14.

20. Ni nini mengine kati ya mambo ambayo jina Yehova linakukumbusha wewe?

20 Je! maoni ambayo wewe unayo juu ya Yehova ni kutia ndani pamoja na mambo yote hayo? Je! unaposikia jina lake likitajwa unakumbuka juu ya kazi zake, uwezo wake, wenyeji wake wa nguvu zote, ustahili wake wa kutumainiwa na ukweli wa ahadi zake? Je! wewe unashirikisha jina lake na Yule Mungu anayejifanya mwenyewe awe jambo lo lote linalotakwa ili makusudi yake yaweze kutimizwa? Je! wewe unalifikiria jambo la kwamba Yehova alipeleka Yesu duniani aondolee jina la Mungu malawama, atufundishe sisi habari za Baba yake na kutoa ukombozi kwa ajili ya wote watakaoukubali? Na je! maoni uliyo nayo moyoni juu ya Yehova ni kutia ndani pamoja na uthamini wako wa ahadi zake za kwamba kutakuwa na wakati ujao wenye uadilifu katika dunia itakayokuwa imesafishwa?—2 Petro 3:13.

21. Nia yetu inaweza kuwa namna gani kama ile ya Mfalme Daudi mwadilifu?

21 Maarifa ya kujua mambo ambayo Yehova amefanya yanazaa imani. Imani inatutia haraka tuchukue hatua. Sisi tunatumia jina lake, tunasema juu ya matendo yake, tunajitoa wenyewe kwa nia ya kupenda tukiwa watumishi wake, na tunatazamia utimizo wa kusudi lake kuu lisiloshindwa la kuiondolea dunia uovu wote na kuanzisha hali mpya za uadilifu kwa ajili ya wanadamu wenye kutii. Tukiwa na imani ya namna hiyo, na kutenda kupatana nayo, tunaweza kusema kama Mfalme Daudi mwadilifu: “Kinywa changu kitazinena sifa za [Yehova]; wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu milele na milele.”—Zaburi 145:21.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate mazungumzo ya mwingi wa unabii huu, ona kitabu “You Will Be Done on Earth,” kilichochapishwa na Sosaiti.

Kwa njia ya kurudia

□ Ubora wa jina ni nini, tofauti na neno la namna nyingineyo ambalo huenda likatambulisha mtu?

□ Jina Yehova linapasa kutukumbusha sisi juu ya nini?

□ Kufundisha kwa Yesu kuliongezaje uthamini wetu wa jina Yehova?

□ Ni kwa njia gani kazi ambazo Yehova alifanya “kwa ajili ya jina lake” ni za faida kubwa kwetu?

[Sanduku katika ukurasa wa 12]

Mtu tusiyemjua jina anaendelea sikuzote kuwa kama mtu tusiyemfahamu vizuri. Wakati Mungu anapotukaribisha tutumie jina lake, hilo ni tendo la urafiki wa kimungu

[Picha katika ukurasa wa 11]

Tendo la Mungu la kuokoa Waisraeli kwa kuwapitisha katika Bahari Nyekundu lilijulishaje jina lake kwao?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki