Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w84 5/1 kur. 7-9
  • Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kikristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kikristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwekwa kwa Maneno Mengine Mahali pa Jina la Mungu
  • Jina la Mungu na “Agano Jipya”
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Jambo Jipya Juu ya Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Magumu ya Kujua Maana ya Jina la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
w84 5/1 kur. 7-9

Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kikristo

WAKATI Yesu alipoita Mungu Baba yake, Wayahudi wenye kumsikia walijua Yule aliyekuwa akimtaja. Wao waliona jina la Mungu katika vitabu vya kukunjwa vya Biblia katika Kiebrania ambavyo vilikuwa katika masinagogi yao. Kitabu kimoja cha kukunjwa cha namna hiyo alipewa Yesu katika sinagogi la mji wa kwao, Nazareti. Yeye alisoma kifungu kutoka Isaya ambacho kilikuwa na jina la Yehova mara mbili.—Luka 4:16-21, NW.

Wanafunzi wa kwanza wa Yesu pia waliona jina la Mungu katika ile Septuagint—tafsiri ya Biblia katika Kigiriki, ambayo Wakristo wa kwanza walitumia katika kufundisha na kuandika. Ni kweli kwamba wakati mmoja ilifikiriwa kwamba jina la Mungu halikuwa katika Septuagint, lakini sasa inajulikana waziwazi kabisa kwamba jina hilo liliheshimiwa sana mpaka ile Tetragramatoni (neno ambalo wanachuo wanatumia kutaja zile herufi nne ambazo kwazo jina la Mungu linaandikwa katika Kiebrania) ikanakiliwa kwa herufi za Kiebrania na kuingizwa ikiwa hivyo moja kwa moja katika maandishi ya Kigiriki.

Akila aliandika jina la Mungu kwa herufi za Kiebrania katika maandishi yake ya Kigiriki baadaye sana kwenye karne ya pili. Katika karne ya tatu Origen aliandika kwamba “katika hati zinazofuatisha maandishi kwa uaminifu zaidi sana JINA LENYEWE limeandikwa kwa herufi za Kiebrania.” Katika karne ya nne Jerome mtafsiri wa Biblia aliandika hivi: “Sisi tunakuta jina la Mungu lenye herufi nne (yaani, יהוה) katika mabuku fulani ya Kigiriki hata mpaka leo hii zikiwa zimeonyeshwa kwa zile herufi za kikale.”

Dakt. Paul E. Kahle anaandika hivi: “Sasa sisi tunajua kwamba maandishi ya Kigiriki ya Biblia [ile Septuagint] kwa kadiri yalivyoandikwa na Wayahudi kwa ajili ya Wayahudi hayakutafsiri jina la Kimungu kwa kutumia ky’rios [Bwana], bali ile Tetragramatoni iliyoandikwa kwa herufi za Kiebrania au Kigiriki ilidumishwa katika hati hizo.”—The Cairo Geniza, kurasa 222, 224.

Hiyo inamaanisha nini? Inamaanisha kwamba, hata kama walikuwa wasemaji wa Kiebrania au Kigiriki, wakati wenye kumsikia Yesu walipoyasoma Maandiko waliona jina la Mungu katika maandiko hayo. Hivyo, ni jambo linalopatana kabisa na kufikiri kuzuri kwamba wakati walipotumia maneno ya maandishi hayo walikuwa wakifuata desturi waliyokuwa wameshika—kuingiza zile herufi nne za Kiebrania za jina la Yehova katika maandishi yao ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

Katika jarida linaloitwa Journal of Biblical Literature, George Howard, profesa mshirika wa dini kwenye Chuo Kikuu cha Georgia, aliandika hivi: “Kwa kuwa bado Tetragramu iliandikwa katika nakala za Biblia ya Kigiriki ambayo ndiyo iliyokuwa Maandiko ya kanisa la kwanza, ni jambo la akili nzuri kuamini kwamba waandikaji wa A[gano] J[ipya] walihifadhi Tetragramu ndani ya maandishi ya kibiblia wakati wa kutumia maneno yaliyotokana na Maandiko.”—la 1977, Buku la 96, Na. 1, ukurasa wa 77.

Kuwekwa kwa Maneno Mengine Mahali pa Jina la Mungu

Inaelekea kuwa jina la kimungu liliondolewa baadaye katika Septuagint na pia katika “Agano Jipya” wakati Wakristo wasio Wayahudi walipokuwa hawazielewi tena zile herufi za Kiebrania. Hivyo Dakt. Kahle anaandika hivi: “Wakristo ndio walioweka neno kyʹrios [Bwana] mahali pa ile Tetragramatoni, wakati jina la kimungu lililoandikwa kwa herufi za Kiebrania lilipokuwa halieleweki tena.”—The Cairo Geniza, ukurasa wa 224.

Ukosefu huo ulikuwa mkubwa kadiri gani? Profesa Howard anasema hivi: “Kwa maoni yetu, kuondolewa hivyo kwa ile Tetragramu kulitokeza mvurugo katika akili za Wakristo wa kwanza wa Mataifa yasiyo ya Kiyahudi juu ya uhusiano ulio kati ya yule ‘Bwana Mungu’ na yule ‘Bwana Kristo.’ “—Ukurasa wa 63 wa makala iliyotangulia kutajwa.

Kwa mfano, Zaburi 110:1 (NW ) inasema hivi: “usemi wa Yehova kwa Bwana wangu ni.” Maneno hayo yametumiwa katika Mathayo 22:44 ambapo, baada ya jina Yehova kuondolewa, tafsiri zilizo nyingi za kisasa zinasema hivi: “Bwana alimwambia Bwana wangu.” Hivyo, kwa washiriki wa makanisa ya Jumuiya ya Wakristo ile tofauti iliyo wazi kati ya Yehova (“Bwana”) na Yesu (“Bwana wangu”) ilipotea.

Kuna faida kubwa katika kuufuata mfano wa Kibiblia wa kutumia jina la Mungu: (1) Kunatusaidia tuwe na maoni ya kwamba Mungu ni Mtu, si nguvu tu. (2) Kunatusaidia tumkaribie zaidi. (3) Kunaondoa kabisa mvurugo, kufanya fikira zetu ziwe sahihi zaidi juu yake, kufanya mawazo yetu yafuatane kwa usahihi zaidi na yale ambayo kwa kweli Biblia inayafundisha.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Jina la Kimungu lilikuwa katika tafsiri za kwanza za Kigiriki za Maandiko ya Kiebrania likiwa katika herufi za Kiebrania

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki