Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 3/15 uku. 24
  • Barua ya Shukrani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua ya Shukrani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 3/15 uku. 24

Barua ya Shukrani

“Kwa miaka mitano mke na mwana wangu walikuwa Mashahidi wa Yehova bila ya mimi kuwapa ruhusa kamili. Nafahamu sasa kwamba niliwapa shida na mzigo mkubwa sana kupitia kwa vitendo vyangu na kwa kushindwa kumwamini Yehova. Mungu peke yake ndiye ajuaye yaliyowapata katika wakati huo. Nami natumaini kwamba yeye ni Mungu mwenye kusamehe sana, sana.

“Ijapokuwa nilikuwa Mkatoliki asiyetenda, nikifanya dhambi kila siku ya maisha yangu, bado nilijiona kuwa bora kuliko Mashahidi wa Yehova, niliokuwa nikiwaona kuwa washikilia dini sana. Nilishindwa kufahamu kwamba Yesu Kristo vilevile aliitwa mshikilia dini sana katika wakati wake. Sana sana jina Yehova lilinichukiza sana.

“Walakini baada ya magumu mengi nilipokuwa nikihamia California kutoka Missouri, niliona kwamba kitu fulani kilikosekana maishani mwangu. Ilikuwa kama kwamba nilikuwa nimepotea katika ulimwengu huu uliovurugika, nami sikujua namna ya kuanza maisha yangu tena katika njia inayofaa. Kwa hiyo, nilianza kumwomba Mungu Mwenye Nguvu Zote aniongoze, na kunionyesha njia ya kuondolea utupu niliokuwa nao ndani yangu. Mara hiyo, mlango wa chumba changu ukagongwa. Nilipoufungua, nilimwona mwanamke, Shahidi wa Yehova.

“Kwa kawaida ningaligeuka, na kufunga mlango kwa upole, walakini wakati huu, kwa kuwa nilikuwa nimemaliza tu kuomba uongozi, nilijisikia tofauti ndani yangu. Tulizungumza kwa muda wa dakika kama 40 hivi, kisha akanikaribisha nihudhurie mikutano katika jumba. Hata alichukua wakati akachora ramani ya kuniongoza namna ya kufika huko. Nilikuwa sijapata kuona Mkatoliki ambaye angechukua wakati kama huo na kuhangaikia faida za kiroho za mwanadamu mwenzake. Nilijisikia vingine ndani yangu kwa sababu mtu huyu alikuwa akihangaikia sana wokovu wangu.

“Kwa hiyo sasa ninahudhuria Jumba la Ufalme pamoja na mke wangu Christine na mwana [wangu] Philip. Pia najifunza Biblia kwa ukawaida. Natumaini kwamba sikumwona Yehova nikiwa nimechelewa mno nisiweze kuupata uzima wa milele.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki