Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w79 9/1 uku. 16
  • Je! Wewe Waweza Kufaidika Kutokana na Imani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Waweza Kufaidika Kutokana na Imani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Inafaa Kuwachukia Watu wa Jamii Nyingine?
    Amkeni!—2003
  • Namna Imani Ishindayo Inavyoweza Kukuhusu Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Ni Nini Suluhisho la Chuki ya Kijamii?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
w79 9/1 uku. 16

Je! Wewe Waweza Kufaidika Kutokana na Imani?

KATIKA miaka ya karibuni duniani pote kumekuwako kile kinachoitwa na watu wengi kuhuishwa kwa dini. Kwa sababu gani jambo hilo limetokea?

Akitoa jibu lake, Martin E. Marty Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Chicago cha Masomo ya Elimu ya mambo ya Dini alisema hivi: ‘Kwanza, hakuna jambo jingine linaleta matokeo​—⁠hii ni njia ya wazi ya kusema kwamba karibuni tu kama miaka 15 iliyopita watu waliweka imani nyingi katika uwezo wa kibinadamu, katika kutumia elimu ya ufundi na siasa. Nami nafikiri kwamba tulipata faida kubwa katika nchi yetu [United States]​—⁠ katika haki za raia, haki za kibinadamu, katika uhusiano wa watu, na katika sehemu fulani za utunzaji wa afya na mpango wa usalama.’

‘Walakini,’ akaendelea Mwalimu Marty, ‘vilevile tulipata kujua kikomo cha jitihada za kibinadamu. Tulipata kuona kwamba mambo hayo tuliyotimiza hayakuyapa maisha maana. Hayakuwa yakitupa kanuni bora ambazo zingetumiwa na kizazi kipya. Na wakati wo wote katika historia ambapo watu wanatambua kikomo cha uwezo wao, watu huelekeza jitihada zao katika pande mbili​—⁠mmoja, ndani ndani sana yao wenyewe ili wapate maono ya ndani, na wa pili, ulio bora kuliko wao, wenye nguvu zipitazo za kibinadamu. . . . Watu hutafuta sababu. Watu wanatafuta kukubaliwa. Na kuna sababu za muhimu za hilo sana katika miaka hii ya kuanzia na mwaka wa 1970, nami nafikiri ndiyo sababu kuna kuhuishwa huku kwa dini.’

Hata hivyo, je! kuhuishwa huku kwa ki-siku-hizi kwa dini kumeondoa vizuizi vya kikabila ambavyo vinatenganisha jamii ya kibinadamu? Je! dini kwa ujumla imepata kubadilisha kweli kweli maisha na kutoa ‘kanuni ambazo zingetumiwa na kizazi kipya’? Je! imewapa watu tumaini hakika la wakati ujao?

Watazamaji wenye ufahamu wajua kwamba, kujapokuwako kuhuishwa huku kwa dini ulimwenguni pote, vizuizi vya kikabila vingali vinatenganisha jamii ya kibinadamu. Madai hayo ya imani hayakumaliza magomvi ya ndoa, talaka zenye kuongezeka kwa haraka sana, pamoja na ngono zinazofanywa ovyo-ovyo ambazo huleta mvunjiko wa moyo na kukosa furaha. Zaidi ya hayo, ijapokuwa watu wengi zaidi na zaidi wanaigeukia dini, hakuna ushuhuda mwingi kuonyesha kwamba yale wengi wao wanayopata yanawapa uhodari wa kweli na kuwapa tumaini lenye msingi mzuri la wakati ujao. Kwa mfano, kati ya vijana wenye umri wa miaka 15 mpaka 24 katika United States kujiua kumekua jambo la tatu kati ya yale mambo makuu yanayotokeza kifo, naye Dakt. Calvin J. Frederick wa Chama cha Kitaifa cha Utabibu wa Akili anasema kwamba sababu ya kujiua huko ni “kushuka moyo kunakoletwa na ‘kutofaniki-wa, kukosa msaada na kukosa tumaini.’”​​—⁠Newsweek, Ago. 28, 1978.

Kwa kuwa kuhuishwa huku kwa dini kwa miaka ya karibuni hakukufanyiza jambo la kutokeza juu ya jamii ya kibinadamu mtu anaweza kuuliza kwa kufaa hivi: ‘Mimi naweza kufaidika kutokana na imani? Je! inaweza kuwa na matokeo katika maisha ya mtu?’

Ndiyo, watu fulani wanayo imani yenye msingi wa Maandiko, nayo ina matokeo juu ya maisha yao. Imani hiyo inashinda vizuizi na magumu. Ina uwezo wa kugeuza maisha. Imani ya kweli haikubaii vizuizi vya kikabila. Inatoa uhodari na kutoa tumaini la wakati ujao.

Je! hii ni misemo tu isiyo na msingi? Hata kidogo! Tafadhali fikiria kwa uzito ushuhuda unaotolewa katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki