Ni Nani Waliokuwa Wazao wa Misiraimu?
Mmoja wa wana wa Hamu alikuwa Misiraimu. (Mwa. 10:6, ZSB) Maandiko yanaonyesha pasipo kukosea kwamba yeye ndiye aliyekuwa babu wa Wamisri wa kale. Kwa mfano, wakati Wakanaani walipoyaona maombolezo ya matanga (mazishi) ya Wamisri katika sakafu ya Atadi, walipaita mahali hapo “Abeli-Misuraimu,” maana yake “maombolezo ya Wamisri.”—Mwa. 50:7-10, ZSB.