Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 4/1 kur. 3-4
  • Mungu Atanisahau Muda Hata Wakati Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Atanisahau Muda Hata Wakati Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Kumtegemea Yehova Kikamili Kunatuchochea Kuwa na Uhakika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Uhakika Wakati wa Hatari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Yehova Alikuwa “Mwokoaji” Katika Nyakati za Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • “Unifundishe Kufanya Mapenzi Yako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 4/1 kur. 3-4

Zaburi

Mungu Atanisahau Muda Hata Wakati Gani?

ULIPOKUWA unavumilia magumu na matatizo makubwa, je! ulipata kuona kwamba Mungu alikuwa amekusahau? Je! ulipata kuona kwamba huenda akawa hapendezwi nawe na, hivyo, hakuwa akikupa msaada wa kutatua matatizo yenye kukaza?

Hivyo ndivyo Daudi alivyoona, pengine alipokuwa akipata mateso kutoka kwa Mfalme Sauli, au baadaye, wakati wa uasi wa mwanawe Absalomu. Walakini hata kiwe kilikuwa kipindi gani, Daudi alipatwa na majaribu kwa muda mrefu sana hata kwamba akajikuta yu katika hali ya chini sana, akiwa anajiuliza kama Yehova alikuwa amemsahau. Alisukumwa atamke hivi: “Hata lini, Ee Yehova, utanisahau? Milele? Utanificha uso wako hata lini?” (Zab. 13:1, NW) Ilionekana kwa Daudi kama kwamba Yehova alikuwa ameficha uso wake kwa kutopendezwa, asimsaidie. Kwa hiyo anaendelea kuuliza hivi: “Nitaendelea kuzuia nafsi yangu kwa muda mrefu kadiri gani, huzuni moyoni mwangu wakati wa mchana?” Hiyo yaweza kumaanisha kwamba alitaka kujua angeachwa kwa muda mrefu kadiri gani ajifanyie njia zake za kuzuia hali zenye kutaabisha ambazo alijikuta ndani yake nao ni muda mrefu kadiri gani huzuni yake ingeendelea kuwapo siku baada ya siku.

Kisha, mtunga zaburi huyo anatokeza ulizo hili: “Adui yangu atainuliwa juu yangu kwa muda mrefu kadiri gani?” Ikionekana kama kwamba ameachwa na Yehova, anataka kujua adui zake wangeendelea kuongoza mambo kwa muda mrefu kadiri gani. Anafuatisha ulizo hilo kwa ombi hili: “Unitazame; nijibu, Ee Yehova Mungu wangu. Yafanye macho yangu yaangaze, ili nisilale katika mauti, ili adui yangu asiseme: ‘Nimemshinda!’ ili kwamba adui zangu wenyewe wasifurahi kwa sababu ninafanywa nitikisike.” (Zab. 13:2-4, NW) Ndiyo, Daudi alitaka sana Aliye Juu Zaidi ajibu kusihi kwake, amsaidie na kumchangamsha ili macho yake “yaangaze.” Alitamani kuendelea kuwa hai ili kwamba adui zake wasikate shauri kwamba walikuwa wameshinda kweli kweli na kufurahia kwamba alikuwa ametikisika na kuanguka asisimame tena.

Hata ingawa Daudi aliona kana kwamba alikuwa ameachwa na Yehova, imani yake iliendelea kuwa na nguvu. Hilo linaonekana wazi kutokana na maneno yake ya kumalizia: “Mimi, katika fadhili zako za upendo nimetumaini; acha moyo wangu ufurahie wokovu wako. Nitamwimbia Yehova, maana amenitendea kwa njia ya kunithawabisha.” (Zab. 13:5, 6, NW) Yajapokuwa matatizo aliyokuwa anakabili, Daudi alitumaini fadhili za upendo za Yehova au kuhangaikia kwa huruma na, akiwa na tumaini na furaha, alitazamia wokovu kutoka kwa majaribu yake. Alikumbuka namna Yehova alikuwa amemthawabisha katika wakati uliopita naye akaazimia kuendelea kuimba nyimbo za kusifu.

Kama vile Daudi, hatupaswi kusahau kamwe mambo makuu ambayo Yehova Mungu ametufanyia. Katika kuonyesha upendo wake unaozidi, alimtoa Mwanawe mzaliwa-pekee. (Yohana 3:16) Tangu tulipomjua Aliye Juu Zaidi, sisi binafsi tumeona uangalizi wake wa upendo na msaada katika kujibu sala zetu. Kutokana na yale tunayojua juu ya kushughulika kwa Muumba na watumishi wake wakiwa wote na wakiwa mtu mmoja mmoja, twaweza kuwa na hakika kwamba atatutia nguvu wakati tunapokuwa na uhitaji. Tunapokuwa katika kipindi chenye kujaribu sana, twaweza kufarijiwa na maneno haya yaliyoongozwa kwa roho: “Mkimtupia mahangaiko yenu yote, kwa sababu anawajali.”​—1 Pet. 5:7, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki