Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 2/15 uku. 24
  • Uchawi Waachwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uchawi Waachwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 2/15 uku. 24

Uchawi Waachwa

Miaka fulani iliyopita, katika kisiwa cha Ometepe katikati ya Ziwa Nicaragua katika Amerika ya Kati, aliishi msichana mchanga ambaye babaye alikuwa anafanya uchawi na kuponya kwa uchawi. Alikuwa na sifa ya kuponya waliolemaa kwa kuita roho wabaya. Baada ya kifo chake, hata hivyo, bintiye alilemaa na kulazwa kitandani.

Mwanamke huyo alipewa utibabu na mtu ambaye anafanya uchawi, pia. Walakini siku moja mwangalizi Mkristo mwenye kusafiri alitembea kwake nyumbani na kumpa zawadi—nakala ya Biblia ya “New World Translation of the Holy Scriptures.” Kwa kuisoma, mwanamke huyo aliona amri ya Mungu juu ya uchawi, kama ilivyoandikwa katika Kumbukumbu la Torati sura ya 18. Basi akaachana na utibabu aliokuwa akipewa na mchawi.

Shahidi mwingine alifanya ziara ya pili kwa mwanamke huyo na funzo la Biblia la nyumbani likaanzishwa. Mwishowe, aliulizwa kama babaye aliyekufa alikuwa ameacha vitabu au karatasi zo zote zinazohusiana na uchawi wake, naye mwanamke huyo akajibu kwamba vitoto kadha vya meza vilikuwa vimejaa vitu hivyo. Kwa hiyo wakateketeza vitu hivyo. (Matendo 19:18, 19) Vilevile, mwanamke huyo alisihiwa amwombe Yehova msaada. Muda mfupi baadaye, akaanza kutembea tena.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki