‘Wanawake Kumi Wakioka Mkate Katika Tanuu Moja’
MMOJAWAPO wa misiba ambayo ingeipata Israeli kwa sababu ya kutoaminika unaonyeshwa katika Mambo ya Walawi 26:26: “Wanawake kumi wataoka mikate yenu katika tanuu moja.’’ Katika hali za kawaida, kila mwanamke angehitaji tanuu (joko) yake mwenyewe ya kuokea vitu vilivyohitajiwa. Walakini, maneno ya Mambo ya Walawi 26:26 yalielekeza kwenye wakati ambao katika huo chakula kipatikanacho kingekuwa kidogo sana hivi kwamba joko moja lingetosha kutumiwa na wanawake 10 katika kuoka.