Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 4/1 kur. 14-20
  • Iweni na Uhodari! Miaka Elfu Imekaribia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Iweni na Uhodari! Miaka Elfu Imekaribia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MFANO WA DANIELI WA UJASIRI
  • KATIKA SHIMO LA SIMBA
  • KATIKA “WAKATI WA TAABU”
  • “IWENI HODARI NA MOYO WA USHUJAA”
  • Jifunze Kutokana na Mfano wa Danieli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Yehova Huthawabisha Imani na Ushujaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Uwe Hodari Yehova Yupo Pamoja Nawe!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Danieli Katika Shimo la Simba
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 4/1 kur. 14-20

Iweni na Uhodari! Miaka Elfu Imekaribia

“Katika ulimwengu ninyi mnapata dhiki, lakini iweni na ujasiri! Mimi nimeushinda ulimwengu.” —Yohana 16:33, NW.

1. Sababu gani wanafunzi wa Yesu wangehitaji kuwa wajasiri sana?

HAYA yalikuwa maneno ya Yesu ya mwisho ya kuwashauri wanafunzi wake, yaliyonenwa katika usiku wa mwisho wa kukamatwa na kuuawa kwake mwenyewe. Yeye mwenyewe alionyesha sifa hiyo ya ujasiri kwa kadiri kubwa, naye alitaka wafuasi wake waliojitoa kufanya vivyo hivyo. Wangehitaji kuwa wajasiri sana, kwa kuwa Yesu alikuwa ndipo tu amemalizia kuwaambia hivi: “Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi. Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi, watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni. Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia, kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia. Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.”​—Yohane 15:18-21, HNWW.

2. Ni mambo gani yanayotiwa ndani ya ujasiri kama wa Kristo? (Linganisha Zaburi 27:13, 14; 31:24)

2 Walakini, ni jambo gani linalotiwa ndani ya ujasiri kama wa Kristo? Je! maana yake ni ujasiri kama ule unaoonyeshwa na askari katika shimo wanalojichimbia ili wajikinge na risasi zinazofyatuliwa katika vita vikali? Hasha, unamaanisha zaidi ya hilo. Ujasiri wa Kikristo unamaanisha kuonyesha nguvu za adili zilizo mfano mzuri katika nyakati zote. Unatuhitaji tuunge mkono ufalme wa Mungu pasipo kusita-sita chini ya hali yo yote na hali zote. Unatuhitaji tuwe wenye uthabiti, uvumilivu pamoja na ushikamanifu wenye kuendelezwa kwa kanuni za haki. Ujasiri wa kweli unatia ndani kuazimia na kuwa na nia inayofaa ya kusonga mbele na kufaulu, hata kukiwa upinzani na magumu yanayoelekea kutoshindika. Unatia ndani azimio ambalo mtume Paulo alionyesha, akisema hivi: “Jambo moja nafanya: nayasahau yale yaliyopita na kufanya bidii kuyazingatia yale yaliyo mbele. Basi, nimo mbioni kuelekea lengo langu.”​—Fil. 3:13, 14, HNWW.

MFANO WA DANIELI WA UJASIRI

3. Danieli na wenzi wake walionyesha ujasiri gani ulio mfano mzuri kwa habari ya chakula na kinywaji?

3 Neno la Mungu limejaa masimulizi ya ujasiri mwingi mno ulioonyeshwa katika kuelekeana na majaribu yenye kujaribu imani. Mtu mmoja ambaye alionyesha ujasiri wa namna hiyo mara kadha alikuwa nabii wa Mungu Danieli. Akiwa kijana aliyefanywa mtumwa katika Babeli, yeye “aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa,” na katika jambo hili Shadraka, Meshaki na Abednego walijiunga naye. (Dan. 1:8-19) Jambo hili lilihitaji ujasiri, ujasiri kama ule ambao umehitajiwa kwa upande wa mashahidi wa Yehova vijana katika nchi fulani leo, kwa mfano kwa kukataa kula chakula cha shule cha alasiri chenye vitu vilivyotengezwa kutokana na damu.​—Matendo 15:28, 29.

4. Vijana wengi leo Wamepata mfano gani mzuri katika Danieli sura ya 3? (Warumi 15:4)

4 Baadaye, wakati wenzi ao hao watatu walipochukua msimamo imara juu ya suala la kuabudu sanamu, bila shaka Danieli aliukubali msimamo wao. Akiwa chini ya uongozi wa roho yeye aliandika tukio hilo kwa urefu sana, kwa ajili ya kutuonya sisi katika nyakati hizi zenye hatari.​—Dan. sura 3.

5. (a) Kwa sababu gani Danieli alihitajiwa kuwa na ujasiri ili aweze kuzungumza mbele ya Nebukadreza, na baadaye mbele ya Belshaza? (b) Ujasiri kama huo unahitajiwaje kwa Mashahidi wa Yehova leo?

5 Danieli alihitaji kuwa na ujasiri ili aweze kusimama mbele ya Nebukadreza wa Babeli mwenye nguvu, na kujulisha mafasiri ya ndoto za mtawala huyo—sana sana kwa kuwa unabii wa Danieli ulionyesha kuanguka kwa Milki ya Babeli hatimaye, vilevile kushushwa kwa mfalme huyo. (Dan. 2:36-38, 44, 45; 4:24, 25, 33) Vilevile, wakati wa kula karamu ya kuabudu sanamu ya Belshaza, wakati mwandiko wa mkono kutoka kwa Yehova ulipotokea kwenye ukuta wa nyumba ya mfalme huyo, Danieli alitakiwa awe mjasiri sana katika kumwarifu mfalme huyo na wakuu wake kwamba Babeli kuu ilikuwa imekwisha na ingepewa kwa Umedi na Uajemi. (Dan. 5:1-6, 17-28) Vivyo hivyo, ujasiri umehitajiwa kwa upande wa wengi wa Mashahidi ya Yehova leo wapate kusema kwa uhodari kuhusu hukumu za Mungu juu ya Babeli Mkuu na taratibu nyingine za ulimwengu huu zilizohukumiwa maangamizi.​—Ufu. 16:12-16, 19.

KATIKA SHIMO LA SIMBA

6, 7. (a) Sababu gani Danieli alipata sifa wakati wa utawala wa Dario? (b) Ni kwa njia gani tu adui zake wangepata nafasi ya kumwinukia? (c) Ni hali gani kama hizo zilizotokea katika wakati wetu?

6 Katika mambo waliyoyapata yenye kujaribu, Danieli na wenzi wake walimtegemea sana Yehova katika sala. (Dan. 2:17, 18) Na ilikuwa kuhusiana na sala kwamba Danieli alitakiwa aonyeshe tena ujasiri thabiti. Babeli ilikuwa imeanguka, na sasa Dario alikuwa akitawala juu ya Umedi na Uajemi, mamlaka ya ulimwengu ya nne kulingana na maandishi ya Biblia. Kwa sababu ya “roho bora” aliyopewa na Mungu wake, Danieli aliyekuwa amezeeka alipata kuheshimiwa zaidi ya wakuu wengine wote wa ufalme huo. Watu hawa wenye kujulikana, wakiwa wanaonea wivu hekima na cheo cha Danieli, walitafuta njia fulani ya kumletea uharibifu. Walakini walifahamu vema kwamba wasingepata singizio lo lote, isipokuwa wafanye hivyo kuhusiana na “sheria ya Mungu wake.”​—Dan. 6:1-5.

7 Wakiwa wanafahamu desturi ya Danieli ya kuomba na kutoa sifa kwa Mungu wake mara tatu kila siku, wafanya hila hawa walimfanya mfalme atie sahihi amri kwamba mtu ye yote ambaye angemwomba mungu au mwanadamu ye yote kwa siku 30, isipokuwa mfalme, angepaswa kutupwa kwenye shimo la simba. Amri hiyo ikawa sheria isiyobadilika ya Wamedi na Wajemi. (Dan. 6:6-9) Hii inafanana na hali leo katika nchi nyingi ambako wakuu wadogo au viongozi wa kidini, wenye kuchomwa na kukataa kwa Mashahidi wa Yehova kuwa sehemu ya ulimwengu au kupunguza utendaji wao wa Ufalme, na wakionea wivu baraka za Mungu juu ya kazi yao, hujaribu ‘kuwapata’ Mashahidi na kuwaachisha utendaji wao. Wapinzani hawa wanafahamu vema kwamba watu wa Yehova ndio watu wenye kutii sheria sana na wenye unyofu zaidi katika ujamii. Kwa hiyo wanabuni masuala yanayotia ndani sherehe na salamu za kuabudu sanamu, na kupiga kelele kwa kusema semi za chama au za utukuzaji wa taifa, kama vile “Heil (mshangilie) Hitler,” “Viva (aishi milele) Franco,” na nyinginezo.

8. Mashahidi waaminifu wa leo wamefuataje mfano wa Danieli wa kutoridhiana?

8 Danieli aliacha mfano wenye kutokeza kama nini kwa habari ya kuelekeana na masuala ya namna hiyo! Maandishi yanatuambia hivi: “Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake; (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu), akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.” (Dan. 6:10) Yeye hakuacha ibada yake kwa Yehova iliyokuwa desturi yake. Katika njia iyo hiyo, mashahidi waaminifu wa nyakati za kisasa hawaachi kumwabudu Mungu wao kwa sababu mgandamizaji fulani amepiga marufuku au kuzuia utendaji wao wa Kikristo. Huenda wakahitaji kuenenda kwa akili, kama vile kubadili utendaji wa nyumba kwa nyumba, au kwa kutoa ushuhuda kwa Biblia peke yake, au hata kukazia kuhubiri kwa vivi hivi. Walakini ni lazima waabudu! Hawawezi ‘kuacha kuyanena mambo waliyoona na kusikia.’​—Matendo 4:20.

9. Danieli alipataje ulinzi, nalo jambo hili linatiaje moyo leo?

9 Kwa sababu ya mwendo wake wa kushika ukamilifu, Danieli alitupwa kwenye shimo la simba. Walakini hiyo maana yake ilikuwa kwamba Mungu wake alikuwa amemwacha? Ala, wapi! Wala Yehova hawaachi mashahidi wake wanapotupwa kwenye gereza chafu leo. Danieli hakuwa hata ameachwa na Mfalme Dario, ambaye ‘alikesha usiku kucha, akifunga’​—yaelekea akimwomba Mungu wa Danieli. Hakika, ulinzi wa Yehova ulijionyesha kuwa wenye nguvu kuliko amri isiyobadilika ya sheria ya Wamedi na Waajemi. Asubuhi iliyofuata, wakati mfalme huyo alipofanya haraka kwenda kwenye shimo la simba na kumwuliza Danieli kama Mungu wake aliyekuwa ‘akimtumikia daima’ aliweza kumwokoa, Danieli angeweza kujibu hivi: “Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafunga makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yake, Ee mfalme, sikukosa neno.”​—Dan. 6:18-22.

10. Watu wa Yehova wanawezaje kuzuia njia za huyo “simba angurumaye,” Ibilisi?

10 Kutoa sala kwa Yehova ni jambo la maana leo kama vile katika wakati wa Danieli, na lo! namna inavyoweza kuwa na matokeo! Ingawa huenda siku hizi Mashahidi wa Yehova wasitupwe katika mashimo ya halisi ya simba, wanaishi katika ulimwengu ambao ‘adui yao, Shetani, huzunguka-zunguka kama simba angurumaye akitafuta mawindo.’ Basi, Wakristo wanapaswa kufanya nini, wanapoelekeana uso kwa uso na mateso na majaribu mengineyo? Wanapaswa kuwa wajasiri. Wanapaswa kujitiisha kwa unyenyekevu kwenye hali hizo zenye kujaribu na kuomba, wakiwa na hakika pia kwamba ndugu zao kila mahali wanaomba kwa bidii sana kwa ajili yao. Mtume Petro anatupa shauri zuri: “Mwekeeni matatizo yenu yote, maana yeye anawatunzeni. Muwe macho; kesheni! . . . Muwe imara katika imani na kumpinga [Ibilisi], mkijua kwamba ‘ ndugu zenu pote duniani wanapatwa na mateso hayo hayo. Lakini mkisha teseka muda mfupi, Mungu aliye asili ya neema yote . . . mwenyewe atawakamilisheni na kuwapeni uthabiti, nguvu na msingi imara. Kwake uwe uwezo milele! Amina.”​—1 Pet. 5:6-11, HNWW.

11. Ni mifano gani iliyopo ya siku za kisasa ya Mashahidi wa Yehova wakiokoka ‘shimbo la simba’?

11 Kumekuwako na mifano mingi ya kisasa ya Mashahidi wa Yehova wakitupwa katika ‘shimo la simba.’ Wajumbe walio kama simba wa huyo ‘simba mwenye kunguruma,’ Ibilisi, wakati wote wanatafuta kuwala watu wa Mungu. Hata hivyo, Mashahidi wake hudumu katika sala, wakitupa wasiwasi wao juu ya Yehova, na kuchukua msimamo wao “imara katika imani.” Kwa mfano, kulikuwako na msichana mchanga katika Rhodesia ambaye alikuwa amefunzwa vizuri na wazazi wake juu ya kanuni za Biblia. Alitekwa na askari magaidi. Wazazi wake walikuwa wakimhofia, kwa kuwa magaidi walikuwa na tabia ya kuwanajisi au kutia mafundisho katika wasichana tineja (miaka 13-19). Jambo peke yake ambalo wazazi wake wangeweza kufanya lilikuwa kuomba tu kwa ajili ya usalama wake. Baada ya siku kadha, yeye alirudi bila kuumizwa. “Ni jambo gani lililokupata?” wakauliza wazazi wake. “Mimi niliendelea kuwatolea ushuhuda tu,” akaeleza msichana huyo. Kwa hiyo watekaji wake wakamrudisha nyumbani. Baadaye, kiongozi wa magaidi hao alikuja kwenye kijiji hicho na kutafuta wazazi wake. Yeye aliwaambia kwamba alitaka tu kuwaona wazazi wa msichana mdogo aliyezoezwa vizuri hivyo.

12. Ni sala gani ya bidii tuwezayo kutoa wakati wote kwa Yehova, na kwa uhakika gani?

12 Ni kweli kama nini kwamba Yehova huwaangalia na kuwategemeza watumishi wake wenye kusali! Tukiwa na hakika, twaweza kuomba wakati wote kama vile Daudi: “[Yehova], Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe, uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye. Asije akaipapura nafsi yangu kama simba, akiivunja-vunja pasipokuwa na wa kuponya.” Ndiyo, huenda nyakati nyingine tukaona moyoni kwamba ‘nafsi yetu imo katikati ya simba,’ kwamba sisi tu katikati ya ‘walaji, wanadamu meno yao ni mikuki na mishale, na ndimi zao ni upanga mkali.’ Walakini sala zetu za bidii kwa Yehova, na kukimbilia kwetu katika uvuli wa mbawa zake, kutatupitisha katika majaribu haya, kama watu wenye kuendeleza ukamilifu. (Zab. 7:1, 2; 57:1-4) Kama ambavyo Daneli ‘kwa imani . . . alivyofunga vinywa vya simba,’ hata na sisi twaweza.​—Ebr. 11:33.

KATIKA “WAKATI WA TAABU”

13. (a) Katika wakati wa utawala wa Koreshi, sababu gani Danieli alihitaji kutiwa nguvu? (b) Ni ujasiri gani kama huo ambao Mashahidi wa Yehova wamehitaji kuwa nao leo?

13 Baadaye, wakati wa utawala wa Mfalme Koreshi, malaika alimtokea Danieli katika njozi na kumtia moyo, akisema: “Ewe mtu upendwaye sana, usiogope; amani na iwe kwako, uwe na nguvu, naam, uwe na nguvu.” (Dan. 10:1-19) Danieli alihitaji kuwa na ujasiri ili aweze kupokea na kuandika unabii huo wenye nguvu ambao alipewa baada ya hapo na malaika huyo, na ambao twaupata katika Danieli sura za 11 na 12. Nao Mashahidi wa Yehova wamehitaji kuwa na ujasiri ili waweze ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu’ wakati wa utimizo wa sehemu ya mwisho ya unabii huu, kwa kuwa unaeleza mapambano kati ya “mfalme wa kaskazini” wa Kikomunisti na “mfalme wa kusini” wa kibepari katika kizazi hiki cha nuklea.

14. (a) Ni nini kinachomtambulisha Mikaeli kuwa Bwana Yesu Kristo? (b) Twaweza kupataje ujasiri kutokana na maandishi katika Danieli sura ya 12?

14 Mara kadha kitabu cha Danieli kinamtaja Mikaeli, ambaye jina lake lamaanisha “Ni Nani Aliye Kama Mungu?” (Dan. 10:13, 21) Hivyo huyu mwana mkuu wa mfalme anatambulishwa kama Bwana Yesu Kristo, anayeshindana kwa ajili ya kuitetea enzi kuu ya Yehova. Akizungumza juu ya huu “wakati wa mwisho,” malaika huyo anamwambia Danieli hivi: “Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile.” (Dan. 12:1, 4) Na tuwe wajasiri sana kufanya yote ambayo Mungu wa Danieli anataka kwetu, mpaka huo “wakati wa taabu” utakapofagilia mbali ulimwengu mwovu wa Shetani. Kwa kuwa wakati huo, siku yenye utukufu ya utawala wa mileani wa Yesu itapambazuka. “Wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka” wakiwa na mataraja ya uzima wa milele duniani. Danieli mjasiri, pia, ‘atasimama kwa ajili ya fungu [lake] katika mwisho wa siku hizo.’​—Dan. 12:2, 9, 13, NW.

“IWENI HODARI NA MOYO WA USHUJAA”

15, 16. Watu wa Danieli, Israeli, walihitaji ujasiri katika wakati gani ya mapema? (b) Kama vile katika Israeli, ujasiri wa watu wa Mungu unaweza kutiwaje nguvu?

15 Leo, watu wa Mungu wanasimama malangoni kabisa ya mileani. Hali inalingana na ile ya watu wa Danieli, Israeli, katika kipindi cha mapema zaidi cha historia yao. Huu ulikuwa wakati walipokuwa wamepiga kambi kando ya Mto Yordani, tayari kuvuka na kuingia katika Nchi ya Ahadi. Mradi ulikuwa unaonekana. Walakini bado majaribu na matatizo yalikuwa mbele. Ujasiri ulihitajiwa. Kwa hiyo, nabii mwingine wa Yehova mwenye kujulikana sana, Musa mzee, aliambia Israeli maneno haya: “Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope ”‏’ala msiwahofu [adui zenu]; kwa maana [Yehova], Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha.” Na kwa mrithi wake mwenyewe aliyewekwa, Yoshua, Musa alimpa shauri kama hilo: “Uwe hodari na moyo wa ushujaa.”​—Kum. 31:1-8.

16 Hakika, watu wote wangehitaji kuwa wajasiri sana; na, hivyo, Musa aliwaagiza makuhani, Walawi na wanaume wazee wa Israeli kwa habari ya yale ambayo yangetukia kila miaka saba kwenye sikukuu ya vibanda ambayo wote wangetakiwa waiadhimishe: “Wakusanye watu, wanaume na wanawake na watoto, na mgeni wako aliyemo malangoni mwako, wapate kusikia na kujifunza, na kumcha [Yehova], Mungu wenu, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii.” (Kum. 31:9-12) Kusikiliza, kujifunza na kutii sheria ya Yehova yalikuwa mambo ya lazima ili taifa hilo lipate kufanikiwa, nalo jambo hilo pia ni la lazima leo iwapo watu wa Mungu wataweza kupewa ujasiri utakaowawezesha kuokoka mwisho wa ulimwengu.

17, 18. Ni nini kinachohitajiwa kuwa “hodari na moyo wa ushujaa,” na sababu gani wazee wa Kikristo wapaswa kukaza fikira kipekee kwa jambo hili?

17 Katika wakati huo wa hatari katika Israeli, lilikuwa jambo la lazima kwa mwanamume mzee Yoshua aonyeshe ujasiri ulio mfano bora, kama vile tu linavyohitajiwa kwa wazee wa Kikristo katika kundi leo. Hivyo, maneno ya Yehova yaliyosemwa moja kwa moja kwa Yoshua, na yenye kukazia yale yaliyokuwa yamesemwa mbeleni na Musa, yanapaswa kukaziwa fikira sana nasi: “Uwe hodari na moyo wa ushujaa, . . . Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, . . . Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa [Yehova], Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.” (Yos. 1:6, 7, 9) Yehova alimwambia Yoshua kile kilichohitajiwa ili kuwa “hodari na ushujaa mwingi,” na kutenda kwa hekima katika kila hali. Nacho kitu hicho ni nini? Acha andiko hili lijibu:

18 “Kitabu hiki cha torati [ya Yehova] kisiondoke kinywani mwako, bali [yasome kwa sauti ndogo] maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.”​—Yos. 1:8.

19, 20. Matokeo hatimaye yatakuwa nini kwa sisi kuwa “hodari na moyo wa ushujaa”?

19 Ni jambo gani lililotokea hatimaye kutokana na tendo lenye hekima la Yoshua, pamoja na utii wenye ujasiri wa watu hao? Baada ya kushinda vizuizi vyote, baada ya Yehova kupatia Israeli ushindi juu ya adui zao zote na wakati mwishowe watu wote walipokuwa wamekwisha kuchukua makao katika hiyo “nchi ijaayo maziwa na asali,” Yoshua aliweza kuwatia moyo hivi: “Munajua kwa mioyo yenu yote na nafsi zenu zote ya kama hata neno moja halikupunguka katika maneno mazuri yote [Yehova] Mungu wenu aliyosema juu yenu, yote yalitimia kwenu, hata neno moja halikupunguka.”​—Yos. 5:6; 23:14, ZSB.

20 Wakati watu wa Yehova wenye ujasiri wa nyakati za kisasa watakapokuwa hatimaye wamekwisha kutoka katika “wakati wa taabu” wenye msiba na kuingia kwenye mileani ya utawala wa amani wa Kristo, wataona kutimizwa kwa ahadi za Yehova kwa kadiri kubwa sana, ndiyo, kwa kadiri yenye kudumu. Ee sote na tuwe “hodari na ushujaa mwingi” ili tuokoke na kuingia katika mileani hiyo ambayo sasa imekaribia sana!—Kutoka The Watchtower Oct. 15, 1979.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Kama vile Yehova alivyomlinda Danieli, ndivyo anavyolinda mashahidi kutokana na “simba” wa siku za kisasa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki