Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 1/1 sura 6 kur. 21-24
  • Kuzaliwa Kupitia kwa Roho Takatifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzaliwa Kupitia kwa Roho Takatifu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • “KIUMBE KIPYA’*
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 1/1 sura 6 kur. 21-24

Kuzaliwa Kupitia kwa Roho Takatifu

(Funzo la Kitabu)

1. Ili Mkristo aliyebatizwa awe na taraja la urithi wa kimbinguni ilimpasa roho takatifu ifanye utendaji gani juu yake?

KUNA sehemu nyingine inayohusu kutenda kazi kwa nguvu hii ya utendaji ya Mungu. Yesu aliionyesha wakati aliposema hivi: “Mtu asipozaliwa kwa roho na kwa maji, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3, 5) Ni lazima Mkristo anayetazamia urithi wa kimbinguni amwige Bwana wake Yesu kwa kubatizwa katika maji. Katika njia hiyo, anaonyesha kwamba amejiweka maisha yake wakf kwa Yehova Mungu, ili afanye mapenzi yake. (Mt. 28:19, 20) Walakini ni lazima vilevile roho takatifu ifanye kazi juu yake. Sababu gani? Kwa sababu, kama vile mtume Paulo alivyoandika katika 1 Wakorintho 15:50, “nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.”

2. Baada ya kuandika juu ya kutiwa mafuta, mtume Yohana asema juu ya uhusiano gani ambao wale waliotiwa mafuta wanakuwa nao pamoja na Mungu?

2 Ikiwa wanafunzi hao wangewekwa kwenye njia ya kuingia katika ufalme wa mbinguni wa Mungu, iliwapasa ‘wazaliwe kwa mara ya pili’ na hivyo wawe wana wa kiroho wa Mungu. Kama ilivyokuwa kwa habari ya Yesu mwenyewe, mwana wa Mungu ndiye anayetiwa mafuta kwa roho takatifu. Hii inaonyesha sababu gani baada ya kuzungumza juu ya kutiwa mafuta, mtume Yohana aliyetiwa mafuta aliendelea kusema hivi katika 1 Yohana 3:1-3:

“Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. Na kila mwenye matumaini hata katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.”

3. Imeonyeshwaje katika Yohana 1:11-13 kwamba wazazi wa kibinadamu hawahusiki katika “kuzaliwa mara ya pili” kwa mtu?

3 Wazazi wa kibinadamu hawahusiki katika huku ‘kuzaliwa kwa kwa mara ya pili’ kwa mtu. Mtu mwenyewe anaposadikishwa anamkubali Yesu kuwa Masihi na kumfuata kama yeye aliyetiwa mafuta na Mungu awe Mfalme katika ufalme wa Kimasihi wa kimbinguni. Kisha inategemea mapenzi ya Mungu juu ya kama atamzaa mfuasi huyo wa Kristo kwa roho takatifu. Si wazazi wa kibinadamu, bali Mungu ndiye anayezaa watoto kusudi waende mbinguni. Ndivyo anavyosema mtume Yohana. Maneno ya Yohana ndiyo haya: “[Yeye,]” yaani, Yesu Kristo alipokuja kwa taifa la Kiyahudi karne kumi na tisa zilizopita, “alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.” (Yohana 1:11-13) Kwa kuzaliwa na Mungu, wanakuwa wana wake wa kiroho. Yeye hawazai katika tumbo la uzazi la mama.

“KIUMBE KIPYA’*

4. Ni nani ambaye huamua kama kutakuwako wana wa kiroho wa Mungu, nao hawa wanakuwaje “limbuko la viumbe vyake,” katika njia fulani?

4 Je! wazazi wa kibinadamu hawajiamulii wao wenyewe juu ya kupata watoto wa mwili na damu yao wenyewe? Ndiyo! Vivyo hivyo, na Mungu vilevile, anaamua juu ya yule ambaye atamzaa awe mwana wake wa kiroho mwenye urithi wa ki-mbinguni. “Kwa kupenda kwake mwenyewe alituzaa sisi kwa neno la kweli, tuwe kama limbuko la viumbe vyake.” Ndivyo mwanafunzi Yakobo anavyowaandikia Wakristo anaowaita “kabila kumi na mbili waliotawanyika.” (Yak. 1:1, 18) Katika ukulima, ‘malimbuko’ huvunwa kutoka kwa mazao mapya na kuwekwa wakf kwa Mungu kama kitu kitakatifu na kitu kilicho haki yake. Basi ni nani walio malimbuko ya kiroho? Ni wale wanaozaliwa na Baba wa kimbinguni kulingana na mapenzi yake mwenyewe na kupitia kwa “neno la kweli.” Anawachukua hawa kutoka katika jamaa ya kibinadamu ili wawe jamii ya kimbinguni ya Ufalme.

5. Ili Mkristo aweze kuingia ufalme wa mbinguni, 1 Petro 1:3, 4 linaonyesha kwamba ni jambo gani lililo la lazima kwake?

5 Mtume Petro aliwaandikia ‘malimbuko’ ayo hayo hivi: “Mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.” (1 Pet. 1:23) “Kuzaliwa mara ya pili” au ‘kuzaliwa tena’ ni kwa lazima ili mwishowe Mkristo aweze kuingia kwenye ufalme wa kimbinguni. Kwa hiyo Petro anaandika hivi: “Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; tupate urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu.”​—1 Pet. 1:3, 4; angalia pia 1 Yohana 3:9.

6, 7. (a) Wale ambao wamepata ‘kufanywa kuwa wana’ wanamliliaje Mungu? (b) Wale ambao wamefanywa kuwa wana namna hiyo wamo katika agano gani nao wametoka katika taifa la namna gani?

6 Mtume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo katika jimbo la Kirumi la Galatia waliokuwa wamepata ‘kufanywa kuwa wana wa Mungu’: “Kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu [alituma roho ya] Mwanawe mioyoni mwetu, [aliaye], ‘Aba, yaani, Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.”​—Gal. 4:5-7.

7 Wayahudi waliofanywa kuwa Wakristo, kama vile mtume Paulo mwenyewe, hawakuwa watumwa tena chini ya agano la torati ambalo nabii Musa alikuwa amekuwa mpatanishi wake. Sasa wao walikuwa wana wa kiroho wa Mungu na walikuwa katika “agano jipya” ambalo Yesu Kristo ndiye mpatanishi wake, Nabii aliye Mkuu kuliko Musa. Agano jipya hilo hutokeza kile ambacho agano la kale la Torati ya Musa lilishindwa kutokeza, yaani, ‘ufalme wa makuhani na taifa takatifu.’ (Kut. 19:5, 6; Ebr. 8:6-13; 1 Tim. 2:5, 6) ‘Taifa takatifu’ hilo ambalo liko katika agano jipya ni Israeli wa kiroho, ambalo washiriki wake ni Wakristo ambao ni Wayahudi au Waisraeli, kindani. Hawa wametahiriwa katika mioyo yao mahali pa nje-nje katika miili yao. Ndivyo tusomavyo katika Warumi 2:28, 29.

8. Kulingana na 2 Wakorintho 5:16, 18, sababu gani hatumtambui Mkristo ye yote, hata Kristo mwenyewe, kulingana na hali ya mwili?

8 Kukiwako mambo haya yote mapya kuhusu wana wa Mungu wa kiroho, je! twaweza kustaajabu kwamba mtume Paulo anazungumza juu ya ‘kiumbe kipya’? Hapana! ni jambo la akili kabisa afanye hivyo. Akitoa sababu juu ya uhakika wa kwamba Yesu Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu kama Mwana wa Mungu wa kiroho wa kimbinguni, mtume Paulo anasema hivi: “Hata imekuwa, sisi tangu sasa hatumjui mtu [Mkristo] awaye yote kwa jinsi ya mwili. Ingawa sisi tumemtambua Kristo kwa jinsi ya mwili, lakini sasa hatumtambui hivi tena. Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! yamekuwa mapya. Lakini vyote pia vyatokana na Mungu.”​—2 Kor. 5:16-18.

9. Ili kuingia ufalme wa kimbinguni, je! kutahiriwa katika mwili ni kwa lazima, au, kama sivyo, ni jambo gani lililo la lazima?

9 Kutokana na yote haya inakuwa wazi kwamba kutahiriwa kwa mtu mwilini kama mzao wa mwili wa mzee wa ukoo Ibrahimu au kama Myahudi wa asili si takwa kwetu ili tupate wokovu kupitia kwa Masihi, Kristo. Kwa habari ya watu wanaotazamia kwenda mbinguni, ni jambo gani hasa lililo la maana? Mtume Paulo aliyeongozwa kwa roho ya Mungu anajibu kwa maneno haya yaliyo wazi: “Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutotahiriwa, bali kiumbe kipya. Na wote watakaoenenda na kanuni hiyo, amani na iwe kwao na rehema, naam, kwa Israeli wa Mungu.” (Gal. 6:15, 16) Hawa Israeli wote wa Mungu ni “kiumbe kipya.”

10. Ili ubishi juu ya kama kutahiriwa mwili ni kwa lazima ili kupata wokovu wa milele upate kumalizwa, kundi la Antiokia lilifanya jambo gani?

10 Leo huenda watu wengi waliotahiriwa mwili wakapinga maneno hayo ya mtume Paulo, Myahudi aliyefanywa kuwa Mkristo. Walakini hata baada ya miaka kumi na sita baada ya Yesu Kristo kufa, kufufuliwa na kupaa mbinguni, kulikuwako wale waliopinga wakisema kwamba kutahiriwa mwili ni kwa lazima ili kupata wokovu wa milele. Ndivyo ilivyokuwa katika Antiokia, Shamu, ambako kwa mara ya kwanza, wanafunzi wa Kristo waliitwa Wakristo. (Matendo 11:26) Kwa hiyo, vipi basi? Kundi la Antiokia liliwatuma Paulo na Barnaba mmisonari mwenzake pamoja na wengine “wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo.” (Matendo 15:1, 2) Kwa hiyo baraza ya mitume na wanaume wazee wa kundi la Yerusalemu ikakutana ili kutoa uamuzi juu ya kama waamini wasio Wayahudi waliomwamini Kristo walipaswa kutahiriwa nje-nje katika mwili.

11. Roho takatifu ilihusikaje katika kutoa amri iliyotolewa na Baraza ya Yerusalemu, nayo amri hiyo ilisema nini?

11 Mwishowe, baada ya kuzungumza sana na kutoa ushuhuda wenye kuunga mkono jambo hilo, mwanafunzi Yakobo alitumia maneno yenye kufaa ya Amosi 9:11, 12 yaliyokuwa yameongozwa kwa roho takatifu ya Mungu na ambayo yalikuwa tayari yakitimizwa chini ya uongozi wa roho takatifu. Kwa wazi, huu ulikuwa uongozi wa roho takatifu ya Mungu kwamba kutahiriwa nje-nje katika mwili hakukuwa kwa lazima kwa waamini wa Mataifa ambao walikuwa wametolewa kutoka kwa mataifa kwa ajili ya jina la Yehova. Bila shaka roho takatifu ya Mungu ilimkumbusha Yakobo andiko hilo lenye kutoa uamuzi na pia ikamwongoza apendekeze mambo ya maana ya kuzungumzwa katika azimio ambalo lingetolewa na Baraza ya Yerusalemu. Hivi ndivyo amri ya Baraza hiyo ilivyosema:

“Kwa maana roho takatifu na sisi wenyewe tumependekeza tusiongeze mzigo zaidi kwenu ninyi, isipokuwa mambo haya ya lazima, kuendelea kushika mwiko wa vitu vinavyotolewa dhabihu kwa sanamu na wa damu na wa vitu vinavyonyongwa na wa uasherati. Ikiwa kwa uangalifu mnajiepusha ninyi wenyewe na vitu hivi, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!” (Matendo 15:3-29, NW; 21:25)

Kwa hiyo iliamuliwa kwamba lililokuwa la lazima kwa Wakristo ili kupata urithi wa kimbinguni lilikuwa, si kutahiriwa nje-nje katika mwili, bali mtu kuwa “kiumbe kipya.”

12. Kwa kutiwa mafuta kwao, kundi lililozaliwa kwa roho linakuwa na lazima ya kutimiza agizo gani, naye Yehova anawafundisha nini kuhusiana na jambo hilo?

12 Huko nyuma katika karne ya kwanza W.K. Wakristo waamini walifurahishwa na uamuzi huo wa Baraza ya Yerusalemu. Sisi wenyewe leo twaweza bado kufurahishwa na uamuzi uo huo ulioongozwa kwa roho. Kutokana na Maandiko Matakatifu twatambua kwamba kundi la Kikristo lililozaliwa kwa roho kama “kiumbe kipya,” linatiwa mafuta kwa roho ya Yehova, kama vile alivyotiwa mafuta Yule Mkuu wa kundi hilo, Yesu Kristo. Kwa hiyo, lazima sasa kundi hilo lifanye yale ambayo kutiwa mafuta kwalo kunavyolitaka lifanye, yaani, ‘kuwahubiri wanyenyekevu habari njema.’ Yesu Kristo mwenyewe hakuepuka daraka la kufanya hivyo walakini aliweka kielelezo kwa wafuasi wake wote. (Isa. 61:1-3) Wakiwa wana wa kiroho wa Mungu, wanafunzwa na Yehova yale wanayopaswa kusema kama “habari njema” kutoka Kwake. (Isa. 54:13) Kwa mfano wa uaminifu na kwa maneno ya Mwana wake Yesu Kristo, Yehova anafundisha kundi la Kikristo kwamba habari njema zenye kuokoa uhai za kutangazwa kila mahali ndizo habari njema za ufalme wa Mungu wa Kimasihi.

—Kutoka Holy Spirit—the Force Behind the Coming New Order, Sura ya 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki