Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 4/1 uku. 24
  • Sala Yake Ilijibiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala Yake Ilijibiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 4/1 uku. 24

Sala Yake Ilijibiwa

Biblia inatoa ushuhuda kwamba malaika wamewaongoza wale wanaotangaza “habari njema.” (Matendo 8:26-38; Ufu. 14:6, 7) Basi inafaa kwamba mashahidi wa Yehova wamwombe msaada na fanaka katika kazi yao ya kuhubiri. Kwa habari hii, mwanamke Mkristo katika Trinidad (kisiwa kilicho upande wa kaskazini wa Amerika ya Kusini) anaripoti hivi:

“Ilikuwa asubuhi yenye mvua na baridi nilipoondoka nyumbani nikakutane na kikundi kwa ajili ya utumishi wa shambani. Maoni yangu ya moyoni yalifanana na hali ya hewa, kwa kuwa nilikuwa sina uchangamfu. . . . Mwenzangu nami tulipoondoka, nilimwomba Yehova moyoni mwangu kwamba nikutane na mtu ambaye angependezwa kweli kweli na kujifunza Biblia. Nilikuwa ningali naomba tulipofika kwenye lango la kwanza. Tulibisha mlango na mwanamke kijana akatokea na kutualika ndani.”‏

Mazungumzo ya Biblia yalitokea na mwanamke huyo kijana alialikwa ahudhurie mkutano wa Kikristo. Alihudhuria, vilevile akatumia kwa kufaa funzo la Biblia lililopangwa na Shahidi huyo kwa ajili ya faida yake. Akiwa na tamaa ya kuwaambia wengine mambo mazuri aliyokuwa akijifunza, alianza kuongoza funzo la Biblia pamoja na mamaye na rafiki mmoja. Mwanamke huyo kijana alifanya maendeleo ya haraka naye akabatizwa kuonyesha wakf wake kwa Yehova Mungu.

Anapokumbuka hayo, Shahidi huyo, anasema hivi: “Mara nyingi nakumbuka namna nilivyojisikia asubuhi hiyo yenye mvua na kumshukuru Yehova kwa kujibu sala yangu juu ya kukutana na mtu mwenye kupendezwa kweli kweli na kujifunza Biblia.”

Ndiyo, Mashahidi wa Yehova wanachukua kwa uzito utendaji wao wa kushiriki “habari njema” pamoja na wengine, sikuzote wakiomba uongozi na baraka ya Yehova juu ya kazi hiyo. Je! unatamani kujifunza kweli ya Neno la Mungu? Iwapo ndivyo, usisite kumweleza tamaa yako Shahidi fulani atakapobisha mlango wako wakati mwingine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki