Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 1/1 uku. 24
  • Kila Silaha Itakayofanywa Juu Yako Haitafanikiwa’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kila Silaha Itakayofanywa Juu Yako Haitafanikiwa’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 1/1 uku. 24

Kila Silaha Itakayofanywa Juu Yako Haitafanikiwa’

MANENO hayo ya Yehova, yaliyoandikwa katika Isaya 54:17, yametimizwa mara nyingi katika karne zote. Kwa kweli kutimizwa kuwayo kwaweza kuwa na sehemu yenye kuchekesha, kama inavyoonyeshwa na ripoti hii kutoka nchi ya Kiafrika ambako Mashahidi wa Yehova wanateswa:

‘Katika mji wa K​——, mwenye mamlaka wa mahali hapo alituma askari wakamate kikundi cha Mashahidi ili kihojiwe. Katika siku iliyofuata Mashahidi wapata 80, wanaume kwa wanawake, walikusanywa wakapelekwa [mjini]. Baada ya kuulizwa-ulizwa maulizo, mwenye mamlaka wa sehemu aliamua kuwaadhibu wanaume kabla ya kuwafungia gerezani. Waliamriwa wakimbie kuuzunguka uwanja mkubwa wa kambi mara tano, nao askari wakaagizwa waende pamoja nao, kuhakikisha kwamba wanakimbia na kwamba hawakupitia njia za mkato. Kusudi lilikuwa kuwachosha na kufanya usawa na kufikiri kwao kuwe dhaifu.

‘Wenye mamlaka wa mahali walisahau jambo moja. Mashahidi hao waliokamatwa waliishi mashambani. Ijapokuwa baadhi yao walikuwa wanaanza kuzeeka, walikuwa wamezoea kukimbia, kwa kuwa walikuwa wakiwinda wanyama kwa chakula chao. Kwa hiyo hawakuwa wamevunjwa moyo na wazo la kukimbia kuuzunguka mji mara tano wakiwa na askari. Lilikuwa jambo lenye kukubalika zaidi kuliko kupigwa. Kinyume chake, askari ndio hawakufurahishwa na wazo la kulazimika kukimbia ili wawasimamie hao Mashahidi.

‘Baada ya kukimbia mara moja, Mashahidi wa Yehova walikuwa wakikimbia kwa urahisi. Lakini, askari walikuwa wakiwatia moyo wakimbie polepole, na kuongeza mwendo wakati tu wanapokaribia mahali wanapoweza kuonekana na wenye mamlaka wa mahali hapo. Mashahidi walieleza kwamba “sisi tunatii tu maagizo” na, polepole, askari wakaanza kuachwa nyuma.

‘Baada ya kukimbia mara ya pili, baadhi ya Mashahidi walikuwa wameanza kuchoka, lakini waliendelea kwa uaminifu. Lilikuwa jambo lenye kushangaza kama nini wakati huo wakati ndugu mmoja mzee, wa umri wapata miaka 60, alipowapita wengine wote na kuongozo. Kufikia wakati huo tukio hilo lilikuwa limevuta watazamaji waliozidi kuongezeka walioanza kupiga kelele na kushangilia. Jambo lote hilo lilikuwa limeanza kuchekesha huku mwanamume mzee “akiongoza kikundi hicho,” na bila askari hata mmoja kuonekana po pote. Hata baadhi ya wenye mamlaka wa sehemu walikua wakianguka kwa kicheko kwa sababu ya tamasha hiyo.

‘Kwa kuona kwamba hata Mashahidi hao walikuwa wakifurahia “mchezo” huo na kwamba wote walikuwa wamekimbia na kwamba hakuna hata mmoja wao aliyejaribu kutoroka, na sana sana kwamba mwanamume mzee alikuwa amewashinda wengine wote, mwenye mamlaka wa mahali hapo aliwahurumia, akazikomesha mbio hizo, na kuwaachilia Mashahidi. Mashahidi hao waliitumia vizuri nafasi hiyo kuwatolea ushuhuda watazamaji. Mashtaka yote yakasahauliwa.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki