Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 2/1 uku. 8
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 2/1 uku. 8

Je! Wakumbuka?

Umesoma matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kwa uangalifu? Ikiwa ndivyo, bila shaka utayakumbuka mambo haya:

● Je! ni mtu binafsi anayejichagulia kama tumaini lake litakuwa la kidunia ama la kimbinguni?

Hapana. Kabla mtu hajakuwa na tumaini lo lote la Kimaandiko, ni lazima ajiweke wakf kabisa kwa Yehova Mungu na kubatizwa, akikubali kufanya mapenzi ya Mungu kuanzia na wakati huo. Yehova anafanya mapenzi yake yatendeke kupitia kwa utendaji wa roho yake takatifu, na kati ya washiriki wa lile “kundi dogo” roho hiyo imechochea tumaini la kimbinguni. Walakini, ule “mkutano mkubwa” unaokusanywa sasa wakiwa na taraja la kuishi duniani milele, wanapokea vilevile roho ya Mungu. (Luka 12:32; Rum. 8:14-17)—2/1/81 uku. 7. 

● Inatupasa kutendaje ikiwa mtu fulani anatutungia nia mbaya?

Inafaa kutokasirika. (Mhu. 7:9) Sisi kama Wakristo, twapaswa tutamani kumwiga Mungu, ambaye huonyesha sifa ya kujiweza anaposhtakiwa. Yeye atatufariji, nasi tutapata furaha ikiwa tutaendelea ‘kumtumaini [Yehova] na kufanya mema.’ (Zab. 37:3) Mungu akitaka kututetea, aweza kufanya hivyo wakati ufaao.—9/15/80 uku. 8.

● Ni ‘maumivu gani ambayo hayatakuwapo tena’ kati ya raia za kidunia za utawala wa Ufalme?

Ahadi ya kiunabii ya kwamba maumivu hayatakuwapo tena haimaanishi kwamba raia za Ufalme duniani watakuwa hawawezi kuona maumivu yo yote. (Ufu. 21:4) Uwezo wa kuona maumivu ya mwilini waweza kufaidi. Walakini maumivu ya akilini, ya moyoni, na maumivu makali yanayotokana na dhambi na kutokamilika ‘hayatakuwapo tena’ katika maana ya kwamba sababu zinazoyaleta zitaondolewa.—10/1/80 uku. 5.

● Kwa Wakristo, ni nini iliyo njia kubwa zaidi ya kuonyesha upendo kwa Mungu na jirani?

Kuhubiri “habari njema” ni njia moja kubwa ya kuonyesha kwamba tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote, nafasi, nguvu na akili. (Luka 10:27) Vilevile kuwafundisha wanadamu wenzetu “habari njema” ni mojayapo ya njia kubwa za kuonyesha kwamba tunawapenda kwa sababu kufanya hivyo kunawasaidia wawe na hali yenye kukubalika mbele za Yehova.—10/1/80 uku. 24.

● Mtu anafaidikaje kwa kuwa mwanafunzi aliye wakf na kubatizwa wa Yesu Kristo?

Mtu kama huyo anaridhika kwa kujua kwamba anafanya yale yanayokubalika mbele za Yehova Mungu na Yesu Kristo. Kama Mkristo, anapata vilevile ndugu, dada, mama na watoto katika maana ya kiroho.—10/15/80 uku. 11.

● Babeli Mkuu ni nini, na kwa sababu gani tutii mwito wa ‘kutoka kwake’?

Babeli Mkuu ni milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, nako kutoka kwake ndiyo njia peke yake ya kuepuka kuharibiwa pamoja naye wakati wa “dhiki kubwa inayokuja. (Mt. 24:21; Ufu. 18:4) ‘Kutoka kwake’ ni jambo la haraka, kwa kuwa haitawezekana kutoka katika Babeli Mkuu baada ya wale waliokuwa hawara zake za kisiasa kumgeukia. (Ufu. 17:15-18)—11/1/80 ku. 9, 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki