Kukumbuka Kifo cha Yesu
Wakati wa sherehe isiyo na mambo mengi, Yesu alitumia divai na mkate usiotiwa chachu kuwa mifano ya uhai wa kibinadamu ambao angetoa dhabihu kwa ajili ya wanadamu. Alipokuwa akianzisha sherehe hiyo, alisema: “Endeleeni kufanya hivi kwa ukumbusho wangu.”—Luka 22: 19, NW.
Mwaka jana watu mamilioni walikumbuka Yesu kwa kuhudhuria ukumbusho wa kifo chake kwenye mikutano ya pekee iliyodhaminiwa na Mashahidi wa Yehova. Wewe unakaribishwa kwa mikono miwili uhudhurie mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka huu kwenye Jumba la Ufalme lililo katibu zaidi na nyumbani kwako. Utafanywa Alhamisi, Aprili 4, baada ya jua kushuka. Waulize Mashahidi wa Yehova wa kwenu wakueleze wakati wenyewe.