Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/1 uku. 23
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu ana maoni gani kuhusu Kuhusu Kuvuta Sigara?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Watetea Tumbaku Waanzisha Puto la Hewa-Joto
    Amkeni!—1995
  • Je, Kuvuta Sigara Ni Dhambi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kwa Nini Uache Kuvuta Sigareti?
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/1 uku. 23

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

◼ Je! ingekuwa vibaya kuvuta sigareti zisizo na tumbaku ili kusaidia kushinda mazoea ya kutumia tumbaku?

Kuna sababu kadha kwa nini jambo hilo linapasa kuepukwa na watu wanaotaka kutumia mashauri ya Maandiko na kuwa washiriki wa kundi la Kikristo.

Watu wengi mmoja mmoja waliokuwa na mazoea ya kutumia tumbaku, na hasa sumu ya dawa ya kulevya iliyo katika tumbaku, wamejaribu kuvunja zoea hilo. Njia moja imekuwa kutumia vitu vingine, kuvuta sigareti zilizofanyizwa kutokana na majani mengine yasiyo na sumu ya tumbaku. Huenda hilo likaelekea kuwa jambo la kutamanika kwa sababu hii: Mvutaji anaepuka sumu ya tumbaku, lakini magumu makubwa ya kuvunja zoea ambalo limekuwako kwa muda mrefu huenda yakaonekana kama kwamba yameacha kuwa makali kwa sababu anaweza bado kushika kitu na kukivuta, sigareti isiyo ya tumbaku.

Ili kuthamini ni kwa sababu gani jambo hilo haliwapasi Wakristo, fikiria sababu fulani zinazofanya Mashahidi wa Yehova wasivute sigareti.

Kwanza, zoea Iililoenea sana la kuvuta tumbaku​—katika sigareti, viko au sigara​—linapingana na yale ambayo mtume Paulo aliandikia kundi la Korintho: “Rafiki wapendwa, acheni tujitakase na kila kitu kinachochafua ama mwili ama roho.” (2 Wakorintho 7:​1, The Twentieth Century New Testament) Muda mfupi tu kabla ya maneno hayo, Paulo alikuwa amesema juu ya utendaji mbalimbali wa kidini uliokuwa sawa na ‘kugusa kitu kilicho kichafu.’ (2 Wakorintho 6:17) Halafu akatoa maelezo zaidi katika 2 Wakorintho 7:​1, nayo yangehusu utendaji wo wote ambao ungechafua Mkristo kiadili, kiroho au kimwili. Kwa uhakika kanuni hiyo inatumika kuhusu mazoea ya kutumia tumbaku ambayo sana sana ni ya kisasa.

Kwa kuwatazama watumiaji wa tumbako wakiwa karibu nawe, labda umeona kwamba vidole na meno yao vinakuwa na alama, na inaelekea unajua kwamba mapafu ya wavutaji yanakuwa yametiwa katika hali ya weusi na ya kuchafuliwa. Zoea lao ni chafu na linahatirisha sana afya na uhai wako. Lakini je! dhara lenyewe linatokea kwa sababu wanavuta tumbaku tu? Ni vigumu kuwa hivyo. Hata mtu akivuta kwa ukawaida sigareti zilizofanyizwa kutokana na mmea mwingine​—uwe ni bangi, saladi, mhindi au kitu kingine​—si jambo la asili kuvuta moshi siku baada ya siku. Je! wewe hukubali kwamba kuvuta moshi wo wote kwa ukawaida kungechafua mapafu na kungeweza kuhatirisha afya ya mtu? Kwa hiyo kama moshi wenyewe unatokana na tumbaku, bangi, au namna fulani ya sigareti zisizo na sumu ya tumbaku, kwa ufupi kuvuta hakuwafai watu wanaotaka kuishi kulingana na shauri lililo kwenye 2 Wakorintho 7:1.​—Linganisha Warumi 12:1.

Wala mtu hawezi kusemwa kuwa anaonyesha upendo wa jirani kwa jamaa na washirika wake hali anawalazimisha wavute moshi wake, hata kama unatokana na kitu kingine kilicho tofauti na tumbaku.​—Marko 12:​31,

Zaidi ya hilo, kuvuta tumbaku kumeenea sana hivi kwamba watazamaji wakiona mtu akivuta namna fulani ya sigareti, sigara au kiko, hawangejiona kuwa vimbelembele wakidhani ni tumbaku anayovuta. Kwa hiyo hata ikiwa mtu atakuwa akivuta sigareti zile tu zisizo na sumu ya tumbaku, huenda bado watazamaji wakakwazwa au wakakata shauri kwamba Mashahidi wa Yehova wana ugeugeu katika kuepuka zoea lenye kuchafua na kudhuru afya la kuvuta tumbaku.​—Luka 17:​1,2.

Wengi ambao sasa ni Wakristo walio watumishi safi na wenye afya wa Yehova wameweza kushinda tabia ya kuvuta tumbaku bila kugeukia uvutaji wa namna nyingine. Maelezo yenye msaada juu ya jambo hili yanapatikana katika makala inayosema “Udhaifu Huo Unaweza Kushindwa” katika toleo la Mnara wa Mlinzi wa Machi 15, 1985.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki