‘Msichana Huyu Anayajua Majibu Yote ya Biblia’
Mwanamke mmoja katika Mkoa wa New York alimpelekea kwa posta rafiki yake waliyekuwa wakisoma darasa moja zamani, na sasa akawa ni mwenye watoto, nakala ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Baada ya muda fulani mwanamke huyo akapokea barua kutoka kwa huyo mwenzake. Aliandika hivi akisema habari za binti yake:
“Elizabeth anakipenda sana kitabu hicho—ni hicho tu anitakacho nimsomee wakati wa usiku. Mimi humsomea hadithi 5 kila usiku (kwa maana umri wake ni miaka 5), na juma iliyopita mwalimu wake wa Shule ya Jumapili aliniambia kwamba nyakati zote yeye huwa na uhakika kwamba akimwuliza Elizabeth maswali ya Biblia atayajibu yote. Kwa hiyo pasipo shaka kitabu hiki kiliandikwa na mtu fulani mwenye kuelewa vizuri mambo wayapendayo watoto.”
Mwanamke yule wa New York anasema hivi kuhusu yule mwingine waliyekuwa darasa moja zamani: ‘‘Yeye aliyatoa maoni hayo kwa unyofu wa moyo, kwa maana yeye ni mtu wa kusema mambo wazi na asingalikisifu kitabu hicho kama asingalikipenda.”
Sisi tunaona kwamba hata wewe utakipenda sana kitabu hiki chenye picha nzuri na kilichopigwa chapa kwa maandishi makubwa. Masimulizi 116 ya Biblia yaliyomo yanasaidia msomaji kujua kwa kiasi fulani ni mambo gani hasa yaliyomo katika Biblia. Hadithi zimepangwa kwa kufuatana na wakati ambao matukio yalitendeka katika historia. Utapata msaada ujue wakati mambo yalipotukia katika historia, namna yalivyohusiana na mengine kwa habari ya wakati wa kutukia kwayo. Kipokee kitabu hiki chenye kurasa 256 kwa kujaza hati yenye anwani iliyopo chini na utupelekee.