‘Niliomba Nipewe Kitabu Hicho’
Hivyo ndivyo kijana mmoja katika Zimbabwe alivyoandika. Rafiki yake alikuwa na nakala ya “Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia,” lakini akakataa kumpa ajapoombwa sana. Hata hivyo, yeye alimpa anwani ya kuandikia ili kupata kitabu hicho, na akasema: “Nenda kanunue chako.” Kwa hiyo kijana huyo aliandika hivi:
“Mimi sina pesa, walakini tafadhali, mheshimiwa, niambie bei ili nikope kutoka kwa baba yangu wa kambo ambaye ni tajiri. Tafadhali, mheshimiwa, sikiliza sala yangu. Ninatamani kama nini uniletee kitabu hicho. Nafikiri sitakuwa mkatili kwa rafiki zangu kama mvulana yule niliyemwona na kitabu hicho. Kila siku nitangojea jibu lako. Mimi nina umri wa miaka kumi na miwili.”
Ulimwenguni pote kitabu hicho kimetakwa na watu wengi sana. Tayari kinapatikana katika lugha zaidi ya 40, na karibu nakala milioni 20 zimekwisha kuenezwa.
“Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia” kina chapa kubwa na picha kubwa zaidi ya 125, nyingi yazo zikiwa na rangi nyingi. Masimulizi yacho ya Biblia 116 yanampa msomaji wazo fulani juu ya yanayosemwa na Biblia. Hadithi hizo zimepangwa katika utaratibu ambao matukio yalitokea katika historia. Utaona kuwa jambo hilo linasaidia sana katika kujifunza ni wakati gani, kuhusiana na matukio mengine, mambo yalitokea katika historia. Pokea kitabu hicho chenye thamani cha kurasa 256 kwa kujaza na kupeleka kwa posta hati hii yenye anwani.
Tafadhalini nileteeni, bila ada ya posta, kitabu chenye ngozi ngumu “Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia,” nimekilipia shilingi 25.00 (Z9).