Kitabu cha Watoto na Watu Wazima Pia
Biblia imekuwa kitabu cha kuvutia sana watoto na watu wazima pia kwa sababu ya habari zilizomo katika “Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.” Hiki ni kitabu chenye picha malidadi. Barua moja iliyotoka nchi ya Denmark inaeleza maoni aliyokuwa nayo mwanamume mzee aliyekipokea kitabu hiki:
“Mimi nilifurahi ajabu kumwona akipendezwa sana na ‘Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.’ Macho yake yaling’aa kwa furaha kila mara alipofungua ukurasa tofauti wa kitabu hicho. . . . Niliporudi muda fulani baadaye, akachukua nakala zaidi za kitabu hicho, akanieleza kwamba yeye anasoma kwa sauti kubwa ili vitukuu (watoto wa watoto wake) walio wengi waweze kusikia. Mwanamume huyu ana umri wa miaka 97.”
Wewe unaweza kujipatia kitabu hiki chenye ngozi ngumu cha kurasa 256. Kina herufi kubwa zenye kusomeka vyepesi. Ijaze hati yenye anwani iliyopo chini kisha uitume.
Tafadhali nipelekeeni “Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia,” ambacho ni kitabu chenye ngozi ngumu cha kurasa 256, mkiwa mmelipia bei ya posta. Mnipelekee kitabu hicho pamoja na kile kijitabu cha bure “Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona.” Mimi nimewapelekea Kshs. 25/-, Tshs. 35/-, RWF 250.