Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 8/1 kur. 6-7
  • Walifanikiwa-Kwa Unyofu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walifanikiwa-Kwa Unyofu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Yeye Angesema Uongo kwa Niaba ya Tajiri Wake?
  • Mnyang’anyi Mwenye Kutumia Silaha Abadilika
  • Maisha Yenye Tazamio la Wakati Ujao
  • Uwe Mnyofu Katika Mambo Yote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Uwe Mnyoofu Katika Mambo Yote
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Faida ya Kuwa Mnyoofu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 8/1 kur. 6-7

Walifanikiwa-Kwa Unyofu

INGEKUWA vizuri kama nini kuacha milango yako wazi bila woga wa kunyang’anywa mali! Maisha yangekuwa mazuri kama nini na yenye kupendeza kama nini kuweza kumtumaini kila mtu na wewe kutumainiwa!

Lakini yote hayo yanaanza na mtu binafsi, sivyo? Jitihada yetu ya kibinafsi inakuja kwanza.

Ebu fikiria mifano michache ya watu ambao wameyashinda maelekeo yao mabaya na kujitahidi wakawa huru kwa sababu walitaka kufanya hivyo.

Je! Yeye Angesema Uongo kwa Niaba ya Tajiri Wake?

Katika Rio de Janeiro, Brazil, mwanamume mmoja alikuwa anakabili ama kupoteza kazi yake ama sivyo aendelee kuwadanganya makastoma (wanunuzi) wake. Kwa sababu gani alijikuta katika hali hiyo? Baada ya kuwa mwenye kufanya bila kusita yaliyotakwa na tajiri wake, alianza kujifunza kanuni za Mungu katika Biblia. Kufuatia hilo angefanya nini? Angefanya mara moja yaliyosemwa na Biblia? Hata kidogo. Aliifuata njia rahisi; aliacha kujifunza Biblia. Kwa muda mfupi akaendelea kuwa na kazi yake. Lakini mambo hayakwishia hapo.

Dhamiri yake haingeweza kumruhusu atulie tena na akajiuzulu. (Warumi 2:14, 15) Lazima sala zake alizomtolea Mungu za kutaka dhamiri njema ziwe zilisikiwa, kwa maana alimtafuta mmoja wa Mashahidi wa Yehova walioishi karibu naye ili aendelee na funzo lake la Neno la Mungu. Kwa kupendeza, haikuchukua muda mrefu kabla aliyekuwa tajiri wake kumwita. Kwa sababu gani? Alitaka arudi kazini. Mtu aliyeandikwa kuchukua mahali pake alikuwa mdanganyifu, si kwa makastoma (wanunuzi) peke yao bali hata kwa tajiri mwenyewe! Wakati huo, akiwa ameazimia kwa dhati (kwa nguvu) kuwa mnyofu, mwanafunzi huyo wa Biblia akasema angefikiria kurudi kazini, lakini kwa matakwa yake mwenyewe​—kuwa mnyofu chini ya hali zote. Wakapatana juu ya takwa hilo. Unyofu ulishinda, na mwanamume huyo sasa ni Mkristo aliyebatizwa.

Mnyang’anyi Mwenye Kutumia Silaha Abadilika

Je! mnyang’anyi mwenye kutumia silaha anaweza kubadili njia yake mwishowe’? Katika upande wa kusini wa Brazil kijana mwenye umri wa miaka 19 alikuwa sehemu ya genge (kikundi) lililokuwa likivunja nyumba. Alipokuwa gerezani alipata vitabu vya Biblia vinavyochapishwa na Sosaiti. Mambo aliyojifunza yalimshtua. Matakwa ya Yehova kwa Mkristo yalikuwa tofauti sana na yale ya njia yake mwenyewe ya maisha, ingawa kwa jina alikuwa Mkatoliki.

Polepole akafanya maendeleo. Kuthamini kwake kuliongezeka huku mashaka yake yalipokuwa yakiondolewa. Wakati huu yeye mwenyewe anajifunza Biblia pamoja na wafungwa wengine, naye anajulikana kwa wakuu wa gereza, mawakili na mahakimu kwa sababu ya badiliko la ajabu. Wakuu wamevutwa sana na tabia yake iliyobadilika hata kwamba wanaruhusu funzo la Biblia la kikundi lifanywe kila juma, na kuhudhuriwa na watu 40.

Katika London, Uingereza, kijana mmoja alichukizwa sana na taratibu iliyomzunguka hata akawa mwasi wa moja kwa moja. Akiwa hana kazi ya kawaida na akiwa hataki kufanya kazi, aliona kwamba kishawishi cha kuiba kilikuwa kikubwa. Akiwa mpeleka barua kwenye nyumba za watu alikuwa akijichukulia vifurushi na pia akawa akiiba tamutamu katika maduka. Upesi akawa mmoja wa genge lenye kuvunja nyumba, lakini akakamatwa, akapelekwa mahakamani na kupatikana na hatia. Akiwa mwenye umri wa miaka 16 tu, alipelekwa kwenye tengenezo la Kiingereza la kurekebisha tabia liitwalo Borstal. Baada ya miaka miwili aliachwa huru, na kwa muda fulani akajiepusha na matata, kwa kuogopa kizuizi zaidi.

Je! tengenezo hilo lilikuwa limemrekebisha? Hata. Baada ya mwaka mmoja akaanza wivi. Akiwa kondakta wa bas alitumia kwa faida yake saa ambazo watu wanasafiri kwa wingi na kwa haraka akawa akiweka pesa hizo mfukoni mwake badala ya kukata tikiti. Kwa mara nyingine akaipoteza kazi yake. Wakati huo akaoa, lakini tangu mwanzo matatizo mazito yakaanza kutokea kwa sababu ya ulevi na kufanya ngono pamoja na wanawake wengine nje ya ndoa.

Kufikia hapo, miezi miwili baada ya arusi yao, wenzi hao wawili wakafahamiana na Biblia. Walikubali funzo la Biblia. Je! lilitokeza badiliko la ghafula? Kwa kweli sivyo. Mwendo wa udanganyifu ulikuwa umetia mizizi ndani sana. Akaacha kuketi wakati wa funzo. Hata hivyo, mbegu fulani ilikuwa imepandwa.

Anapoangalia nyuma, yeye anakubali kwamba ndani-ndani alijua kwamba aliyokuwa amesikia katika juma chache za funzo la Biblia yalikuwa ndiyo ile kweli na ndiyo iliyokuwa njia pekee ya kumnyosha. Moyo wake ulitaka kufanya hivyo, lakini alikosa nguvu. Siku moja alipigana na polisi. Alikamatwa kwa ajili ya kuendesha motokaa akiwa mlevi katika motokaa isiyo na bima. Asubuhi iliyofuata alipojitazama kwenye kioo na kuona shati lake jeupe limefunikwa kwa damu, aliichunguza hali yake.

“Nilikuwa na njia mbili tu zilizo wazi,” anasema. “Futi sita chini ya mchanga au kujirekebisha; kuchukua msimamo. Nilisali kwa Yehova atume Shahidi fulani aje. Na kwa hakika, upesi akaja nami nikamwomba ajifunze Biblia pamoja nami. Hiyo ilikuwa katika Novemba 1973. Katika Machi 1974 nilibatizwa.”

Je! mambo yamekuwa rahisi kwake huyo aliyekuwa mwivi na msema uongo? “Hapana,” anajibu. “Kumekuwako nyakati za kusisimuka na kuhuzunika, na kutaka kurudia kidogo nia ya kale. Bila msaada wa Yehova singaliweza kamwe kuondoka katika mvurugo niliokuwa ndani yake.”

Anajua kwamba furaha inategemea kufuata sheria ya Mungu ya upendo. “Jamaa yangu imeunganika katika Jumba la Ufalme. Nami ninajitahidi sana kuwalea watoto wangu katika njia ya Mungu. Ninasikitika kwamba wazazi wangu hawakujua ninayojua na kwa hiyo hawangeweza kunisaidia.”

Maisha Yenye Tazamio la Wakati Ujao

Katika ulimwengu huu wenye mavumbuzi makubwa mno, huenda wengine wakafikiri kwamba “nafasi hufanya mtu awe mwivi.” Lakini hata waliokuwa wevi hapo kwanza wanaweza kuona kwamba maisha ya unyofu yanatoa mengi zaidi.

Kwa sababu gani? Kwa sababu yanatokeza uadilifu, dhamiri njema, kutumainiana na, zaidi ya yote, Mungu kupendezwa naye vizuri. Hilo ni takwa la msingi la kuishi katika mfumo mpya wa Mungu unaokaribia sana, wakati ambao hakutakuwa kuiba tena wala ukosefu wa unyofu.

Jambo kuu lenye kuongoza litakuwa ni upendo katika maisha yenye kuridisha sana na yenye kutosheleza kabisa katika dunia iliyo paradiso chini ya utawala wa mileani wa Kristo Yesu. Unyofu utakuwapo kila mahali. Kwa sababu gani usichunguze zaidi juu ya tumaini hilo linalofaa sasa? Mashahidi wa Yehova katika mtaa wenu watapendezwa sana kukusaidia wewe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki