Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 8/1 uku. 23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Mtoto Aliyeahidiwa
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Alikata “Kauli Moyoni Mwake”
    Igeni Imani Yao
  • Mtoto wa Ahadi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 8/1 uku. 23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ Hata wakati Yesu alipokuwa kitoto, yeye alikuwa mkamilifu; na basi Luka 2:22-24 inasema Mariamu alimpeleka Yerusalemu “zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati”?

Yesu hakuhitaji kwa sababu alizaliwa akiwa mwana wa Mungu aliye mkamilifu wa kibinadamu. (Waebrania 7:26; 1 Petro 1:19; 2:22) Kwa hiyo yeye hawezi kuhesabiwa kati ya lile neno lenye kusema “kwao” katika Luka 2:22-24, ambapo panasomwa hivi: “Kisha, zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati ya Musa, walikwenda naye [mtoto Yesu] hata Yerusalemu, wamweke kwa Bwana, (kama ilvyoandikwa katika sheria ya [Yehova]), kila mtoto mwanamume aliye kifungua mimba ya mamaye na aitwe mtakatifu kwa [Yehova], wakatoe na sadaka, kama ilivyonenwa katika sheria ya [Yehova], Hua wawili au makinda ya njiwa wawili.”

Kwa haki Yusufu na Mariamu walitaka kufuata vile sheria ilivyotaka kwa habari ya kuzaliwa kwa mtoto. Takwa moja lilikuwa kwamba mwana-mzaliwa-wa-kwanza apokezwe kwa Mungu hekaluni na kukombolewa kwa malipo, Mariamu na Yusufu walienda Yerusalemu wakafanye hivyo. (Hesabu 18:15, 16) Takwa jingine, lililokazia kwamba wanadamu walikuwa wenye dhambi na walipitishia watoto wao hali ya kutokamilika kupitia uzazi, lilihitaji mwanamke atakaswe baada ya kuzaa. Ikiwa mtoto wake alikuwa wa kiume, mwanamke huyo alikuwa mchafu muda wa siku 40, na siku 80 ikiwa mtoto alikuwa wa kike. Dhabihu za usafishaji zilitolewa mwishoni mwa kipindi hicho cha kutakaswa. (Mambo ya Walawi 12:1-8) Hata Mariamu na Yusufu wangelifuata takwa hilo baada ya kufunga safari kwenda Yerusalemu.

Walakini, Luka 2:22 imetokeza maulizo kwa sababu inataja “siku za kutakasika kwao.” Neno “kwao” linawataja nani? Hati fulani za maandishi ya kwanza zina neno la Kigiriki lenye kumaanisha “yeye” kwa hali ya kike, kama kwamba andiko hilo linataja kutakaswa kwa Mariamu peke yake. Ni wazi kwamba tofauti hiyo ya kimaandishi iliingizwa na wanakiliji waliotatizwa kwa kusoma neno hilo “kwao.” Ingawa hivyo, sasa neno “kwao” linakubaliwa kuwa ndilo sahihi, kwa maana linaungwa mkono na hati za kale zilizo bora zaidi. Basi, je! neno “kwao” linawataja nani?

Kama ilivyokwisha kusemwa, lisingeweza kumtia ndani Yesu, kwa maana yeye hakuwa na uhitaji wa kusafishwa. Walakini, wanachuo fulani wanashikilia kwamba Yesu alihesabiwa humo wakitegemea msingi wa kwamba yeye ‘alikombolewa’ katika safari iyo hiyo waliyofunga kwenda hekaluni. Walakini, dai hilo halina nguvu, kwa sababu ‘kutakaswa’ na ‘kukombolewa’ yalikuwa ni matakwa mawili yenye kutofautiana na ile Torati. Inaelekea zaidi kuwa Yusufu alikuwa mmoja wa wenye kuhusika katika neno “kwao.”

Kwanza, mstari huo unaendelea kusema kwamba “walikwenda [na Yesu] hata Yerusalemu.” Wenye kwenda naye ni Yusufu na Mariamu. Na ingawa ile desturi ya utakaso ilimhusu mamaye peke yake kabisa kabisa, Yusufu ndiye aliyeipanga safari, naye akiwa ndiye kichwa cha jamaa alikuwa na daraka la kuhakikisha kwamba dhabihu imetolewa. Kwa sababu hizo huenda ikawa Luka alimhesabu mumewe Mariamu (baba wa kambo wa Yesu) katika neno hilo “kwao.” Hivyo Luka 2:22 ingeweza kueleweka kuwa inamaanisha kwamba: ‘Zilipokwisha siku za utakaso Mariamu na mumewe, ambaye alikuwa chini ya wajibu wa kuhakikisha kwamba Torati imefuatwa, walimleta Yesu huko juu Yerusalemu wakampokeze kwa Yehova.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki