Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w82 10/1 kur. 12-15
  • Kwa Sababu Gani Kuomba, “Ufalme Wako Uje’?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Sababu Gani Kuomba, “Ufalme Wako Uje’?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Iweni Hodari!
  • Ule Ufalme​—ni Halisi
  • Sala Yetu ya Shauku
  • Ufalme wa Mungu Watawala
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Mafundisho ya Yesu Kuhusu Ufalme wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
w82 10/1 kur. 12-15

Kwa Sababu Gani Kuomba, “Ufalme Wako Uje’?

“Ufalme wa Mungu hautakuja kwa kuonekana waziwazi, wala watu hawatakuwa wakisema, ‘Tazama hapa!’ au, ‘Hapa!’ Kwa maana tazama! ufalme wa Mungu uko katikati yenu.”​—Luka 17:20, 21, NW.

1, 2. Kupatana na vyanzo vya habari vya kutegemeka, kwa sababu gani nyakati zetu zaweza kusimuliwa kuwa za kuogopesha?

JE! SISI tunauhitaji ufalme wa Mungu? Hakika tunauhitaji sana! Kwa maana leo sisi wanadamu tunapita katika wakati ulio wenye hatari kuliko nyakati zile nyingine za historia yote. Hizi ni nyakati zenye kuogopesha sana! Likikazia hilo, gazeti Guardian Weekly la Manchester la Juni 7, 1981, lilisema hivi: “London, Paris, Bonn, Roma, na Brussels yote ingeweza kuharibiwa kabisa na mizinga ya SS-20 ambayo Urusi imeunda tangu mwanzoni mwa mwezi huu. . . . Kila mzinga unachukua vichwa viwili vyenye baruti ya kilotani 150, hivyo kwamba nguvu za mlipuko juu ya kila mmojawapo miji hiyo kwa jumla zingekuwa mara 30 zaidi ya zilizolipuliwa juu ya Hiroshima. Ikifyatua tano kati ya SS-20 zake Urusi bado ingekuwa na 210 zilizosalia za kulipua kwingine, bila kutumia jeshi lake la ndege za makombora, kikosi cha sabmarini, au ile mizinga 1,400 yenye kuweza kuruka kutoka bara moja mpaka nyingine, kila mmoja ukiwa unachukua megatani nyingi ambayo inahifadhiwa kwa ajili ya pindi za hatari zaidi.”

2 Gazeti Time la Oktoba 26, 1981, kwenye habari yalo “Kuupa Ulimwengu Silaha” ambayo ilikuwa msingi wa jalada, lilisimulia hali hiyo kuwa “isiyozuilika na hakuna vizuizi vinavyoonekana.” Lilizungumza juu ya “jambo la kawaida lenye kuogopesha sana na lenye kuongezeka sana: kwa mataifa makubwa na madogo pia, njia kuu ya ushauriano imekuwa ni uuzaji wa silaha . . . [silaha ndizo] ‘vitegemezaji vikuu vya siasa za ulimwengu zilizoharibika.’”

3. (a) Kulingana na Mwanzo 6:11, 13, siku za Nuhu zilifananaje na siku zetu? (b) Ni maneno gani ya Yesu yenye kutimia kwa njia yenye kutokeza sana?

3 Kweli kweli, “kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu,” dunia ‘imejaa dhuluma’ (‘jeuri,’ NW) na uwezo mwingi sana wa kuleta jeuri yenye kutokeza msiba mkubwa sana. (Mwanzo 6:11, 13; Mathayo 24:37) Haishangazi kwamba Yesu alipotabiri juu ya “mambo yanayokuja” kwenye mwisho wa ulimwengu, alizungumza juu ya “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea . . . , huku wanadamu wakizimia moyo kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.”​—Luka 21:25, 26, 36, NW.

Iweni Hodari!

4. Kwa sababu gani maoni yetu yapasa kuwa ya kutazamia mazuri?

4 Hata hivyo, je! tunaweza kutazamia kwamba Muumba wa dunia yetu yenye kuvutia ataruhusu watu au mataifa yenye jeuri, yanayofurahia kutumia silaha yaiharibu kazi ya mikono yake? Je! tunaweza kuwaza kwamba Yehova Mungu ataruhusu wanadamu wale ambao ‘wamefua panga zao zikawa majembe’ na ambao wanamwabudu “katika roho na kweli” waharibiwe na adui zake? (Isaya 2:2-4; Yohana 4:24) Hata kidogo! Na ndiyo sababu Yesu anaongeza maneno haya kwenye masimulizi yake kuhusu matukio ya siku hizi: “Mambo hayo yaanzapo kutokea, jiinueni wenyewe wima na kuinua vichwa vyenu juu, kwa sababu wokovu wenu unakaribia.” (Luka 21:28, NW) Yesu anatuambia tuchukue hatua inayofaa, nia yenye maoni mazuri kuhusu hali mbalimbali zinazotuzunguka kwenye huu “umalizio wa taratibu ya mambo.”​—Mathayo 24:3-8, 33, NW.

5. Tunalazimika kuishi ndani ya ulimwengu wa namna gani, hata hivyo twapaswa kuwa na maoni gani?

5 Katika sehemu nyingi za ulimwengu si salama tena kutembea barabarani. Hesabu ya talaka inapanda juu sana, jamaa zinafarakana, na matumizi mabaya ya dawa za kulevya na ngono haramu zimefikia hesabu za juu sana. Huo ndio ulimwengu ambao waabudu wa Yehova wanalazimika kuishi ndani yake. Lakini ingawa tumo ndani ya ulimwengu, haitupasi kumezwa na ulimwengu. Kwa maana tunaweza kuwa na nia ile ile ya akili kama Yesu, ambaye alitangaza hivi: “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.”​—Yohana 16:33.

6. (a) Yesu aliweka mfano gani mzuri wa ‘kuushinda ulimwengu’? (b) Kwa sababu gani Yesu alitufundisha kusali “Ufalme wako uje”?

6 Kwa nini Yesu aliweza ‘kuushinda ulimwengu’? Ni kwa sababu yeye aliuamini kwa uthabiti ufalme wa Mungu ulioahidiwa. Yeye alijua kwamba Yehova angeuleta Ufalme huo kwa wakati Wake mwenyewe na kwa njia yake. Yesu alithamini sana mgawo wake wa kuwa Mfalme-mkusudiwa. Ili aupate Ufalme huo, yeye aliacha kila kitu ambacho angaliweza kuwa nacho akiwa mwanadamu mkamilifu duniani. Yeye pia anataka sisi tufurahie baraka za Ufalme. Ni kwa sababu hiyo Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali hivi: “Ufalme wako uje.” (Mathayo 6:9, 10) Karne nyingi ambazo zimepita, mamia ya mamilioni ya wanadamu wameisema sala hiyo. Lakini jamani! ni wachache namna gani wanaoifahamu maana halisi ya Ufalme huo!

Ule Ufalme​—ni Halisi

7. (a) Ni ulinganifu gani unaotusaidia kuthamini kwamba ufalme wa Mungu ni halisi? (b) Watawala wa Ufalme huo wanachaguliwaje, na ni kwa sababu gani tunaweza kuwa na hakika kwamba wataangalia faida za wanadamu kikweli?

7 Ufalme wa Mungu ni ufalme ambao uko kweli kweli. Kama vile tulivyo bado na falme za kibinadamu, kama vile serikali ya Tanzania, Uganda, Kenya na nyingine nyingi, ndivyo ufalme wa Mungu ulivyo mpango halisi wa kiserikali. Kama vile falme za dunia zenye mabunge, maseneti au wajumbe waliochaguliwa, ndivyo ufalme wa mbingu ulivyo na Yesu akiwa ndiye Mfalme aliyewekwa na Mungu, pamoja na watawala wenzake waliochaguliwa. Lakini katika habari yao, wao wamechaguliwa na Mungu mwenyewe kati ya wanadamu wenye sifa ya kutumainiwa. Wao ni “wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao.” (Wakolosai 3:12) Mungu mwenyewe ndiye anajua zaidi ya watu wote ni sifa gani zinazotakika katika watawala wenye haki, ili wapate kutimiza mambo yenye kufaidi wanadamu kweli kweli. Baada ya kufufuliwa kwao waingie katika ule ufalme wa kimbingu, watawala hawa wa kimbingu 144,001 watakuwa katika mahali penye kuwafaa sana katika maarifa ya kuweza kuyasimamia mambo ya makao ya Ufalme duniani.​—Ufunuo 14:1.

8, 9. (a) Kwa sababu gani Jumuiya ya Wakristo inashindwa kufundisha kwamba Ufalme huo una raia? (b) Lakini raia hao ni nani, na wanaweza kufurahia ahadi gani za Biblia? (c) Ni nani peke yao leo wanaotangaza “habari njema,” na unaweza kuwa na furaha gani leo?

8 Basi, ni nani watakaokuwa raia za Ufalme huo? Kama ungekwenda kwenye dini za Jumuiya ya Wakristo ukapewe jibu, wao wangekuambia kwamba hakutakuwa na raia kama hao. Zinafuata falsafa ya Kigiriki kwamba nafsi zote zina hali ya kutokufa, na kwamba ama zinakwenda “mbinguni” au kwenye “moto wa mateso.” Haziamini ahadi nzuri sana ya Biblia ya ufufuo wa kidunia, na kwamba Mungu ‘atakuwa na maskani’ pamoja na wanadamu na ‘kufuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena.’ (Yohana 5:28, 29; Ufunuo 21:3, 4) Ndiyo, raia za Ufalme huo watakuwa mabilioni ya wanadamu watakaoishi milele katika paradiso ya duniani pote papa hapa katika dunia hii. Na kati ya dini zote duniani, Mashahidi wa Yehova peke yao ndio wanaowaambia watu wa dunia hizi “habari njema.”​—Zaburi 37:9, 29.

9 Iwapo umekwisha kuzikubali “habari njema,” je, wewe hufurahi kwamba mtu fulani alikuja kushiriki nawe tumaini hilo? je! wewe hufurahi sana kujua mambo ambayo ufalme wa Mungu utawafanyia wanadamu? Je! hufurahi kwamba, kwa kuyatazamia mambo yote ambayo Ufalme utayatimiza, unaweza kushiriki sehemu fulani katika kulitakasa jina tukufu sana la Mtoaji wa ufalme huo, Mungu wetu, Yehova? Hakuwezi kuwako pendeleo kubwa leo kuliko kuzihubiri “habari njema hizi za ufalme” kwa wanadamu wengine wenye uhitaji!—Mathayo 24:14; Zaburi 145:10, 11.

Sala Yetu ya Shauku

10. Kuhusiana na Ufalme huo, kwa sababu gani tunapaswa kutoa sala ya shauku, na tukiwa na uhakika gani?

10 Basi tunapaswa kuwa wenye shauku kama nini katika kusali kwa ajili ya jina la Mungu litakaswe kupitia kuja kwa ufalme wake! Tunapaswa kuwa na hakika kama nini kwamba Ufalme huo ‘utakuja’ karibuni, ili utimize mapenzi ya Mungu kwa dunia yetu! Pia, tukiwa tumekwisha kuwa watumishi wa Mungu waliojiweka wakf na kubatizwa, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atajibu sala zetu za riziki ya kila siku, za msamaha wa dhambi zetu, na za ulinzi kutokana na hila za yule “joka” wa zamani, Ibilisi. Hayo ndiyo mambo ambayo Yesu alitufundisha tusali.​—Mathayo 6:9-13; Ufunuo 12:9.

11. Kwa sababu ya matatizo ya ulimwengu, ni shauri gani la Paulo la wakati wake linalofaa, na kwa sababu gani?

11 Hakika ni ulimwengu mkatili na mkali, ambao katika huo vichwa vya jamaa wanaona kuwa vigumu zaidi na zaidi kukabiliana na infuleshoni yenye kupanda juu sana na matatizo mengine ya kiuchumi. Na sikuzote tunahitaji kulinda ili tusiangushwe katika njia ya kiroho au ya adili na mashambulio ya adui. Kwa kupatana na shauri la mtume Paulo katika Waefeso 6:11-18, ‘kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika roho.’ Kwa maana ni hakika Mungu atajibu sala za watu wake waliojitoa—sala zinazopatana na mapenzi yake.​—Zaburi 65:2, 4, 5.

12. Kwa sababu gani Ufalme huo utajwe kama jambo kuu katika sala zetu?

12 Kwa moyo wote, na tusali hivi, “Ufalme wako uje.” Na kwa nini Ufalme huo utajwe kama jambo kubwa sana katika sala zetu? Kwa sababu hiyo ndiyo njia ya Mungu, chombo chake cha kuuondolea kabisa uumbaji wote yule adui mkubwa zaidi wake na wote wanaojiweka chini ya Shetani atawale maisha zao. Ufalme wa Kimasihi ni mpango Wake ambao utaliondolea jina lake lililo zuri sana malawama yote ambayo limemwagiwa muda wote wa karne 60 zilizopita. Ufalme utakaokuwa mikononi mwa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, utawatolea wanadamu uwezo wenye kukomboa wa dhabihu ya Yesu, hata ufufue mabilioni ya wale ambao sasa wamelala usingizini katika makaburi. (1 Timotheo 2:3-6; Ufunuo 20:12) Je! wewe unahuzunika sana kwa kufiwa na mpendwa fulani? Je! unahuzunishwa na hali zenye kuharibika sana za ulimwengu? Basi, je, hufurahi kwamba unaweza kuwa sehemu ya watu pekee ulimwenguni ambao tumaini lao ni katika Yehova na ahadi zake tukufu za Ufalme? (Zaburi 144:15; 146:5) Unapaswa kufurahi! Na kwa uhakika unapaswa kuwa ukiomba hivi, “Ufalme wako uje.”

YATAKAYOTIMIZWA NA ‘KUJA’ KWA UFALME

□ Kuondoa uovu, vita, uonezi

□ Kuwaokoa wote wanaomwabudu Mungu “katika roho na kweli”

□ Kuleta serikali halisi yenye wasimamizi waliochaguliwa na Mungu

□ Kufufua wafu, kuunganisha jamii zote za kibinadamu ziwe raia wa kidunia wa Ufalme huo

□ Mahali pa umaskini na ufisadi ulete fanaka, haki ya hukumu kwa wote

[Picha katika ukurasa wa 14]

Kama vile serikali za kibinadamu zilivyo halisi, ndivyo ilivyo serikali ya Ufalme wa kimbinguni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki