Kilifanya “Mwujiza”
Mwanamke mwenye umri wa miaka 29 aliandika hivi: “Mimi sina watoto lakini dada yangu ana watoto wawili wa kiume. Kwa kuwa yeye ni mtu asiyeamini Mungu yuko, mimi sikufikiri angechukua Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, lakini yeye akakichukua bila kukitaka hata kidogo. Nilikuwa nimejaribu kumtolea sababu za kumwonyesha Mungu yuko lakini hiyo ikawa kazi bure. Majuma machache baada ya mimi kumpa kitabu hicho cha Hadithi za Biblia yeye aliniita akasema amekisoma kutoka jalada mpaka jalada.”
Matokeo yakawa nini? “Sasa yeye anachukua vitabu vyetu vinavyohusu Biblia,” ndivyo dada yake anavyosimulia. “Kitabu hiki cha kupendeza ndicho kilichofanya mwujiza huo hivi kwamba sasa mimi nina tumaini kubwa zaidi kwamba siku moja yeye atampenda Baba yetu wa kimbingu pamoja nami.”
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kimekuwa kikisaidia mamilioni ya watu wapate ufahamu mzuri zaidi juu ya Neno la Mungu. Kina masimulizi ya Biblia 116 yanayompa msomaji wazo la mambo yaliyo katika Biblia. Kitabu chenyewe kimeandikwa kwa herufi kubwa na kina picha zaidi ya 125, na hesabu kubwa kati yazo zina rangi yakupendeza. Wewe unaweza kupokea kichapo hiki chenye thamani kubwa cha kurasa 256 kwa kujaza na kutuma hati yenye anwani iliyo hapa chini.
Tafadhali mnipelekee kile kitabu chenye jalada gumu kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Ninyi mtanilipia malipo ya kukipeleka kwa njia ya posta. Mimi nimewapelekea Kshs. 30/- (Tshs. 50/-).