Upendo wa Kikristo Wenye Matendo
UFILIPINO ni nchi inayokumbwa mara nyingi na tufani na mvua nzito za majira kwa majira ambazo mara kwa mara zinafanya kuwe na mafuriko makubwa. Nyakati kama hizo kinachothaminiwa sana ni upendo wa Kikristo wenye matendo, kama linavyoonyesha jambo hili lililoonwa.
Katika eneo la kusini la baraza la mji wa Carmen, Davao del Norte, Mashahidi wa Yehova katika Kundi la Mabuhay hawakupata hasara kubwa sana kutokana na mafuriko. Walakini, bila kukawia walitimiza mahitaji ya ndugu zao Wakristo katika mji huo katika sehemu ambayo kwa kweli ilipata hasara. Mchele na vyakula vingine vilikusanywa na kupelekwa huko. Akina ndugu wa eneo lenye kuhusika walipotimiziwa mahitaji yao, vyakula vilibaki vingi sana mpaka maafisa wa mji wakapewa mabaki hayo ili watu wengine wenye uhitaji wagawiwe.
Tendo hilo la upendo la kuwahangaikia watu hao lilisukuma maafisa wa mji kufanya azimio la kusifu Mashahidi wa Yehova. Kwa ufupi, azimio hilo linasema hivi:
“KWANZA, Mashahidi wa Yehova wa Mabuhay, . . . walipojua shida ya wenye kupatwa na hasara ya mafuriko katika eneo hili la baraza la mji, . . . walitoa usaidizi wa chakula bila kukawia ili kuwapunguzia magumu yao na msiba wao;
“NA IAZIMIWE, . . . kupitisha Azimio lenye kupiga asante na shukrani kubwa kabisa kwa Mashahidi wa Yehova wa Mabuhay . . . kwa sababu ya usaidizi wa chakula ambao wamewapa wenye kupatwa na hasara ya mafuriko.”
Ni jambo la kuchangamsha sana moyo kusikia habari za Wakristo wa kweli ambao katika nyakati za shida wanachukua hatua, si ya “maneno na kusema-sema” tu bali ya “upendo wa kweli, ambao unajionyesha wenyewe kwa matendo”!—1 Yohana 3:18, Today’s English Version.