Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 10/15 uku. 16
  • Upendo wa Kikristo Wenye Matendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo wa Kikristo Wenye Matendo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Kukua Pamoja Katika Upendo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Endelea Kutembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Furiko Katika Hekaya za Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 10/15 uku. 16

Upendo wa Kikristo Wenye Matendo

UFILIPINO ni nchi inayokumbwa mara nyingi na tufani na mvua nzito za majira kwa majira ambazo mara kwa mara zinafanya kuwe na mafuriko makubwa. Nyakati kama hizo kinachothaminiwa sana ni upendo wa Kikristo wenye matendo, kama linavyoonyesha jambo hili lililoonwa.

Katika eneo la kusini la baraza la mji wa Carmen, Davao del Norte, Mashahidi wa Yehova katika Kundi la Mabuhay hawakupata hasara kubwa sana kutokana na mafuriko. Walakini, bila kukawia walitimiza mahitaji ya ndugu zao Wakristo katika mji huo katika sehemu ambayo kwa kweli ilipata hasara. Mchele na vyakula vingine vilikusanywa na kupelekwa huko. Akina ndugu wa eneo lenye kuhusika walipotimiziwa mahitaji yao, vyakula vilibaki vingi sana mpaka maafisa wa mji wakapewa mabaki hayo ili watu wengine wenye uhitaji wagawiwe.

Tendo hilo la upendo la kuwahangaikia watu hao lilisukuma maafisa wa mji kufanya azimio la kusifu Mashahidi wa Yehova. Kwa ufupi, azimio hilo linasema hivi:

“KWANZA, Mashahidi wa Yehova wa Mabuhay, . . . walipojua shida ya wenye kupatwa na hasara ya mafuriko katika eneo hili la baraza la mji, . . . walitoa usaidizi wa chakula bila kukawia ili kuwapunguzia magumu yao na msiba wao;

“NA IAZIMIWE, . . . kupitisha Azimio lenye kupiga asante na shukrani kubwa kabisa kwa Mashahidi wa Yehova wa Mabuhay . . . kwa sababu ya usaidizi wa chakula ambao wamewapa wenye kupatwa na hasara ya mafuriko.”

Ni jambo la kuchangamsha sana moyo kusikia habari za Wakristo wa kweli ambao katika nyakati za shida wanachukua hatua, si ya “maneno na kusema-sema” tu bali ya “upendo wa kweli, ambao unajionyesha wenyewe kwa matendo”!—1 Yohana 3:18, Today’s English Version.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki