‘Yalisaidia Ndoa Yetu’
HAYO ni maelezo ya Glenn, mwanamume wa huko Louisiana. “Mimi nilipokutana na Glenn mara ya kwanza,” anaandika mmoja wa Mashahidi wa Yehova “alikuwa chini ya gari lake la kuchukulia mizigo, lakini alitoka hapo chini akayasikiliza vizuri mahubiri yangu. Yeye alikubali bila kipingamizi kufanya uandikishaji awe akiyapokea magezeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Majuma mengi yalipita kabla hatujaweza kupata tena mtu ye yote nyumbani. Mwishowe tukakuta mke wake, naye akasema: ‘Ndiyo, yeye aliniambia alifanya uandikishaji awe akipokea magazeti hayo. Mimi nilishangaa kwa sababu kawaida yake hapendi kuandikisha magazeti hayo. Lakini yameanza kufika nayo ni mazuri kama nini! Tunayasoma pamoja usiku. Yatakapoacha kuja, hakika tutaandikisha upya tuwe tukiyapokea!’
“Tulipanga kurudi tena wakati ambao mume na mkewe wangekuwa nyumbani, nao walikuwa wakitungojea wakati tulioupanga. Tukaanzisha funzo la Biblia. Glenn alisema hivi: ‘Hakika magazeti hayo ni mazuri. Yamekwisha saidia ndoa yetu. Siku hizi nikirudi nyumbani kwenye chakula cha mchana, mimi humwuliza Rebeka kama gazeti jingine limefika.’”
Hata wewe unaweza kupata majarida mawili haya yenye kuitegemea Biblia kwa kujaza hati yenye anwani iliyo hapa kisha uitume.
Tafadhalini mnipelekee uandikishaji wa mwaka mmoja wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni!; nimewapelekea Kshs. 50/- (Tshs. 100/-, RWF 500).